Vijana someni Uuguzi, una fursa nyingi

Vijana someni Uuguzi, una fursa nyingi

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Nimezunguuka dunia hii hususani Ulaya, Marekani, Australia, na Asia, kote huko nimekuta Uuguzi (Nursing) ikiwa na fursa nyingi sana kuliko kada nyingine za Afya. Kule Marekani Uuguzi uko juu kwa ajira, malipo na kulidhika (satisfaction) ukifuatiwa na udakatari wa memo (dentist).

Vijana wengi wanadhani kuwa udaktari ndio taaluma yenye pesa na hadhi, labda hiyo ilikuwa zamani sana zilizopita wakati Tanzania kulikuwa na chuo kimoja tu cha sayansi za tiba (Muhimbili). Sasa hivi hali sio hiyo tena, udaktari sio dili tena baada ya zaidi ya wahitimu zaidi ya 2000 nchini kuhitimu kila mwaka kutoka vyuo mbalimbali. Wahitimu wa Udakatari wanasota mitaani ukilinganisha na wahitimu wa Uuguzi. Na wengi wao wanafanyakazi zisikuwa za kidaktari kama biashara,na uongozi. Kule Marekani na Ulaya wako madaktari ambao wameamua kusoma upya kozi ya uuguzi ili wapate manufaa kwa urahisi.

Sababu hasa ya mapinduzi haya ni:
1. Hospitali nyingi zinaajiri Madakatari wachache kuliko Wauguzi, hivyo wauguzi wanahitajika wengi kuliko madakatari.

2. Manesi wana taaluma nyingi ukilinganisha na madaktari, hivyo unaweza ukawatumia pia kwa kazi nyingi nyingine kama vile kwenye Uongozi, kutoa na kutunza dawa, kuzalisha, chanjo, stoo, maabara, kupima na kuhudumia watoto, utafiti, komputer/data, au Ualimu, kwasababu mtaala wa Uuguzi unawafundisha vitu vingi sana mbali ya uuguzi wa wagonjwa.

3. Mapato makubwa. Mbali ya mshahara lakini wauguzi wana overtime nyingi, seminar na mafunzo mengi ya kila wakati ambayao yanawaongezea kipato. Wauguzi wanaweza kufungua na kumiliki Maternity Home zao wenyewe na wanaweza kufungua au kutoa huduma kwenye maduka ya dawa muhimu. Daktari mara nyingi anapata kipato cha ziada kwa "kujilipua". Yaani kuhangaika na kutafuta part-time kwenye vi-hospitali mbalimbali wakati ule anaopaswa kupunzika na familia yake ili aweze kujiongezea kipato.

4. Wauguzi siku hizi wanasoma hadi ngazi ya PhD sawa na madaktari kitu ambacho zamani hakikuwepo, hizo siku hizi wauguzi wanafanya tafiti kubwakubwa wao wenyewe na kuandika vitabu na machapisho mbalimbali.

5. Wauguzi wanasomesha watoto wao, wanajenga nyumba, wanaendesha magari yao na ni viongozi wakubwa.

Vijana jiungeni na uuguzi kwa wingi fursa zipo huko pia, avuamae bahari papa kumbe wengine wapo. Achananeni na mawazo ya kizamani.
 
Humu watu wanajadili jinsi ya kuajiri au jinsi ya kutumia masaa ya watu waoga. Yaani wewe mfano kwa sababu huna kazi na masaa yako basi una mbinasifishia mtu mwenye kazi nayo, wewe atakakuwa anakulipa kwa kutumia masaa yako.

Akisha yatumia baada ya miaka kadhaa akisha ona umechoka na masaa yako hayana faida kunwa ndo pale mkataba itasitishwa na utaenda kijijini kuanza kufuga Ng'ombe.

na si jinsi ya kuajiriwa. Hii ulipaswa kuipeleka jukwaa la Elimu.

Mod wasaidie kupeleka huko

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hayo yote uliyoyasema ni sawa ila sio kwa TZ hapa

Uuguzi kwetu ni miongoni mwa kazi ngumu na yenye risk kubwa na mapato kidogo sana

Muuguzi mwenye shahada serikalini ana basic ya 980K na amesoma miaka minne..Yani analingana mshahara na Lab scientist aliyesoma miaka mitatu
 
uwongo wa wazi,moja ya kazi za kishamba basi ni huo uuguzi... mwanaume nurse huwa anakosa kujiamini kabisa....daktari anaandika wew unafuatisha kwa vitendo kilichoandikwa, unakaa na mgonjwa masaa yote.. aah wapi mazee bora msome ufundi magari hasa kwa wanaume
 
