Tetesi: Vikwazo vyanukia kumshinikiza Magufuli aingilie kati ili mshindi atangazwe Zanzibar

Tetesi: Vikwazo vyanukia kumshinikiza Magufuli aingilie kati ili mshindi atangazwe Zanzibar

Status
Not open for further replies.
Umesema "ikiwa"which means huna hakika.It could be vikwazo vya kufa mtu.Lakini kwa nini asiishinikize Zanzibar ikatangaza matekeo halali?Mbona mshindi anafahamika.
Ikiwa vikwazo vyenyewe ni vya kutokusafiri kwenda ulaya na marekani, wala wasihangaike maana keshajipiga ban mwenyewe.
 
Mkuu wa majeshi ameongezewa muda mwa mwaka mmoja kwa ajili ya usalama wa zanzibar na si kwa lingine lolote. Marekani na Uk awawezi kuweka vikwanzo vya kiuchumi kwa serekali ya Tanzania kwani CCM ndio wamewapa Uranium na GAS. CUF watabaki kupiga kelele tu.
Una uwezo mdogo sana wa kuelewa mambo. Unangozwa na hisia tu. Unaielewa Marekani vizuri hasa kwa sera zake za nje? Hivi Gas ni kitu gani kwa Mmarekani? Uranium yako ni jambo dogo sana kwao. Ungekuwa na mafuta wangekufikiria! Waulize Akina Saddam Hussein! Walikuwa marafiki wa Marekani kabla hawajatiwa adabu. Waulize Iran,walipewa mpaka msaada wa kijeshi lkn walitiwa adabu na vikwazo toka kwa hao hao Marekani na Uingereza!
Uwezo wa kivita wa Osama bin Laden ulijengwa na Mmarekani ili apambane na Urusi. Lkn sote tunajua leo Osama yupo wapi na nani alimfikisha huko!
Ukweli ni kwamba Tanzania hatuna ubavu wa kubishana hata na India,achilia mbali Marekani na Uingereza!
Wao ndio waliubuni Muungano wetu, sababu wanazo wao na sio sisi! Usalama na utulivu wa Zanzibar zaidi wanauhitaji wao. Ikitokea CCM inaleta ujinga juu ya hilo hawatasita kuishughulikia!
Wao wanajua kila mwizi ndani ya CCM na wapi ameficha! Wakisema wazuie hizo mali zao huko nje utashangaa hata Shein akijiuzulu mwenyewe bila hata shinikizo!
Tuache kudhania ubingwa wetu ktk wizi wa kura ni sawa na kuhimili vikwazo vya Kimataifa!
 
Ya kenya usiyaseme huku..... tumuombe ALLAH ya malizike kwao na kwetu yasije kabisa.
Na Wakenya walikuwa wanasema kama hivyo, "Tumuombe Allah ya Burundi na Rwanda yamalizike kwao kwa kwetu yasije kabisa". Duaa inaambatana na vitendo vya kweli na haki. Dua wakati unakula haramu na kuvaa vya haramu haivuki hata mata 100 kwenda juu!

Mungu wanaomuabudu Wakenya, Wwburundi, Warwanda, Wacongo ndio huyo huyo tunaemuabudu sisi. Tusubiri wakati wetu tu dharuba ya mauwaji yafike, mpaka sasa hivi hakuna dalili za kuepukika hayo, tusijidanganye bure
 
vp maalim seif kujitangaza mshindi co kosa? Kwanin afanye kaz icyo yake
Alfan issa.
Kwa mantiki ya hoja tu. Chukulia kuwa Maalim Seif amejitangaza mshindi na kwa kufanya hivyo ametenda kosa.

Kisheria Seif atakuwa ni mtuhumiwa kwa kutenda kosa. Hatua inayofaa kuchukuliwa baada ya hapo ni Seif kufikishwa mahakamani.ZEC au Mwenyekiti wa ZEC, CCM au mwananchi yeyote angelalamika Polisi. Polisi ingefungua jalada na kufanya uchunguzi. Polisi ingejiridhisha kuwa Seif ana kesi ya kujibu, Polisi ingepeleka jadala hilo kwa DPP ambaye ana mamlaka ya kumfungulia mashitaka mtuhumiwa. Mahakama baada kusikiliza kesi, madai na utetezi,ingeamua kama Seif amefanya(ametenda) kosa au hapana. Kama Mahakama ingemtia hatiani Seif kwa kutenda kosa angepewa adhabu. Adhabu hiyo itakuwa imetajwa kwenye sheria husika kulingana na kosa alilotenda. Kama Mahakama ingeona,ingejiridhisha kuwa Seif hakutenda kosa, ingemwacha huru ili aendelee na shughuli zake.

