Vijana tuingie kwenye ufugaji wa kuku, kuna dhahabu isiyoonekana

Hakuna Biashara inayo lipa ambayo mtu alishwa wahi washirikisha wenzake
 
Kwa uzoefu wangu ili ufanikiwe kwenye ufugaji hauhitaji mtaji mrefu sana, ila unahitaji ni uvumilivu tu. Unaweza kuanza na kuku 1 ila baada ya miaka 5 ukawa umetoboa mbaya sana
 
Acha wenye kejeli waendelee kukejeli,Tatizo la vijana watanzania wanaamini kubet wakiwa kwenye stuli ndefu.Hawataki kuchafuka.
Badala ya kumsikiliza mtu na kujifunza, wao ni kejeli mtindo moja, inaonyesha ukomo wao wa kujielewa!
  1. Kuna wengi wanalaani biashara ya daladala, lakini kuna watu biashara yao ya daladala inakuwa kwa kasi!
  2. Kuna watu wanafunga biashara ya shule sababu biashara mbaya, lakini wapo wanaofungua shule mpya kwa kasi sababu biashara inalipa!
  3. Kuna watu wanalaani bar ni biashara kichaaa kwani imewakata mtaji, lakini kina wengi bar zinawapa faida kubwa na kupelekea kufungua miradi mingine!
  4. Kuna watu wamefunga biashara za ufugaji kuku sababu hailipi kama ndugu wanaokejeli hapo juu, lakini kuna watu nawajua wamenunua viwanja kwa bei kubwa na kupanua uzalisha Sababu biashara ya kufuga kuku inawalipa!
Kwa hiyo issue siyo kulaani biashara fulani kwamba haifai sababu imekushinda, la, issue ni kujifunza kwa waliofanikiwa wamefanyaje.
 
U
Fuga kuku kwa PDF. wanakuwa tayari siku 3 tu maana ni shughuli kuu.

baada ya huo utani niseme wazi ufugaji sio jambo jepesi unahitaji kupata maarifa sahihi namna ya kuufanya. na ni vyema ukapata mafunzo kwa vitendo kabla ya kuingia.
Jakoseaaaaaa ..mie nafuga lakin sio kuku kuna wakat kilimo cha pdf nilkipnda mno ila nilfuga mnyama wa miez mi 2na wek 3 nikauza 60elfu kuna wakati niliuza mkubw wa miezi u kwa elfu 50 oyah ufugaji sio jambo jepes..
 
Nimekuwa mfugaji wa kuku kwa muda mrefu kidogo. Wacha nikupe nondo zangu
1. "Jua gharama kubwa iko wapi. "

Kuna tofauti kubwa sana kufuga kuku mjini na kufuga kuku kijijini. Mjini vyakula vya mifugo utanunua kwa bei kubwa. Kijijini utanunua kwa bei ndogo nafaka na utanunua vya kichanganyia kwa bei ndogo. Zaidi ya asilimia 70 ya gharama ziko kwenye chakula.

2. "Zalisha bidhaa soko linahitaji"

Kwamba hicho unachozalisha kiwe kinahitajika kwa wingi na kina soko la uhakika. Mfano mayai ya kisasa. Broiler, nk

3. Elewa msimu. Kila kitu kina msimu wake. Mfano soko la december la kuku tofauti na la Januari. Msimu wa mavuno bei za malighafi zinashuka tofauti na msimu mwingine. Hasa kwa wanaofuga kuku wa kienyeji ni muhimu sana kujua wakati gani soko linakuwa juu na wakati gani soko sio zuri.

4. Elewa namna ya kuzuia magonjwa.
(usalama wa kibayologia) biosecurity.

Matibabu kwenye mifugo ni gharama zaidi kuliko kinga. Sasa kwenye kinga inajumuisha mfumo mzima wa ufugaji kuanzia banda, namna ya uhudumiaji na mfumo unaotumia kufuga. Pia elewa hali ya hewa na magonjwa ambayo hali hiyo ya hewa inaambatana nayo.

5. Kama una malengo makubwa kabisa ili kupata faida kubwa anza na yafuatayo.
Moja, tafuta shamba kubwa.
Mbili, lima mazao ya nafaka kwa kiwango ambacho utahitaji kwenye mradi wako na ziada kidogo
Tatu, kuwa na ghala ya kuhifadhia chakula kwa kipindi hicho utakachofuga chakula kiwepo cha kutosha.
Nne, peke yako hutoboi. unahitaji wataalamu wawili. Mmoja wa kilimo akusaidie kwenye kilimo wa pili wa mifugo akusaidie kwenye mifugo.(kama humudu gharama hizo)

Hudhuria mafunzo na jenga urafiki wa karibu sana na wataalamu.
 
Hapo kwenye Green house haaahaaaa umenikumbusha mbali
Ziliingia Kwa Kasi acha kabisa
Ila sijui zimepotelea wapi Saa HV

Maturubai yametoboka na jua,nguzo zimecharangwa kuni za kupikia supu
Fad fades
 
Ubarikiwe sana
 
Kaka hakuna mfugaji anaweza andika vyote hivi.
Nimesoma mwanzo mwisho unatafuta soko la vitabu.
 

Kilimo Cha PDF

Wakati nyie mnajifariji kuwa ni kilimo cha PDF trust me, kuna watu wana make dough ya kutosha, na wanawaangalia tu.

My take, kama unataka kufanya "mishe" yoyote uliyodhamiria, FANYA regardless ya changamoto zake coz everything must be done, no xcuse
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…