Vijana acheni pombe na Energy drinks, mwifwa

Vijana acheni pombe na Energy drinks, mwifwa

Magonjwa yasiyo ya kuambukizwa mfano moyo, kiasukari presha na saratani yanakua na risk factors nyingi ikiwemo
👉Umri
👉mtindo wa maisha
👉Genetics
Na tunajua risk factors sio chanzo cha moja kwa moja bali ni mambo ambayo ukiyafanya yanaweza kukuelekea ukapata magonjwa hayo

Mtu anaweza asiwe na umri mkubwa na mtindo wake wa maisha ni wa kawaida sio sedentary lifestyle, anapiga zoezi vizuri lakini akapata kisukari akapata pia saratani na hata (cardiac diseases) juzi tu tumesolve kesi moja mtoto wa miaka miwili ana myocardial infraction. Ila anaendelea vema
Hapo kuna factor moja imebaki ambayo ni genetics.
Kuhusu energy drinks na kuleta magonjwa ya moyo probably inaweza sababisha lakini inaingia hapo kwenye mtindo wa maisha.
Energy drink ni kwaajili ya kupunguza fatigue ikiwa kuna ulazima wa kuendelea kufanya kazi na ingredient yake kubwa ni caffeine, ambayo pia unaipata kwenye kahawa na alkaloids zingine. (kwa waliokutana na pharmacognosy wataelewa nini namaanisha )ikitumiwa kiasi sidhani kama inaweza leta ugonjwa wa moyo, na tunajua too much is harmful.

Hapo juu nimeona kuna member anakunywa energy 6 kwa siku
Wanachuo wanakunywa energy na skonzi😂 hio ndio chai pia mtu anakunywa energy drink kisha anaenda kulala😂😂 for what?
Kwa staili hio tutapona kweli?
All in all too much is harmful

Dkt. Gwajima D
Dr Restart
DR Mambo Jambo
Dr am 4 real PhD

Mnaweza ongeza jambo hapa.
Sasa majibu muda wote mnayo mnaangalia tu watu wanabishana. Enzi zetu tulikuwa tunakunywa red bull ila tulikuwa tunasema moja tu kwa wiki,sijui tulitoa wapi hii idea.
Ila shida sasa vijana wanakunywa hizi energy drink kama substitute ya maji na juice/soda. Mtu asubuhi ananunua maandazi na Mo energy, mchana chapati na Mo energy na usiku tena kabla hajalqla anakunywa nyingine ni hatari.
 
Imagine Real energy drink kama Redbull inauzwa 3000 hizi za kwetu eti 500 really?? Kuna kupona kweli hapo? Halafu mtu anaagiza na smart gin ya 2000 anapiga mixer daaah
Itakuwa we si unaona redbull packaging yake?! Halafu inatoka nje tofauti na hizi za kwetu.
 
Nimesoma gazeti la Mwananchi jana lenye kichwa cha Habari ukurasa wa mbele kisemacho
Pombe, 'energy drinks' zinavyomaliza vijana

Kwa mujibu wa hili gazeti wakinukuu wataalamu wa afya wa Hospitali ya Benjamin Mkapa Dodoma ni kwamba:-

1. Vijana Wanne hadi Tisa hufika Hospital hiyo kila wiki Figo zikishindwa kufanya kazi.

2. Watanzania 10 kati ya 100 wana tatizo la Figo

3. Wahanga ni vijana umri kati ya 24-40

4. Gharama za kusafisha Figo kwa mwaka ni wastani wa TZS 31,200,000 Hadi 46,800,000 bila kuweka gharama nyingine kv usafiri

5. Energy drinks ni disaster kwenye moyo kwa mujibu daktari bingwa wa JKCI.

6. Matumizi ya vinywaji hivi yanaathiri pakubwa viungo vitatu ambavyo ni
-Ini,
  • Figo na
  • Moyo.

7. Wahanga wakubwa ni vijana wa kiume.

MY TAKE:

Vijana acheni pombe, taifa linawategemea. Linda afya yako. Afya ni mtaji.
Energy drink zina addiction mbaya sana ukizama hutoki

Sent from my SM-A037F using JamiiForums mobile app
 
Hayo yote ni Ile hali ya kutokuwa na kiasi.
Lack of ability to say no!

Kikubwa vijana na watu wote wafuate utaratibu wa ulaji na unywaji kupitia muongozo wa vitabu vya waadventista wasabato.
Ellen G white books👇
Counsels on Diet and Foods
Counsels on Health
The health food ministry
Healthful Living
Temperance
The place of herbs in Rational therapy
 
Imagine Real energy drink kama Redbull inauzwa 3000 hizi za kwetu eti 500 really?? Kuna kupona kweli hapo? Halafu mtu anaagiza na smart gin ya 2000 anapiga mixer daaah
Ikifika tumboni inahamisha maini inayaweka kwenye figo nyingine inaenda kichwa cha juu inatriga button ya matusi na kuendesha bodaboda kama chizi
 
Hayo magonjwa yapo sana tu lakini sio lazima kuwa chanzo ni pombe na hizo energy drink

Hayo magonjwa yapo sana tu lakini sio lazima kuwa chanzo ni pombe na hizo energy drink
Piga lifaru john limoja mwanawane lisipotosha jazilizia na kasichana. tunaishi mara 1, hawa wanatutisha tu
 
Ndo ukweli huo. Tafuta gazeti la Mwananchi la jana Machi 15, 2024 wameandika kwa kina sana...inaonekana unywaji pombe ni tatizo sana hasa kwa Vijana, ushahidi ni ukienda wikiendi Tabata, Kitambaa, Rainbow etc
Hivi kitambaa cheupe ya tabata wameshaitengeneza baada ya kuungua?
 
Ndo ukweli huo. Tafuta gazeti la Mwananchi la jana Machi 15, 2024 wameandika kwa kina sana...inaonekana unywaji pombe ni tatizo sana hasa kwa Vijana, ushahidi ni ukienda wikiendi Tabata, Kitambaa, Rainbow etc
Hivi kitambaa cheupe ya tabata wameshaitengeneza baada ya kuungua?
 
Back
Top Bottom