Nina uhakika adhabu hiyo kama Seif angetiwa hatiani ingekuwa ni kulipa faini au kutumikia kifungo au yote kwa pamoja. Ni wazi adhabu ambayo angepewa Seif si kufuta uchaguzi na matokeo yake.

Vizuri umeuliza swali, kama ulikuwa na nia ya kufahamu na kuongeza maarifa, natumai utakuwa umefaidika na maelezo haya.
Jipatie maarifa zaidi kwa kupitia uzi huu. Link 1. Msaada: Nini kitatokea iwapo CUF hawatashiriki uchaguzi wa marudio Zanzibar?

Pia angalia hii video, maoni juu ya mgombea kujitangazia ushindi.

 
Inauma sana kwa vile watakaosota na maisha ni sisi Watanzania wenye kipato cha chini. Siku zote naombea muungano uvunjike tu kwani ukiangalia udogo wa kisiwa cha Zanzibar na athari zitakazotupata wabara hadi nakereka.
Na hilo ndilo lengo la Marekani. Hataki kuona mtemi mwingine akiibuka.
 
Una uwezo mdogo sana wa kuelewa mambo. Unangozwa na hisia tu. Unaielewa Marekani vizuri hasa kwa sera zake za nje? Hivi Gas ni kitu gani kwa Mmarekani? Uranium yako ni jambo dogo sana kwao. Ungekuwa na mafweuta wangekufikiria! Waulize Akina Saddam Hussein! Walikuwa marafiki wa Marekani kabla hawajatiwa adabu. Waulize Iran,walipewa mpaka msaada wa kijeshi lkn walitiwa adabu na vikwazo toka kwa hao hao Marekani na Uingereza!
Uwezo wa kivita wa Osama bin Laden ulijengwa na Mmarekani ili apambane na Urusi. Lkn sote tunajua leo Osama yupo wapi na nani alimfikisha huko!
Ukweli ni kwamba Tanzania hatuna ubavu wa kubishana hata na India,achilia mbali Marekani na Uingereza!
Wao ndio waliubuni Muungano wetu, sababu wanazo wao na sio sisi! Usalama na utulivu wa Zanzibar zaidi wanauhitaji wao. Ikitokea CCM inaleta ujinga juu ya hilo hawatasita kuishughulikia!
Wao wanajua kila mwizi ndani ya CCM na wapi ameficha! Wakisema wazuie hizo mali zao huko nje utashangaa hata Shein akijiuzulu mwenyewe bila hata shinikizo!
Tuache kudhania ubingwa wetu ktk wizi wa kura ni sawa na kuhimili vikwazo vya Kimataifa!
Nimekuelewa lakini main point yangu ujaelewa vinzuri. Marekani au UK awawezi kutuwekea vikwanzo vya kiuchumi kwa sababu CUF wameonewa, usithani kwamba wanafanya maamuzi kwa sababu ya interest ya watanzania. Sikuzote hizi nchi za ulaya wanaangalia interest za nchi zao ndio sababu mara nyingi foregn policy zao zinabadilika kila wakati. Kwa hiyo CUF watabaki kupiga kelele, kuandika barua kwenye umoja wa mataifa na kungingine kote hakuna kitakachotokea ni bora wakubali kurudia uchaguzi tu.
 
