Vifo vya ajali ya meli Congo vyafikia watu 78

Vifo vya ajali ya meli Congo vyafikia watu 78

Wapumzike salama waliofariki ila najiuliza Congo kuna laana gani mbona kila janga wao!? Treni yao wanapanda na wanyama na wanakaa juu ya mabehewa, meli zao ni hivyohivyo pia! Kuna namna ile jamii inapaswa kuelimishwa istaarabike.
Huwa nabishana na watu msimamo wangu ni matatizo ya Congo hayatokani na wazungu. Wazungu wamekuja kutokana na mwaya ulioachwa wazi na tabia za hawa Waafrika wenzetu. Congo sijui ina laana gani kila kitu wanafanya vibaya.

Nchi kila siku inalalamika kuteswa na Rwanda wakati ka-Rwanda kanazidiwa na mkoa wa Tabora.
Hivi nchi kubwa kama Congo inashindwa kulinda mpaka wa eneo dogo linalozidiwa na Tabora asitoke kitu au kuingia kitu bila uangalizi wao.
 
Tragic ila wamekufa kiboya. Walilazimishwa kujazana hivyo kwenye boat?
 
Wapumzike salama waliofariki ila najiuliza Congo kuna laana gani mbona kila janga wao!? Treni yao wanapanda na wanyama na wanakaa juu ya mabehewa, meli zao ni hivyohivyo pia! Kuna namna ile jamii inapaswa kuelimishwa istaarabike.

Hakuna laana bali ujinga umetamalaki. Ku overload boat ni ujinga sio laana. Ujinga kwa wamiliki na abiria wenyewe.
 
Kituo cha uokoaji , hawa ambao walichukua kwa simu wangetoa taarifa fasta.
Una uhakika waokoaji wangefika kwa wakati na kufanya la maana? Usisahau hata sisi tukio kama hili limewahi kutukumba pale ukerewe kwa mv nyerere. Mkuu wa mkoa aliamrisha waokoaji wakalale waje tena kesho yake.
 
RIP.

Africa maisha ya mtu hayana thamani kwa sababu.

1. Watu ni wengi sana na wanazaliana sana. Kwa kutumia kanuni za kawaida za uchumi supply and demand thamani ya kitu hushuka kinavyozidi wingi.

2. Kwenye vyombo vya usafiri kama hivi, hakuna vyombo vya kutosha, watu wanajazana bila kujali usalama wao. Wao wenyewe hawajali usalama wao na wanachangia kujiweka hatarini.

3. Elimu iko chini kwa watu wengi. Watu hawafikirii kuwa kujazana sana kwenye chombo kunaweza kusababisha kuzama, mambo kama ukarabati wa vyombo ni nadra na watu wanaenda kwa kudra kudra tu. Yote haya ni kwa sababu ya kukosa elimu.

4. Serikali hazifanyi kazi zake kuwajibika kuwapa wananchi huduma za kijamii kuendana na mahitaji yao. Viongozi wa serikali ni kama maharamia waliokaa kukusanya kodi na kujinufaisha wenyewe zaidi.

Mimi sishangai ajali hii kutokea, nashangaa kwa nini ajali kama hizi hazitokei mara nyingi zaidi. Naomba nieleweke kuwa sisemi natamani ajaki zitokee zaidi, nasema nashangaa kwa nini ajali kama hizi hazitokei zaidi.
Mwendokasi tu watu wanajaza kama nyanya kwenye matenga

Ova
 
Wengine utawaonea, ila wenye dhamana mkuuu
Wapumzike salama waliofariki ila najiuliza Congo kuna laana gani mbona kila janga wao!? Treni yao wanapanda na wanyama na wanakaa juu ya mabehewa, meli zao ni hivyohivyo pia! Kuna namna ile jamii inapaswa kuelimishwa istaarabike.
,
 
Back
Top Bottom