Hapana,Mkuu kipimo cha mafanikio ya waajiriwa ni kujenga tu..?
Unajua unafurahisha sanaUhalisia unaonesha, hakuna kilichokaririwa. Biashara zina mapato ajira zimejaa makato. Assume tu within five years of Magufuli hakuna mshahara umeongezwa.
[emoji16][emoji16][emoji1]mbona mi nimetoboa ila nashindia maji na biskutiInahitajika umachale na umakini mkuu ..ajira popote duniani haiwezi kukutoa labda ufanye savings ya hali ya juu. Tatizo hawaelewi hawa waajiriwa wetu hawaelewi japo ndo wateja wetu.
Hizo no situational factors hata ajira nyingi zimepotea, hili janga la korona walioathirika zaidi ni employees hasa wale wakutegemea mshahara. Nazani wengi wamejifunza kuwa mshahara always hautoshi.Unajua unafurahisha sana
Na biashara ngapi zilifungwa kutokana na kudaiwa malimbikizo ya kodi?.
Kipindi cha corona je?.
Hamna kitu ambacho ni 'risk free'
Unajua unafurahisha sana
Na biashara ngapi zilifungwa kutokana na kudaiwa malimbikizo ya kodi?.
Kipindi cha corona je?.
Hamna kitu ambacho ni 'risk free'
Kwanini mkuu?unamatatzo mkuu sio bure mimi ni dactari bingwa wa magonjwa ya akili.
Hii CUlture ipo Japani; Mzee wangu alipata kuwa Mkuu wa Idara ya Innovation Kwenye Kampuni moja ya Majenereta huko; Sasa kwasababu sisi Tulikuwa huku Tz, yeye akawa anavuta kwenda home maana ataboeka; Wafanyakazi wakawa hawatoki;Sometimes boss ndiye anakuwa mtu wa mwisho kutoka ofisini wakati huo wafanyakazi wengine woooote wamekwishafika makwao.
Daah hongera sana mkuu, kuajiriwa mi nakulia timing tu, huku sio mmh
umbea wa watu kwenye usafiri wa umma unaleta huku..jitathminiShikamooni wakubwa zangu wote wa hapa jamiiforums.
Ndugu zangu vijana msijidanganye;
Ukiamua kujiajiri ni lazima uwe na nidhamu ya kazi (Self-Discipline) mara kumi (10) zaidi ya ulivyoajiriwa ndio utafanikiwa.
Nimeamua kutoa ushauri huu kwa maana kwamba, juzi nilikuwa nimepanda daladala ya kutoka Mnazi Mmoja huku Dar nikawa ninaelekea Kigogo kwenda kumsalimia rafiki yangu mmoja hivi, classmate wa Secondary School, aliyefiwa na baba yake weeks chache zilizopita.
Sasa mimi nilikuwa nimekaa siti ile ya nyuma kabisa maeneo ya dirishani kwa maana ndio pande zangu hizo ninazopendaga mimi, then kiti kinachofuata mbele yangu walikuwa wamekaa wasichana/wadada wawili ambao wanaonekana ni University graduates wa miaka ya hivi karibuni (mimi ni University Graduate wa miaka 11 iliyopita) alafu walikuwa wametoka kazini ila kuna changamoto moja ilikuwa imewakera wakawa wanapiga story kwa sauti kidogo bila kujua kama mimi ninawasikia.
Wale akina dada wakawa wanaambizana kuwa ni bora wajiajiri tu kwa maana kuajiriwa ni utumwa. Ukijiajiri unakuwa na nafasi kubwa sana ya kujitawala na unakuwa free sana kujipangia mambo yako uingie kazini saa ngapi na utoke muda gani tofauti na kuajiriwa katika ofisi za watu wengine ambao wanakupangia kila kitu cha kufanya.
Mimi ninaomba kuchukua wasaa huu kutuma salamu zangu za pole sana kwa vijana wenye akili kama za hawa akina dada wanaofikiri kwamba kujiajiri sio utumwa.
Ndugu zangu kujiajiri ni utumwa na kama unataka kuacha kazi ya kuajiriwa na kutaka kujiajiri kwa kudhani kwamba ukifungua biashara yako hautakiwi kuwa na nidhamu ya kazi, basi ni bora hiyo pesa uende uka-bet kwa mhindi labda zali linaweza kuwa lako ukafanikiwa lakini usifungue biashara yako.
Nidhamu ya kazi kwa aliyeajiriwa ni ile ile kwa hata wewe unayetaka kujiajiri. Usifikiri eti kwa kuwa wewe ndio boss basi ukitaka kuingia kazini hata saa 5 asubuhi basi sawa tu kwa kuwa biashara yako. Hapana ndugu yangu. Unapojiajiri wewe ndiye unayepaswa kuonesha nidhamu ya hali ya juu sana kazini ili uwe mfano wa kuigwa kwa wafanya kazi wako.
