Tetesi: Vijana aliokuja nao Lipumba wapo waliotumika na Masaburi Ubungo

Tetesi: Vijana aliokuja nao Lipumba wapo waliotumika na Masaburi Ubungo

Dah! Kishanunuliwa huyu na ukoo wa mapanya na mafisi. Aibu mtindo mmoja ila wataendelea kumtumia ili alete mtafaruku ndani ya CUF na pia hata UKAWA.

Kati ya vijana alioambatana nao Profesa Lipumba kuja ukumbi wa mkutano mkuu wapo ambao wametambulika kuwa wakati wa uchaguzi mkuu 2015 walitumika na Didas Masaburi katika uchaguzi wa kiti cha Ubunge Ubungo kama vijana wa kuanzisha fujo mbalimbali ikiwemo yale maandamano feki eti ya kumtaka Dr Slaa arejee nafasi yake.
Mmoja wapo aliyetambulika kwa jina moja tuu la Ayubu amekuwa akionekana mara kwa mara ofisini kwa Makonda bila kueleweka anatafuta nini. Hii inaleta mashaka kuwa vurugu za kutaka kurejea madarakani za Lipumba ni mpango unaodhaminiwa na watu nje ya CUF na kwa makusudi maalum, ukizingatia kuwa aliachia ngazi kwa hiari yake na sio kwa kushinikizwa.
 
Kichekesho wanaompinga lipumba ukiwafuatilia wana element za kiuchadema...
 
Kichekesho wanaompinga lipumba ukiwafuatilia wana element za kiuchadema...
Kwa hiyo ile 92% ya wajunbe wa mkutano mkuu wakiompinga Lipumba kwenye mkutano mkuu wana elements za Chadema?
Muwe na fikra guru kabla ya kusema kitu
 
Hahaha mpango ulisukwa Monduli kuinunua cuf imegoma
Hapa kinachozungumziwa ni Fuji za Vijana wa Lipumba walioleta Fujo. Hayo ya kununua chama ni yenu wenye fikra fupi.
Na kwa nini Ccm mnatapambana arudi?
 
Kila nikimuangalia profesa namwona dk rutengwe yule dc wa morogoro, maana lipumba nje cuf hana kitu kingine anachoweza kufanya ndiyo maana sishangai japo ana elimu kubwa lakini anang'ang'ania kutumika na wanasiasa
Kuna kila Namna inahitajika wasomi kujiangalia katika kufanya maamuzi maana wengi wanajishusha thamani
 
Profesa ataenda wapi maana ccm nako awataki wasaliti aje kutubu tu dhambi ya usaliti ina mtesa
 
Kwa kajiutafiti kangu hapa kwa hoja za wana JF najitahidi kuwa neutral! CCM woote wanataka Lipumba Arudishiwe cheo chake, CHADEMA na ukawa kwa ujumla hawamtaki Lipumba!

Why? CCM inaonyesha ni Kweli walimtumia Lipumba hivyo wana matumaini kuwa watamtumia tena pindi wakihitaji, UKAWA wanaamini Lipumba ananunulika hivyo kutaka kurudi kwake ameshafika bei ili aje amalize kazi aliyoianza mwaka Jana!

CUF wako pamoja na UKAWA ila kundi la wafika bei wachache wako lamina na Prof.

End of my findings!!
 
Kati ya vijana alioambatana nao Profesa Lipumba kuja ukumbi wa mkutano mkuu wapo ambao wametambulika kuwa wakati wa uchaguzi mkuu 2015 walitumika na Didas Masaburi katika uchaguzi wa kiti cha Ubunge Ubungo kama vijana wa kuanzisha fujo mbalimbali ikiwemo yale maandamano feki eti ya kumtaka Dr Slaa arejee nafasi yake.
Mmoja wapo aliyetambulika kwa jina moja tuu la Ayubu amekuwa akionekana mara kwa mara ofisini kwa Makonda bila kueleweka anatafuta nini. Hii inaleta mashaka kuwa vurugu za kutaka kurejea madarakani za Lipumba ni mpango unaodhaminiwa na watu nje ya CUF na kwa makusudi maalum, ukizingatia kuwa aliachia ngazi kwa hiari yake na sio kwa kushinikizwa.
mengi tutayasikia ila mwisho wa siku unafiki uhaini usaliti matokeo yake ni aibu
 
Mchawi katumbuliwa kwa demokrasia 92% hawamtaki Lipumba
1471851739335.jpg
 
Lipumba aliahidiwa uwaziri wa fedha endapo asiyejaribiwa atashinda!! Baada ya asiyejaribiwa kushinda hakutimiza ahadi!! Mbaya zaidi mpaka aliyefanikisha kumshawishi Lipumba bwana Dau naye akatumbuliwa!!! Imekua ni Majuto!!!
hapa nakuamin
 
CHADEMA WANAJUWA WAZI AKITOKA TU LIPUMBA ITAKUWA RAHISI KUITEKA MWAMBAO AMBAKO HAWAKUBALIKI
Kwa hiyo wao ndio walinshawishi Lipumba ajiuzulu? Ccm mnapenda sana kujiingiza kwenye mambo ya ndani ya vyama vingine. Sasa hivi professa uchwara ameshakuwa dili kwenu.
Mikakati ya viwanda na ajira imewashinda sasa mumedandia CUF. Kilichotakiwa jana ni baada ya ile kura kumbwaga Lipumba na hao wafuasi wake kuleta zogo ni bakora tuu
 
Back
Top Bottom