Vietnam yaanzisha Idara ya kuoza binti zake nchi za nje!

Vietnam yaanzisha Idara ya kuoza binti zake nchi za nje!

Iga

Senior Member
Joined
Dec 17, 2007
Posts
112
Reaction score
6
WAKATI Tanzania imehamanika na hali mbaya ya kifedha ilizokumba mabwana zake nje na haina mkakati unaoeleweka wa kunusurika bila mabwana zake kunusurika kwanza Vietnam nchi ambayo jana na juzi ilikuwa 'Gza' mara mia ya hii ya leo imekuja na mpya.

Baada ya kuona wasichana wao wanaolewa katika fungate zinazoishia binti hao kunyanyaswa na kugeuzwa jamvi la wazungu huko Ulaya wao wamekwenda hatua moja mbele kwa kuzindua idara maalum ya kupokea posa toka kwa watu wa nje wanaotaka kuoa binti wazuri na poteboo wa Kivietnam.

Sijui JF kama wajumbe wana wazo la kibiashara hapa au kutuonesha uzuri tu, lakini uzuri ebo, weye bwana hauliwi eti!

Hili linatufundisha jambo moja kwamba tukiwa watundu tunaweza kufanya biashara ya rasilimali watu.

Una habari kwamba Cuba inapata sio chini ya bilioni 500 kila mwaka kwa kukodisha madaktari, wanajeshi, walimu na wahandishi nchi za nje?

Amkeni hii ni saa 5 asubuhi sio 11 jamani?
 
WAKATI Tanzania imehamanika na hali mbaya ya kifedha ilizokumba mabwana zake nje na haina mkakati unaoeleweka wa kunusurika bila mabwana zake kunusurika kwanza Vietnam nchi ambayo jana na juzi ilikuwa 'Gza' mara mia ya hii ya leo imekuja na mpya.

Baada ya kuona wasichana wao wanaolewa katika fungate zinazoishia binti hao kunyanyaswa na kugeuzwa jamvi la wazungu huko Ulaya wao wamekwenda hatua moja mbele kwa kuzindua idara maalum ya kupokea posa toka kwa watu wa nje wanaotaka kuoa binti wazuri na poteboo wa Kivietnam.

Sijui JF kama wajumbe wana wazo la kibiashara hapa au kutuonesha uzuri tu, lakini uzuri ebo, weye bwana hauliwi eti!

Hili linatufundisha jambo moja kwamba tukiwa watundu tunaweza kufanya biashara ya rasilimali watu.

Una habari kwamba Cuba inapata sio chini ya bilioni 500 kila mwaka kwa kukodisha madaktari, wanajeshi, walimu na wahandishi nchi za nje?
Amkeni hii ni saa 5 asubuhi sio 11 jamani?


Mzee hebu tupe source ya habari yako. Especially hii ya kwamba Cuba wanaingiza Dollar 500 billion every year. It sound to much to be true!!!!???? Unless siyo USD since hukutaja ni hela gani!!!!!!!!

Mihela yote hiyo kwenye poplulation ya watu kama 10 million halafu bado hujaongeza vyanzo vingine. Nafikiri hiyo figure inabidi uiangalie vizuri la sivyo jamaa wasingekuwa wanasota.
 
Anoher post with no source/link.

Did you hear this from your boy?

If not please provide links to your sources. Especially your claims on Cuba.
 
Oh please!!! That's legalizing human trafficking!
 
WAKATI Tanzania imehamanika na hali mbaya ya kifedha ilizokumba mabwana zake nje na haina mkakati unaoeleweka wa kunusurika bila mabwana zake kunusurika kwanza Vietnam nchi ambayo jana na juzi ilikuwa 'Gza' mara mia ya hii ya leo imekuja na mpya.

Baada ya kuona wasichana wao wanaolewa katika fungate zinazoishia binti hao kunyanyaswa na kugeuzwa jamvi la wazungu huko Ulaya wao wamekwenda hatua moja mbele kwa kuzindua idara maalum ya kupokea posa toka kwa watu wa nje wanaotaka kuoa binti wazuri na poteboo wa Kivietnam.

Sijui JF kama wajumbe wana wazo la kibiashara hapa au kutuonesha uzuri tu, lakini uzuri ebo, weye bwana hauliwi eti!

Hili linatufundisha jambo moja kwamba tukiwa watundu tunaweza kufanya biashara ya rasilimali watu.

Una habari kwamba Cuba inapata sio chini ya bilioni 500 kila mwaka kwa kukodisha madaktari, wanajeshi, walimu na wahandishi nchi za nje?

Amkeni hii ni saa 5 asubuhi sio 11 jamani?

Demand ya wasichana wa kivietnam ni kubwa sana kwa nchi za west. Kuna imani kuwa wanatoa mapenzi sana na siyo wafujaji wa pesa. Wanasheria wengi na makampuni ya kuunganisha wapendanao (dating agencies) yamekuwa yanavuna hela sana kwa kuunganisha na kuozesha mabinti wa kivietnam; google "Vietnamese women" "dating vietnamese" au "marrying vietnamese" uone.

Sioni vibaya kama serikali yao nayo itaamua kuwa inapata mgao kidogo kutokana na mapato hayo yaingiao mifukoni mwa wanasheria na hizo dating agencies hasa kwa vile mabinti hao wataendelea kuolewa nje kila kukicha. Kuhusu ushuri wako, sidhani kama unaweza kutekelezwa hapa kwetu kwa hakuna uhakika kuwa dada zetu nao wanapendwa kwa kiasi hicho huko nchi za nje, hasa kwa jinsi wanavyopenda matanuzi. Inawezekana huo ukawa ukiritimba utakoongeza gharama za serikali bila faida yoyote.
 
Pia wajanja toka nchi tajiri za Asia ya mbali kama Japan na Taiwan, zaidi ni S. Korea, wamekuwa wakiwatapeli wasichana kwa ndoa lakini wakiwapeleka huko kwao wanaingizwa kwenye biashara ya ukahaba au KARAOKE. Mume atajitambulisha kama anaishi Seoul kumbe anatoka Vijijini, tajiri kumbe kwa viwango vya S Korea ni masikini tu. Utalii na Internet ndo chanzo kikubwa cha kuongezeka kwa ndoa hizi na utapeli. Hivyo moja ya sababu mojawapo ya Vietnum kuanzisha idara ni kulinda raia wake wasitapeliwe maana pia ni kweli kuna waoaji wa kweli, hasa S. Korea ambako vijijini si rahisi kupata mke kwani wamekimbilia Mjini halafu hawatosheki. Wakorea wengi wanapenda kuoa Vietnum kuliko China kwani wasichana wa huko ni waumini wazuri, wafanyakazi (hata kwa penzi si wavivu), hawana makuu, ni potable, ni njano kama wao, waaminifu na ndoto yao ya kwenda huko S. Korea nk inakua imekamilika kwa kutumia marriage cover.
 
Back
Top Bottom