Vifaa vya maji safi na salama vyakabidhiwa Jimbo la Gando

Vifaa vya maji safi na salama vyakabidhiwa Jimbo la Gando

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301
JIMBO LA GANDO KUNUFAIKA NA VIFAA VYA MAJI SAFI NA SALAMA

Mbunge wa Jimbo la Gando Mhe. Salim Mussa Omar amesema kwamba amemtuma Katibu wa Ofisi ya Mbunge Jimbo la Gando Ndugu Mshani Ali Kachinga kukabidhi vifaa mbalimbali vya Maji katika Shehia tano vyenye thamani ya Shilingi Milioni 4,800,000.

Ndugu Mshani Ali Kachinga akishirikiana na viongozi wa CCM amekabidhi kwa wananchi vifaa, Matenki ya kuhifadhi Maji, Mashine za kupandisha Maji na Mipira Roli 7 katika Shehia Tano za Gando, Junguni, Kizimbani, Kinyasini na Magogoni.

Vifaa hivyo mbalimbali vya Maji Safi na Salama vina thamani ya Shilingi Milioni 4,800,000 ambavyo vimekabidhiwa mnamo tarehe 21 Mei, 2023 Viwanja vya Ukumbi wa Dolphin Bopwe, Wete, Pemba.

#GandoMpya

WhatsApp Image 2023-05-24 at 23.37.13.jpeg
WhatsApp Image 2023-05-24 at 23.37.13(1).jpeg
WhatsApp Image 2023-05-24 at 23.37.14.jpeg
WhatsApp Image 2023-05-24 at 23.37.14(1).jpeg
WhatsApp Image 2023-05-24 at 23.37.14(2).jpeg
 
Back
Top Bottom