Hospitali zipi zinaajiri madaktari wengi kuliko wauguzi?!!...huu sasa uwongo
 
uwongo wa wazi,moja ya kazi za kishamba basi ni huo uuguzi... mwanaume nurse huwa anakosa kujiamini kabisa....daktari anaandika wew unafuatisha kwa vitendo kilichoandikwa, unakaa na mgonjwa masaa yote.. aah wapi mazee bora msome ufundi magari hasa kwa wanaume
[emoji13] [emoji13] [emoji13] umevuta nadhan kasomee magar yako kama utaajiliwa ata mtaan
 
uwongo wa wazi,moja ya kazi za kishamba basi ni huo uuguzi... mwanaume nurse huwa anakosa kujiamini kabisa....daktari anaandika wew unafuatisha kwa vitendo kilichoandikwa, unakaa na mgonjwa masaa yote.. aah wapi mazee bora msome ufundi magari hasa kwa wanaume
Kuuguza ni kutundulia. Muuguzi anaafikiana na kilichosemwa, andikwa, pimwa na kufanya na daktari, laboratory, mfamasia, mtu wa usingizi na wadau wengine kwenye sector ya Afya sawa na wao wanavyotakiwa kukubaliana na maoni ya muuguzi juu ya magonjwa.

Lakini hafuati maagizo hata yale mabovu. Madaktari wengine ni vilaza, huwezi kufuata kila kitu anachoandika au kusema kwa magonjwa na wengi wao wanafundishwa na kuonyeshwa na wauguzi kuhusu wagonjwa.
 
Hospitali zipi zinaajiri madaktari wengi kuliko wauguzi?!!...huu sasa uwongo
Kinyume chake. Hakuna hospital yoyote itaajiri madaktari wengi kuliko manesi. Na hii ndiyo maana udaktari unachina duniani kote. Wagonjwa wengi Wana Google matatibabu yao ya dawa, hawahitaji kuandikiwa dawa na daktari tena.

Wauguzi huwezi kuwareplace na mtu yeyote maana hata ukienda huko vijijini utakuta zahanati nyingi zinaendeshwa na wauguzi tu mwanzo mwisho. Madaktari wanaweza kugoma kama wakitaka lakini wauguzi hawawezi kugoma wagonjwa wakabaki salama hata kwa masaa 2 tu.
 
Hayo yote uliyoyasema ni sawa ila sio kwa TZ hapa

Uuguzi kwetu ni miongoni mwa kazi ngumu na yenye risk kubwa na mapato kidogo sana

Muuguzi mwenye shahada serikalini ana basic ya 980K na amesoma miaka minne..Yani analingana mshahara na Lab scientist aliyesoma miaka mitatu
Mishahara ya wahitimu inapangwa kwa kufuata vigezo vingi, miongoni mwa vigezo hivyo ni miaka ya kozi mtu aliyosoma na kuhitimu. Udaktari unasomwa miaka 5 pamoja na mwaka mmoja wa mafunzo kazini (internship) na uuguzi ni miaka 4 au 3 au 2.5 kutokana umesoma chuo gani. Ndio maana daktari anapewa 1.2m kwa Mwezi anapoanza na muuguzi na mfamasia wanapewa 0.980m kama unavyosema.

Sasa 1.2 ina tofauti gani kubwa na laki 980? Daktari anapata mapato yake kwa kuhangaika sana huku na huko na kuacha familia yake ili afanye part-time kwenye viosk (hospital za watu binafsi), kuhudhuria seminar, kufanya procedure haramu kama kutoa mimba na kula rushwa (CCD). Kimsingi mchahara wa daktari na muuguzi aliyesema miaka 4 haipishani sana kule utumishi.
 
uwongo wa wazi,moja ya kazi za kishamba basi ni huo uuguzi... mwanaume nurse huwa anakosa kujiamini kabisa....daktari anaandika wew unafuatisha kwa vitendo kilichoandikwa, unakaa na mgonjwa masaa yote.. aah wapi mazee bora msome ufundi magari hasa kwa wanaume
Hiyo ni kasumba ya kale, siku hizi hata wanaume wanapika mahotelini, na wanawake wanafanyakazi za jeshi, urubani, bodaboda. Kuna wauguzi siku hizi Wana maisha mazuri na pesa kuliko madaktari, wewe uko enzi ya giza bado, toka huko uliko.

Siku hizi uuguzi uko juu duniani sio udaktari. Kama wewe sio daktari bingwa na mahiri utaula wa chuya na kuchina. Daktari mmoja kaajiriwa Muhimbili lakini utamkuta Tumaini hospital, Regency, Kairuki, Aga Khan. Huku sio kutapandisha na kuhangaika?
 
Kuuguza ni kutundulia. Muuguzi anaafikiana na kilichosemwa, andikwa, pimwa na kufanya na daktari, laboratory, mfamasia, mtu wa usingizi na wadau wengine kwenye sector ya Afya sawa na wao wanavyotakiwa kukubaliana na maoni ya muuguzi juu ya magonjwa. Lakini hafuati maagizo hata yale mabovu.

