Vijana wekezeni, fainali umri mkubwa!

Vijana wekezeni, fainali umri mkubwa!

Kimwakaleli

JF-Expert Member
Joined
Apr 16, 2018
Posts
7,755
Reaction score
11,737
Habari wanaJF,

Niende moja kwa moja kwenye mada hapo juu. Mimi kwa Sasa nina umri wa miaka Hamsini na tatu(53). Niliajiriwa kwenye kampuni moja wakati huo nikiwa na miaka Ishirini na sita (26). Tukiwa vijana na rafiki zangu tulifurahia sana maisha na kampuni yenyewe ilikuwa inalipa vizuri sana.

Wenye ufahamu mzuri walijiwekeza kwenye ardhi, biashara, mifugo, nyumba, nk. Sasa umri umesonga nayo magonjwa nyemelezi yamekuwa tatizo. Ukimpigia simu mwenzako, utasikia naumwa kisukari mara huyu, kansa, mara, huyu viungo vimechemka, mara pressure nk.

Shida inakuja pale hukuwekeza gharama za matibabu ziko juu hata marafiki huwaoni na hata ukiwaona nao wanachangamoto zao. Tulikuwa na msemo wa kijinga wa ''Uza Nyumba Jenga Heshima Bar. Nisiwachoshe, Ahsanteni kwa kunisikiliza.
 
Nimesoma ila acha vijana wale bata hakuna asiejua fainali uzeeni kila mtu ashinde zake
Bata bukini au Bata mzinga, ukikua ndo utajua ndipo kama ni mme au ke, marafiki huwaoni Bata zipo hamu hamna, nguvu hamna 🏃moja haikai, mbili haisomeki. Baba na mama walishakufa. Duuh omba Mungu sana yasikukute mkuu, hata humu JamiiForums utaona ni mzigo macho hayasomi.
 
Ila tofauti ya life expectancy ya waafrika ni ndogo sana ukilinganisha na wenzetu kufika 90 ni kawaida sana na wao hawadhulumiwi pensions zao na wana raha mpaka wanazeeka kuliko waafrika
 

Attachments

  • Screenshot_20230813_082202_Atlas~2.png
    Screenshot_20230813_082202_Atlas~2.png
    27 KB · Views: 7
  • Screenshot_20230813_082010_Atlas~2.png
    Screenshot_20230813_082010_Atlas~2.png
    39.6 KB · Views: 7
Back
Top Bottom