Haahaa mkuu, twende taratibu, binafsi unaleta kwenye platform? Mimi kuku nimefuga na ninafuga sana. Mimi ni miongoni mwa Tz wachache tuliokitana na Mkurugenzi wa KegFarms ambao ndo wazalishaji wa kuroiler India kwenye hotel ya coral reef.
So ni naongea kitu ninachokijua. Kwenye kuandika kila mtu anapata mafanikio. Kumeshakuja stori za green house, hydroponic, kware, sungura nk. Wengi waliowakimbilia ninyi wazee wa fursa waliishia kupoteza.
Kilimo, ufugaji vinalipa lkn siyo kama mnavoandika na kuielezea, waambieni watu ukweli siyo mnaeleza faida tu. Ufugaji una changamoto sana tofauti na unavoelezwa. Wewe unalenga kuuza vitabu vyako na si ufugaji. Ikiwa unavision yako leave your vision. Ukija hapa jukwaani tutakuchalenge tu. Unaongea miaka kumi kumaliza chuo mwezio nina miaka zaidi ya 17 ya ufugaji wa kuku, kuanzia broiler, layers, Malawi, sasso, kuroiler nk.
Nawapinga sana wale ambao Mnalenga kupata hela huku mkiacha watz wakiumia na hasara