Vijana wanaoongozana na wachezaji uwanjani wakati wa ufunguzi wa mechi wana kazi gani?

Ni amri ya mungu tukaijaze dunia kwa hiyo kila mchezaji anatakiwa aingie na mtoto ili watu wakumbuke kuijaza dunia.....
 
Kuacha hao wanaojibu kimizaha

Wale watoto wengi wao ni Academy Player

Lengo kubwa ni kutoa hamasa ya kimichezo kwa kizazi kijacho

Pili kujengewa waweze kujiamini mbele ya hadhira wanapoonesha vipaji vyao

Kukumbusha haki za watoto

Pia ni kuonesha au kutambua vipaji vipya vya soka
 
Shughuli yao inaweza kuonekana ni ndogo lakini, ina umuhimu mkubwa sana kwa utamaduni wa soka na kisaikolojia pia.
Kwani husaidia kuboresha mazingira ya michezo kwa urafiki, mshikamano, na kuonesha heshima.
Na kwa watoto, ni nafasi ya kipekee ya kujifunza maadili ya michezo na kushiriki katika matukio makubwa ya kimichezo.
Kuwapo kwa watoto hao ni ishara ya kueneza maadili ya michezo, urafiki, na usawa kati ya wachezaji wa timu pinzani.

Kazi yao!
Hali ya uwepo wa watoto husaidia wachezaji kupunguza shinikizo kabla ya mechi muhimu. Inaleta mazingira ya kirafiki na furaha.
Inawahamasisha watoto wadogo kushiriki zaidi na michezo, kuwafanya waone ndoto zao za kuwa wanasoka ziko karibu.
Hupatikanaje?
Vilabu vingi huandaa mashindano au bahati nasibu kwa watoto wanaotaka kuwa sehemu ya tukio hilo.
Baadhi ya watoto ni wa familia za wafadhili/wadhamini au huchaguliwa kupitia makampuni yanayofadhili/ kudhamini mechi hizo.
Watoto wa mashabiki waaminifu au wanachama wa klabu wanapewa nafasi hizi.
Wakati mwingine hutoka vikundi maalum kama shule, vituo vya watoto yatima, au watoto wenye mahitaji maalum hupata nafasi hizi kama ishara ya msaada na mshikamano.

Ova
 
Wanafanya kazi ya kuongozana na wachezaji
 
Borussia Dotmund hili wameliweza sana,wanaingiaga na watoto kibao na hata wakati mwingine wachezaji wa timu kubwa kucheza na vitoto kama kuwafurahisha tu
 
Labda ni vijana wa football academy wale, wanafundisha mchezo wa mpira wa miguu
 
Utekaji
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…