Madaktari wengine ni vilaza, huwezi kufuata kila kitu anachoandika au kusema kwa magonjwa na wengi wao wanafundishwa na kuonyeshwa na wauguzi kuhusu wagonjwa.

Mkuu we utakuwa muuguzi, hiyo shule haina kitu.

Tunagombana na wanaume manesi huku muda wengine hadi wanatuomba mbele ya wagonjwa tusiwaite manesi, nesi huna content ya kumzidi daktari acha kudanganya, kwa mwanaume kuwa nesi ni basi tu hakuna namna, unesi uliandaliwa kwa ajili ya wanawake, hata kanuni zao zilikuwa zimeanza na ''she'' mabadiliko yametokea 2010 kwenda mbele, ni moja kati ya kazi ngumu mno unesi.. ila kwa kuwa umejikubali haina shida nesi wangu.
 
Hiyo ni kasumba ya kale, siku hizi hata wanaume wanapika mahotelini, na wanawake wanafanyakazi za jeshi, urubani, bodaboda. Kuna wauguzi siku hizi Wana maisha mazuri na pesa kuliko madaktari, wewe uko enzi ya giza bado, toka huko uliko. Siku hizi uuguzi uko juu duniani sio udaktari. Kama wewe sio daktari bingwa na mahiri utaula wa chuya.
Hahahahaahaaaah bahati nzuri nipo kwenye field, na nyie manesi pia nipo nao.. wadanganye mtaani kwenu mzee.
 
Mishahara ya wahitimu inapangwa kwa kufuata vigezo vingi, miongoni mwa vigezo hivyo ni miaka ya kozi mtu aliyosoma na kuhitimu. Udaktari unasomwa miaka 5 pamoja na mwaka mmoja wa mafunzo kazini (internship) na uuguzi ni miaka 4 au 3 au 2.5 kutokana umesoma chuo gani. Ndio maana daktari anapewa 1.2m kwa Mwezi anapoanza na muuguzi na mfamasia wanapewa 0.980m kama unavyosema. Sasa 1.2 ina tofauti gani kubwa na laki 980? Daktari anapata mapato yake kwa kuhangaika sana huku na huko na kuacha familia yake ili afanye part-time kwenye viosk (hospital za watu binafsi), kuhudhuria seminar, kufanya procedure haramu kama kutoa mimba na kula rushwa (CCD). Kimsingi mchahara wa daktari na muuguzi aliyesema miaka 4 haipishani sana kule utumishi.
Unatumia nguvu sana kuutetea unesi kwasababu ni mbovu, ungekuwa ni mzuri kusingekuwa na sababu ya kuanzisha thread kuusifia, ungejisifia wenyewe tu. Yaani kabisa nursing ufananishe na medicine?? haupo serious
 
Mkuu we utakuwa muuguzi, hiyo shule haina kitu. Tunagombana na wanaume manesi huku muda wengine hadi wanatuomba mbele ya wagonjwa tusiwaite manesi, nesi huna content ya kumzidi daktari acha kudanganya, kwa mwanaume kuwa nesi ni basi tu hakuna namna, unesi uliandaliwa kwa ajili ya wanawake, hata kanuni zao zilikuwa zimeanza na ''she'' mabadiliko yametokea 2010 kwenda mbele, ni moja kati ya kazi ngumu mno unesi.. ila kwa kuwa umejikubali haina shida nesi wangu.

Kaka udaktari una ngazi kuanzia ngazi ya chini kabisa ya Assistant Clinical officer, Clinical Officer, Medical Officer, Masters na PhD. Hata uuguzi nao unaanzia Certificate, Diploma, Bachelor, Masters na PhD. Madaktari mara nyingi huwa mnakutana wodini na wauguzi wenye Certificate, Diploma au Health attendants.

Hao pia wana elimu ndogo kiwango cha ACO na COs wenu ndio maana huoni makali yao na wanakusikiliza mwanzo mwisho hata ukiboronga. Lakini Nesi mwenye degree ana kiwango cha Anatomy, physiology, Biochemistry, Microbiology, Pharmacology, Parasitology, DS, Biostatistics, Epidemiology sawa na kile cha Daktari. Baada ya hapo anakuwa Obstetrics ya hali ya juu, surgery, medical na Pharmacology nyingine ya hali ya juu kuliko daktari. Unafundishwa leadership na management kubwa.

Fanyakazi na Muuguzi mzoefu mwenye degree au Masters ili uone atakavyokuendesha puta.

Hao uliowaona wewe ni certificate na diploma. Hakuna Daktari ambaye hajafundishwa na kuonyeshwa cha kufanya na muuguzi.
 
Back
Top Bottom