Uchaguzi 2020 Vijana wa CCM tujitokeze kwa wingi kuchukua fomu za kugombea ubunge na udiwani 2020, chama kimetoa fursa

Uchaguzi 2020 Vijana wa CCM tujitokeze kwa wingi kuchukua fomu za kugombea ubunge na udiwani 2020, chama kimetoa fursa

Environmental Security

Senior Member
Joined
May 21, 2020
Posts
181
Reaction score
261
Kidumu Chama cha Mapinduzi

Napenda kutumia fursa hii kuwasihi na kuwahimiza vijana wa Chama Cha Mapinduzi tujitokeze kwa wingi katika kuchukua fomu za kuwania nafasi za kuteuliwa na chama chetu ili kugombea nafasi za kuwakilisha wananchi katika ngazi ya ubunge na uduwani, nawahimiza vijana wenzangu waTanzania hasa baada ya chama chetu kuendelea kutoa fursa pana ya kuhakikisha uwanja unakuwa na usawa kwa kila mmoja anayejitosa, mchakato utakaotumika mwaka huu hautoi nafasi ya kumpatia nafasi kubwa mtu yeyote bali kila mmoja anayo nafasi.

Nafahamu jinsi chama chetu kilivyo na vijana makini, hivyo tutumie fursa hii kuhakikisha tunajitokeza kwa wingi katika majimbo yetu na kugombea, na hii pia ni moja kati ya shabaha iliyopelekea chama kuweka mchakato wa mwaka huu kuwa wa namna hii.

Mimi tayari nasubiri dirisha lifunguliwe niende kuchukua fomu ambayo ni bure kabisa hununui wala hulipii chochote.
Vijana tukutane kwa wingi Dodoma tukiwa wawakilishi wa wananchi mwaka huu baada ya uchaguzi.

Taifa linawaamini, chama kinawaamini na kiongozi wa Taifa hili na chama ana imani kubwa kwa vijana wa Taifa hili na tunao ushahidi wa jinsi anavyowaamini na kuwapa nafasi.

Kidumu Chama cha Mapindizi

CCM imara
 
Tunaotumia night version mwandiko unaumiza macho mkuu(rangi rangi).
 
Hilo haliwezekani mbona !! Maana 45% ya wabunge wa CCM ni watu wazito na wenye uzoefu mkubwa ambao kuwakata ni ngumu watu kama Ngeleja, Chenge, Ndugai, Mhagama, Lukuvi na wengine wengi. Hao vijana watachukua nafasi gani ?? Au ni kuwapa moyo tu kwamba walijaribu hivyo wasife moyo safari nyingine ndio itakuwa zamu yao ?? CCM MNGEBADILISHA KANUNI ZA CHAMA KWAMBA ALIYEKAA BUNGENI MIAKA 10 BASI AWAPISHE WENGINE. """ 10 YATOSHA""".
 
Kichefuchefu!!!
Ni kawaida kwa mwenye mimba changa, ndimu itakusaidia, ongezea na tangawizi pamoja na pilipili kichaa ujaribu kuboost kinga ya mwili maana waoga sana nyie, Corona imewafanya mkimbie majukumu na kujifungia vyumbani matokeo yake ndo hayo, kichefuchefu tiari.
 
Pamoja na changamoto zote za kisiasa Tanzania, CCM bado ni chama kinachojitahidi sana ukilinganisha na vyama vingine na hivyo kuwaacha wengine kwa mbali sana. Hata hivyo kinaweza kufanya vizuri Zaidi ya sasa.

Kuhusu suala la rushwa wakati wa uchaguzi, ni jambo gumu sana kulidhibiti. Hata hivyo utaratibu unaotumiwa na CCM safari hii ni utaratibu mzuri sana ukilinganisha na taratibu zilizotumika hapo kabla na zinazotumiwa na vyama vingine. Ijapokuwa pengine hautadhibiti rushwa kwa 100% kwa kuwa rushwa ni suala mtambuka lenye sura nyingi, lakini kwa mazingira ya kitanzania wamejitahidi sana na kuonesha mfano unaotia moyo.

Kuhusu poleple, anajitahidi sana kukitendea haki chama katika wakati huu. Ni moja ya watu wanaojitahidi sana kukemea rushwa na kuhimiza uadilifu kwenye uongozi kwa miaka ya sasa, jambo ambalo limekuwa ni adimu sana kwenye siasa zetu.

Kwa maoni yangu, pamoja na changamoto zote, bado CCM inajitahidi kufanya vizuri ukilinganisha na vyama vingine. Hata hivyo wanapaswa kujitahidi Zaidi kwa kuwa changamoto bado ni nyingi.
 
Hilo haliwezekani mbona !! Maana 45% ya wabunge wa CCM ni watu wazito na wenye uzoefu mkubwa ambao kuwakata ni ngumu watu kama Ngeleja, Chenge, Ndugai, Mhagama, Lukuvi na wengine wengi. Hao vijana watachukua nafasi gani ?? Au ni kuwapa moyo tu kwamba walijaribu hivyo wasife moyo safari nyingine ndio itakuwa zamu yao ?? CCM MNGEBADILISHA KANUNI ZA CHAMA KWAMBA ALIYEKAA BUNGENI MIAKA 10 BASI AWAPISHE WENGINE. """ 10 YATOSHA""".
Suala la msingi ni kudhibiti rushwa kama wanavyofanya sasa. Kama mchakato wa kuwapata wagombea utakuwa hauna rushwa, then watu wenye sifa ndio watakaopata nafasi na hilo ndilo linalotakiwa. Hapo ndipo tutakapopata competent leaders na itasaidia kupunguza changamoto nyingi.
 
Back
Top Bottom