Neno kujiajiri lina maana pana zaidi ya hiyo waliyoiona hao kina dada.
Mtu kama anapenda anachokifanya yupo tayari kutumia masaa hata 100 kwa wiki kazini maana yake hayo ndo maisha yako na hicho ujifanyacho ndicho ulichochagua na unainjoy kufanya hicho ukifanyacho.
Ila kwa asiyejua maana ya kujiajiri lazima iwe utumwa kama hao wadada.
Sababu nia yao ni pesa tu.
Na wao ni watumwa wa pesa na wala hawajui hilo.
Well bila shaka hao wadada hawajaelewa maana ya kujiajiri na hawajui nini wanataka kwenye maisha yao zaidi ya pesa na kuishi maisha yasiyo na maana wala faida kwenye jamii yao.
Ila kwa mwenye elimu ya pesa basi hayo yote waliyosema ni kweli na sahihi.