Huu mgogoro wa zanzibar ni wa kutengenezwa na kulichafua taifa bure, kwani magufuli anashindwa nini kufanya kazi na upinzani? tatizo kubwa la Tanzania tuliikubali democracia kwa ajiri ya kupata misaada ya wahisani sio kwa ajiri ya manufaa ya Taifa hapo ndo ngoma nzito inapokuja kwa watawala (ccm). Nchi hii ilisifika sana kwa amani duniani na utawala imara lakini sifa hizo tulizipata tukiwa chini ya chama kimoja, sasa mfumo wa vyama vingi ulipoingia tanzania watawala yaani ccm walishauliwa kurekebisha baadhi ya mambo kama vile serikali iwe na nguvu kuliko vyama, kubadili mifumo ya mahakama, police, katiba ili iweze kutoa usawa kwa wananchi pia kwa vyama vingine wakakataa, hivyo ccm/serikali ikaingia kwenye mfumo wa vyama kama main player, bila kujua kuwa Tanzania /watu wanazidi kuwa na maarifa zaidi , na Tanzania au Mtanzania wa sasa ni tofauti na wakipindi kile. Bomu la zanzibar ni moja ya sula ambalo hata magufuli leo ikimuuliza bwana hapa nani kashinda atakuambia yenyewe fulani kashinda sema hatuwezi kumtangaza kwa sababu ni wachama fulani, utaona hata raisi wa nchi hana nguvu kushinda chama chake, taasisi zote nyeti zinatumikia chama kimoja, inakuwa ni gumu serikali iliyoko madarakani kufanya kazi na watu wa upinzani. Kama tungewezeka kubadili haya mambo zamani ilikuwa ni raisi kutatua mgogoro huu wala tusingefika hapa kama taifa. Taasisi kama NEC/ZEC hazina nguvu kwa nchi yetu, wao ni bendera tu, wakiambiwa fanya hivi watafanya. Binafsi naona ni wakati basi wa vyama vyote kufanya kazi kwa pamoja, yaani dhamira itoke moyoni , tufike kipindi haki itawale bila kujali au kuegamia upande mmoja na tuunde taasisi zenye nguvu na tusiziingilie kiasi kwamba zikisema hizo basi tunafuata. Siku zote msingi wa democracia sio ujanja ujanja huu tuufanyao bali ni haki, tukiwa na taifa la haki tutafika mbali, ujanja ujanja usanii hautatusaidia, hata kama tukirudia chaguzi zaidi ya 100 hatutapata jibu.
 
vp maalim seif kujitangaza mshindi co kosa? Kwanin afanye kaz icyo yake

Kama kajitangaza mshindi ni kosa na anafaa kushitakiwa kwa kosa hilo. Hata hivyo kosa hilo si la kufuta uchaguzi wote. Jee ingetokea kama Hashim Rungwe kajitangaza ushindi Lubuva angefuta matokeo ya uchaguzi wa TZ? jifunze na kufikiri pia sio kujua kuandika tu!
 
Ni hatareeeeee
Nani hajui katiba ya ZNZ ikoje? Shida tunatanguliza siasa. Mpaka ZNZ wakikubali ni Watanzania na kuwa na Katiba isiyo na mlengo wa kujitenga ndo patakuwa na nafasi ya Rais wa Jamhuri kuingilia mambo yao.

Kwa sasa imebaki ikitokea tu vurugu. Mambo yao ya ndani watajuana.
 
bora cuf wamegoma kwakweli maana inakera..watu wamchague rais wao ccm wafute ....ingekuwa nikule kwetu....ingekua ni kughecha tu watu..mana hakuna namna sasa
 
Mwenye mawazo mafupi ni anayeshabikia vikwazo vya marekani kwa serikali ya Tanzania wakati anshudumiwa na serikali ya Tanzania. Ni sawa na kushabikia mafuriko wakati unaishi bondeni.


Akili ,akili ,akili,
Elimu,elimu,elimu.
Maarifa,maarifa,maarifa.

Anayeshabikia kwa vitendo kunyimwa misaada ni yupi kati ya aliyefuta matokeo halali aliyoyatangaza kwa wawakilishi na kuwapa hati za ushindi au anayetoa tahadhari ya kuibuka kwa mgogoro mkubwa kwa uroho wa watu walianzisha chama na kusajili chama wakakiita CCM. Wamekifanya kuwa neno CCM ni mungu mwenye nguvu anayetawala milele na milele.

Ni utumwa na ushetani mkubwa kuanzisha chama halafu unakitukuza pasipo kujali usalama,utu,undugu,amani ,furaha ,upendo na umoja wa watu kisa umelenga tu kubaki madaralani milele.

Tutanyimwa misaada kutokana na akili za wanaCCM wengi kulewa madaraka. Ulevi unaondoa busara na hekima.
CCM wamelewa sana. Hawana aibu tena. Wanashabukia ubaguzi wa rangi ili wabaki madarakani kwa mapinduzi yaliyoongozwa na Jecha.
Aibu kubwa kama mtu bado haoni kwa wahisani wako sawa kutunyima misaada.

