Vijana wadogo wakamatwa kwa ujangili, waua Twiga

Vijana wadogo wakamatwa kwa ujangili, waua Twiga

benzemah

JF-Expert Member
Joined
Nov 19, 2014
Posts
1,533
Reaction score
3,187
Jeshi la Polisi mkoa wa Manyara kwa kushirikiana na TAWA limewakamata watu wawili waliotambulika kwa majina ya Richard Paulo (Miaka 23) na Masiaya Lais (Miaka 19) katika kijiji cha Minjingu katika hifadhi ya Jamii ya Burunge wilayani Babati wakiwa nyara za serikali ambazo ni nyama ya Twiga inayokadiriwa kuwa na thamani ya Shilingi Milioni 30 pamoja na silaha mbalimbali zikiwemo bunduki mbili aina ya Gobole pamoja na pikipiki inayotumika kubeba nyamapori.

Kamanda wa polisi mkoa wa Manyara ACP George Katabazi amesema watu hao walikamatwa tarehe 14/2/2023 majira ya saa 8 za mchana.

Pia ameendelea kufafanua kuwa katika hifadhi ya Jamii ya Makame iliyopo kijiji cha Ndedo wilayani Kiteto askari polisi kwa kushirikiana na askari wanyama pori walimkamata mtu mmoja anayeitwa Meshaki Mohammed (54) akiwa na nyama ya Twiga anayekadiriwa kuwa na thamani ya Shilingi Milioni 30 pamoja na silaha aina mbalimbali ikiwemo visu pamoja na unga wa baruti.

WhatsApp Image 2023-02-22 at 11.32.21.jpeg
 
Babati wakiwa nyara za serikali ambazo ni nyama ya Twiga inayokadiriwa kuwa na thamani ya Shilingi Milioni 30 pamoja na silaha mbalimbali zikiwemo bunduki mbili aina ya Gobole pamoja na pikipiki inayotumika kubeba nyamapori.

Twiga anayekadiriwa kuwa na thamani ya Shilingi Milioni 30 pamoja na silaha aina mbalimbali ikiwemo visu pamoja na unga wa baruti.
Hizo millions ndizo kichocheo cha uharamia
 
Wange deal na mapapa wa hio biashara Ina uzunisha hao watoto wa ki maskini kua VESSEL (mbuzi wa kafara)

Japo Sheria hainaga huruma na ni msumeno.....

Na shaur hao vijana waachiwe huru for any means na wasaidie KATIKA kuumaliza mtandao wa wawindaji haramu....

Inasikitisha mtoto kwenda kutumikia miaka miaka 30 Kwa kuua Twiga mmoja.....nashaur hao watoto wange pewa training na kutumika kama ANT-POUCHING TZ AMBASSADOR.....
 
Nyama ya twiga mill 30 duh zaidi ya kuliwa tu ina faida gan nyingine
 
Kuwafunga sio suluhisho!!!

Juhibu TAWA na Tanapa pamoja na Wilaya. Kushirikisha jamii ya Mdori, Minjingu Vilima Vitatu..kaeni mjadili kwa KINA

Kwa uzoefu wangu katika eneo hilo kuna Changamoto kubwa sana kwenye kunufaika na Mapato ya WMA kuhusisha jamii ya mtu moja moja.....wachache ni WANUFAIKA

Hao watoto wahukumiwe ki Jadi kuhusisha wazazi....kuwamangelepaa sio suluhisho
 
Nyama ya twiga inaliwa?
Marehemu Babu yangu mzaa baba alifariki akiwa na miaka around 108....
Alifariki 2006
Maana wakati wa vita ya kwanza ya Dunia WW1
Yeye alikua anatambua kilichokua kinaendelea....
Alikua ananipa story nyingi sana za ki maisha aliwai kunisimulia Kuna jamaa siku wamekula twiga for the first time wakawa wanasema LEO TUMEULA WA TWIGA
Kwa maelezo ya marehemu Babu twiga ana nyama tamu sana...

Wa Tz walianza kula twiga zamani sanaaaa
 
Back
Top Bottom