Wewe kama top boss ndiye unayepaswa kuwa panctual, yaaani kama reporting time ni saa 2 asubuhi, basi wewe ikifika tu saa 1:30, upo kazini. Kama hairuhusiwi kutupa takataka hata karatasi sakafuni boss ndiye anayepaswa kuwa wa kwanza kuonesha hilo na sio vinginevyo
Kijana kama unataka kuacha kuajiriwa na kuanza biashara yako kwa kufikiri eti ukiwa na chako ndio unapaswa kukosa nidhamu ya kazi, you are wrong na tafuta mambo mengine ya kufanya. Nakushauri nenda hata uka-bet. Yangu mimi ni hayo tu.
USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
Mkuu tangu lini mshahara ukatosha?
Naona huu mjadala watu wanaufanya kishabiki, imekuwa ligi Kati ya walioajiriwa vs waliojiajiri
Mtoa mada alikuwa na lengo zuri tu Wala sio kuwakatisha tamaa watu kujiajiri, Ni kuwa kujiajiri hasa pale mwanzo sio kitu rahisi Kama unataka kukua kimaisha kweli
Faida kubwa ya kujiajiri kunakupa nafasi ya kujikuza we mwenyewe kadri uwezavyo badala ya kumtegemea bosi afurahishwe na wewe akupandishe cheo na kujipangia ratiba zako mwenyewe
Lakini hili linakuja na price yake pia, hasa pale mwanzo unatakiwa uwe na nidhamu kubwa ili kukuza huo mradi wako na kujijengea reputation nzuri kwa wateja wako (brand)
Kuajiriwa pia sio vibaya unaweza kupata kazi nzuri inayolipa vizuri na ukawa unakua kikazi na kipato pia, lakini hata hili linahitaji nidhamu pia
Lakini kwa sababu kuajiriwa kunakuwa na misingi tayari iliyowekwa na mwenye hiyo taasisi, aliyeajiriwa hana kazi kubwa sana, yeye ni kuendeleza tu pale palipofikiwa na hiyo taasisi iliyomuajiri
Tofauti na anayeanza from scratch kujiajiri mwenyewe
Ni kweli kabisa. Ajira hata uwe na nidhamu ya fedha kubwa kiasi gani kama unaishi kwa mshahara unateseka tu. Bora uteseke lakini kwa siku una uhakika na faida kadhaa kutokana na hustle zako.Wewe mabosi wengi hawapendi kulipa mishahara mizuri ili ubaki level ile ile na likizo hawakupi
Bora ujitese mwenyewe hata huumii moyo vile kuliko unamtajirisha mtu
Umemaliza kila kitu na thread ifungwekutoboa unamaanisha nini? Maana nawajua watu wengi tu, wameajiriwa hawana miaka hata 10 kazini, wamejenga na wana usafiri, hii haimaanishi kuwa hakuna ambao wanasota, Lakini pia nawajua wengine waliaojiajiri ambao wanasota zaidi pia,
Mambo hayapo black and white kama manvyotaka kuifanya kama ligi ya Simba na Yanga
Kuajiriwa inategemea umeajiriwa wapi na huko kujiajiri inategemea umejiajiri kwenye nini na mtaji wako ni kiasi gani
Watumishi gani unaowazungumzia na waliojiajiri gani unawazungumzia...maana hayo makundi yote tunayo mtaaniHao labda waliiba. Ila kiukweli khali zao ni mbaya.
kujiajiri sio kitu rahisi na guarantee ya kufanikiwa mkuu, wapo wanaojiajiri na wanaangukia puaWewe mabosi wengi hawapendi kulipa mishahara mizuri ili ubaki level ile ile na likizo hawakupi
Bora ujitese mwenyewe hata huumii moyo vile kuliko unamtajirisha mtu
kujiajiri sio kitu rahisi na guarantee ya kufanikiwa mkuu, wapo wanaojiajiri na wanaangukia pua
Ndio maana ikiitwa job interview maelfu ya watu hujitokeza
Ndio maana mtoa mada kasema kujiajiri kunahitaji dedication zaidi hasa kwa anayeanza kuliko kuajiriwa
Kijana umeshajiajiri?najua unasema kweli Lakin bora kujaribu kotekote
TrueBora kujiajiri hata ukijitesa ni ya kwako na utapata uchungu zaidi ili upanue biashara yako na kufanya vitu vingine vya kupata pesa
Kuajiriwa boss wako anakupimia mshahara wako
Japo kila kitu kina faida na hasara
True
Mi kwenye kujiajiri hata sioni hasara asee[emoji848]
Naona mafaida lukuki