Vijana kufanya Maandamano kupinga Mkataba wa Bandari kati ya Tanzania na kampuni ya DP World ya Dubai

Vijana kufanya Maandamano kupinga Mkataba wa Bandari kati ya Tanzania na kampuni ya DP World ya Dubai

I had to do a double take on this one!

Keshokutwa, Jumatatu, kuna watu wamepanga kuandamana jijini Dar kupinga mkataba wa bandarini na kupinga muswada/ sheria mpya ya TISS.

Ngoja nicheke kwanza….bwahahahaaaa.

Kwa niwajuavyo Watanzania, hapo ni kujisumbua na kupoteza muda tu.

Watanzania sisi ni waoga sana. Hatuna mwamko wowote ule ulio wa maana kwenye kupigania maslahi yetu.

Sisi ni watu wa kuburuzwa buruzwa tu kama kondoo.

Tunatoa heshima ya ki Mungu kwa viongozi wetu. Hata wakikosea hatuwatupii lawama zinazostahili.

Viongozi wakikosea, lawama hupewa washauri wa hao viongozi.

Kiujumla sisi ni waoga, ni makondoo, ni mafisi, wasahaulifu, na vivumishi vingine vinavyoelezea tulivyo.

Ukweli ni kwamba hili suala la bandari upepo wake ushaanza kupita. Kufikia mwisho mwa wiki ijayo, tayari litakuwa lishakua historia.

Sidhani kama hiyo Jumatatu kutakuwepo na mwitikio wowote ule wa maana kwenye hayo maandamano.

Sana sana wataojitokeza ni baadhi tu ya wanaharakati wa mitandaoni na vibango vyao viwili vitatu.

Kiufupi itakuwa ni kupoteza muda tu.

Ila, ikitokea kinyume na ninavyodhani, basi sitokuwa na hiana kukubali kuwa nilikosea.

Tusubiri tuone kitachojiri hiyo Jumatatu.

IMG_4461.jpeg
IMG_4460.jpeg
 
Kwani waliokamatwa kwa kuandamana wamehamasishwa na nani? Naona jamaa aliomba ulinzi wake peke yake!
 
Kimeumana!

Nimezipata za chini ya kapeti ya kwamba kuna uwezekano mkubwa wa vijana wa Dsm na wa Dodoma kuingia barabarani weekend hii au Jumatano ijayo kupinga issue ya DP World.

Mambo ni [emoji91][emoji91][emoji91][emoji91][emoji91][emoji91][emoji91]

Vijaaanaa vijana vijana tuko tayari kulitumikia, taifa, taifa, taifa kulitumikia Taifa Taifa Tanzania.

Dodoma = Assembling point ni pale Nyerere Squire

Dar = Ni Pale Mnazi mmoja kwenye mnara wa Mashujaa.

=========

UPDATES:

Kijana Deusdedith Soka aitisha Maandamano ya Amani tarehe 19 Juni, 2023 kuanzia Temeke kwenda Ikulu ya Magogoni kupinga mkataba kati ya DP World na TPA pamoja na kupinga Muswada wa TISS kuwekewa kinga ya kutokushtakiwa kwa makosa ya Jinai.


Deusdedith Soka afanya mkutano na waandishi wa habari kutoa maelezo kuhusiana na route itakayotumika siku ya Jumatatu, Juni 16 kwenye maandamano ya kupinga Mkataba wa Bandari kati ya Tanzaniana Dubai.

Hapa chini ni barua aliyoandika kuhusu maandamano ya Jumatatu 19, Juni 2023

Kupitia ukurasa wake wa Twitter, aliandika: “@tanpol Msije kujeruhi watu waacheni tudai haki zetu kwa njia ya kistaarabu na kiungwana. Maandamano ya amani, wanasheria kuweni macho kwa askari yeyote atakayevunja Haki za binadamu utashtakiwa mwenyewe.”


Hata hivyo, Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limetoa tahadahari kwa wananchi kuhusu taarifa za kuwepo na maandamano siku ya Jumatatu Juni 19, 2023 kwenda Ikulu ya Magogoni, Dar es Salaam. Zaidi, soma hapa.
Haya maandamano yameishia wapi MzeeKipusa ?😂
 
Haya maandamano yameishia wapi MzeeKipusa ?[emoji23]
Mimi huwa naona mambo kabla hayajatokea. Kiufupi mambo sio shwari kabisa!.

Vyombo vya ULINZI , USALAMA na POLISI , vijipange sana.


Note: Polisi sio chombo cha Ulinzi na Usalama. Vyombo vya Ulinzi na Usalama ni USALAMA WA TAIFA pamoja na JWT


POLISI ni Raia tu kama sisi, ni Sawa na JKT tu ( Raia wanaolipwa mishahara na Serikali kwà ajili ya kutulinda sisi na mali zetu )

POLISI ni Sawa na wale walinzi wa nzego...ambao huchangiwa af5 5 KILA mwezi.
 
Mimi huwa naona mambo kabla hayajatokea. Kiufupi mambo sio shwari kabisa!.

Vyombo vya ULINZI , USALAMA na POLISI , vijipange sana.


Note: Polisi sio chombo cha Ulinzi na Usalama. Vyombo vya Ulinzi na Usalama ni USALAMA WA TAIFA pamoja na JWT


POLISI ni Raia tu kama sisi, ni Sawa na JKT tu ( Raia wanaolipwa mishahara na Serikali kwà ajili ya kutulinda sisi na mali zetu )

POLISI ni Sawa na wale walinzi wa nzego...ambao huchangiwa af5 5 KILA mwezi.
Je ulitokea?
 
Back
Top Bottom