Wewe unafikiri Dr. Shein,Jecha ,Mwinyi,Mkapa na Kikwete na Makada wengine wanaochochea ubaguzi kule Zenji wataathirika kwa kukosa hiyo misaada?
Hawa hawajali kwani hawana hata harufu ya shida kwani wamefaidi ujinga na uvumilivu wa watanzania kwa muda mrefu ilihali wao sio wavumilivu hata wa kuona Maalim Seif anakua rais wa kakisiwa ka Zanzibar. Hawana huo uvumilivu. Ni bora mamilioni ya watanzania waumie kwa kukosa misaada lakini mwanachama na rafiki yao anayeitwa shein anakalia Ikulu ya Zanzibar.
Wanahubiri amani ,upendo,uvumilivu,na mshikamano wakati wao hawana hata mojawapo ya wanachohubiri.
 
Alivyotangaza Mb 8 ilikua halali?
Wazazibari watu wapuuzi sana. Wanajua sheria zao zinasemaje lakn wanajitia punguwani kutokubali ukweli.
Tume na mwenyekiti wake ndio kila kitu kwenye uchaguzi , hakuna nguvu zaidi ya hapo hata mahakama inaweza kubatilisha walichosema hiyo ndio sheria ya Zanzibar.
Jecha kaishatangaza kurudia na tarehe imetamkwa , sasa bado mnajitia wendawazimu kwa madai ya kutangaza matokeo yaliyofutwa , manataka tuwaelewe namna gani . Susia Uchaguzi watakaojitokeza tunachagua viongozi na maisha yanaenda,
Huyo sultani wenu anaogopa nini kurudia ?
 
Nimekuelewa lakini main point yangu ujaelewa vinzuri. Marekani au UK awawezi kutuwekea vikwanzo vya kiuchumi kwa sababu CUF wameonewa usithani kwamba wanafanya maamuzi kwa sababu ya maslihi ya watanzania. Sikuzote hizi nchi za ulaya wanaangalia interest za nchi zao ndio sababu mara nyingi foregn policy zao zinabadilika kila wakati. Kwa hiyo CUF watabaki kupiga kelele, kuandika barua kwenye umoja wa mataifa na kungingine kote hakuna kitakachotokea ni bora wakubali kurudia uchaguzi tu.
Mkuu ni kweli. Aliyeanzisha mada anajitekenya na kucheka. Suala la Zanzibar is a speck of sand kwa sasa katika sea of conflicts. Hivi Wazungu hawajui gharama ya kuingilia mambo ya nchi? Wamejifunza mengi na Syria na sasa hao hao upinzani waliokuwa wanawabeba wanawalazimisha wakae mezani ktk mazungumzo ya amani.
Kwa hapa Tanzania CUF wanasahau kuwa hii Tanganyika wanayoichukia ni muhimu zaidi strategically kwao wazungu kuliko visiwa vyao. As long as Magufuli anaendelea na agenda yake ya anti ufisadi hii ya Zanzibar nayo itapita tu. Watatoa tu matamko basi! Vikwazo vya kiuchumi ni wishful thinking ya CUF nothing more.
That been said inabidi tutafute suluhu la kudumu for Zanzibar na Muungano
 
Unadhani CUF kukataa kushiriki uchaguzi ikitaka matokeo ya zamani yatangazwe inaashiria nini?halafu msidhani kwa kupeleka wana usalama wetu visiwani Zanzibar ndio mtafanikisha azma zenu za kisiasa,mgogoro Zanzibar ukilipuka kwasababu ya ujeuri na tamaa zenu za madaraka ujue na huku Bara hatutanusurika,tutaingia ktk matatizo yale yale wanayopitia Wakenya.Usidhani huu mgogoro ukilipuka utakuwa kama wa Burundi na kuzimwa kwa kutumia Nkurunzinza style. It will be a more catastrophic conflict than you think. Power is nothing compared to the lives of Tanzanians. Msije kutuharibia amani yetu jamani,chonde chonde.

Hizo ni kelele za mfa maji, acha kudanganya watu, virugu ziko wapi na nani kakwambia kuwa kutakuwa na vurugu? na zikitokea mwanzilishi wake si yupo. na siku zote wapinzani mnapenda sana vita itokee hapa nchini, kwa bahati mbaya watz walowengi hawakubaliani na ujinga huo.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom