Vijana wa leo, kama umefikisha miaka 30 na huna kazi ya maana fanya hivi

Point yangu na yako havijatofautiana sana tatizo watu wameanza kujibu kwa mihemko.
 
Dah ! ,Nchi ngumu sana hii kmamaee kwa kijana wa familia duni kutoboa tena bila backup yoyote ,
Halafu kila mtu motivation speaker .
Yaani vijana wa tz wengi tunapitia mental depression Kali mno

Bora kuzaliwa mbwa Ulaya kmanina
 
N kwl ila inaitaji ujasr na kujitowa kwa jasho na dam kwa mfano mm niliaza kwa saplai maind kwa mashne za mtaa dengu kweny masoko naenda uko minada ya wamaasai mirongo ksongo na komoro kpnd ilikuwa ya mavuno bei inakuwa nzr ukleta kweny masoko yako ilnakulipa saiv naenda dodoma naleta fillets Arusha na supply kweny hotel na makampun kwaiyo kwl n watu watafute fursa na kuumiza kchwa
 
Mkuu wewe unaeleweka sio huyu boya anasema mtu akurupuke kufungua kampuni huku mtaji hana.
 
Namuunga mkono mtoa mada, alichowasilisha ni kitu muhimu sana. Japokuwa naweza kutofautiana nae katika baadhi ya vipengele.

Kiujumla hizo legal documents nyingi hazina gharama kubwa kuzipata, na kuwa nazo kunakutengenezea fursa kubwa kwa wawekezaji/washirika kama una wazo zuri la biashara.

Kiufupi inakutengenezea mazingira ya kuonekana uko serious na unachokifanya, na ni rahisi kupewa kipaumbele katika mambo mengi.

Ama katika upande wa kufungua kampuni au jina la biashara, nashauri zaidi jina la biashara. Gharama za usajili na uendeshaji ni ndogo. Kampuni ina gharama kubwa kote, na katika uendeshaji kuna penalts kubwa ukichelewa kusubmit baadhi ya vitu.

Pia kwa wadau ambao "wamemuwakia" mtoa mada aliposema atawatoza huduma za usajili, ni rahisi tu, kama unaona wazo ni zuri hizo taratibu unafanya mwenyewe wala sio ngumu.

Huduma nyingi ni online, BRELA (Usajili), TAUSI (Leseni), TRA (Mapato). Nadhani hapa JF huwezi kukosa mtu wa kukuelekeza bila malipo kama utakuwa mgeni kwenye kutumia hizo portals. Lakini mtu kukusajilia BURE ni jambo gumu tuwe SERIOUS.
 
Kiongozi sio lazima uwe na fremu kupata hizo legal documents. Kwa wale wapenzi wa simulizi za analyse watakuwa wanakumbuka ushauri aliopewa na yule "Mzee" wa kufungua kampuni hata kama hana fremu.

Tuchukulie mfano kwa vijana ambao ni mawinga wa bidhaa tofauti tofauti, unasajili jina la biashara 20,000, leseni minimum 80,000 (biashara zingine 200,000 kuendelea), Tin no. na tax clearance <300,000> (muhula wa kwanza - kutegemeana na eneo).

Ukianza kukusanya hizo document kidogo kidogo huku unaendelea na mishe zako, pakitiki kidogo unafungua hata kagoli (100,000 - 200,000/month). Hapo tayari wateja wako wakitaka kuja ofisi unayo.

Kiujumla kijana akijiongeza vizuri panapo majaliwa mambo yanaenda maana hela ndogo ndogo huwa tunazipata tatizo namna ya kuzitumia
 
Akaombe tenda serikalini hii kauli ni nzito pana ndefu kibongobongo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…