Vilabu 15 NBC havijapata mgawo wowote miezi 3

Vilabu 15 NBC havijapata mgawo wowote miezi 3

Tangu mkataba usainiwe Kati ya GSM na TFF na kushirikisha vilabu 15 ,vilabu havijapata mgawo ndani ya miezi yote mitatu .

Tulisema mkataba wa GSM ni wa kihuni na hawana huo ubavu kudhamini ligi , vilabu 15 vilijifanya vyote vimekubali na njaa zao na kukebehi Simba kumbe wanafanya matangazo ya GSM bure.

GSM ni genge la kihuni wamejaa chupli chupli tu.


View attachment 2111652
Je umeusoma huo mkataba kujua majukumu na haki ya kila mdau wa mkataba?

Sent from my SM-N960F using JamiiForums mobile app
 
Je, vigezo vili fuatwa kama walivyo kubaliana kimkatabaa? kama hapana basi bodi ya ligi na Tff wna makosa na kama vilifuatwa Gsm ata fidia hyo miezi aliotangazwa na vilabu [emoji848]
GSM kasema amevunja mkata, it means ulimukuwepo mpaka anaamua kuvunja, mwambie aombe JUA liwake Dar magodoro yakauke lasivyo KISUTU inamngoja.
 
Vishabiki vya simba vinaogopa GSM kutwa kuipa Kiki JF. Andamaneni laivu mueleweke
Waandamane Yanga na vilabu vingine 14 kwa kutoingiziwa 2B. Simba waandamane kwani wanamdai nani?
 
GSM kasema amevunja mkata, it means ulimukuwepo mpaka anaamua kuvunja, mwambie aombe JUA liwake Dar magodoro yakauke lasivyo KISUTU inamngoja.
Vipengele vya mkataba wako visipotekelezwa automatically huo mkataba unakuwa umevunjika

NB:Rudi shule ukajifunze kuandika na kusoma vizuri
 
Kama masharti hayakutimia waliaanza vp kuvaa nembo na kuweka matangazo ya GSM
Mkataba una consist timu 16 zote za ligi kuu kuvaa nembo ya GSM kwenye bega la kushoto

Timu 15 tu ndo zikawa zinavaa hizo nembo na timu ikakataa na hata bila kuchukuliwa hatua za kisheria

TFF na bodi ya ligi kufikia hapo mmevunja makubaliano yetu na mdhamini hana haja ya kuweka pesa tena ktk hilo
 
Kwa hiyo mlikuwa mnaitaka Simba hahahaaaaaaa godoro limelowa maji..
GSM wameidhamini ligi kuu na timu zote lazima wavae nembo Ya GSM na kama Simba alikuwa hataki kuvaa nembo hiyo basi automatically mkataba umevunjika hata ingekuwa timu yeyote iliyobaki isingevaa, hali ingekuwa ni hiyohiyo
 
Tuwe wa kweli...kama Mo angechukua nafasi ya GSM akaidhamini Ligi Kuu.. Unadhani Yanga wasingesumbua?!..Jibu ni hapana..Mpira wa Bongo bila kuzisikiliza hizi timu mbili TFF haina nguvu..
Hata kama walichofanya Simba kisheria na Kikanuni wamekosea,kilitegemewa tu, na Yanga wangefanya hivyo hivyo mdhamini angekua Mo..

Sent from my SM-A405FN using JamiiForums mobile app
Hiki ndo ambacho kimetengenezwa kwasasa mdhamini yeyote akitokea kuja kudhamini ligi na Yanga akiona ana chembechembe za Usimba basi hakuna litakalokubaliwa

Inshort kupitia hili ligi yetu tunaichimbia kaburi sisi wenyewe kwa ushabiki wa kipumbavu kabisa

Mpira unahitaji pesa za kutosha ktk kuendesha timu, hatuhitaji Simba na yanga pekee ndio ziwe timu zenye uwezo mzuri wa kipesa pekee, hapana.

Kupitia udhamini unaokuja ndio na hizi timu ndogo zinapata nafuu kifedha na kuleta ushindani madhubuti katk ligi yetu na kupelekea kupata wachezaji wazuri watakao wakilisha vzr timu ya Taifa Coz ss hatuna wachezaji wengi wanaocheza nje ya nchi, kwahyo tunategemea ligi ya ndani zaidi
 
Taja embu hata mmoja
Unafahamu kwamba mkataba wa TFF na TBC kurusha matangazo kwa njia ya radio ni Milioni 300 kwa miaka 2?

Kwa mwaka inatoka milioni 150 kwa timu zote 16,na ukigawa hiyo pesa hakuna hata pesa ya maana inayopata timu ili kujiendesha

Je, vipengele vya mkataba huo viliwekwa wapi wazi na vikajulikana, na Je, mliweza kuhoji chochote kuhusu hilo

Jitahidi kutokuwa na akili mgando kama vile unafanya kazi kwa wahindi mkuu
 
masharti yapi?
mbona hawakuvunja mkataba mapema kabla hayo masharti hayajafuatwa kwanini wasubiri hadi mzunguko wa kwanza uishe ndo wavunje mkataba?
Mkataba wa GSM na TFF umeingia wakati ligi tayari imeanza na takribani mechi 7 zimechezwa

Wakati ligi inaendelea na masharti ya mkataba hayatekelezwi, GSM akawa anawaandikia barua TFF kuhusu kutotimizwa kwa masharti yake na TFF wala hakujisumbua kujibu

GSM wasingeweza kusitisha mkataba wakati ligi inaendelea na wakasubiri mzunguko wa kwanza uishe ili wavunje mkataba wao ili tukirudi round ya pili basi kila iwe imetoa nembo ya GSM kwenye mabega yao

Just simple as it
 
𝐓𝐀𝐍𝐆𝐀𝐙𝐎 𝐋𝐀 𝐔𝐊𝐎𝐌𝐎 𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐊𝐔𝐁𝐀𝐋𝐈𝐀𝐍𝐎 𝐘𝐀 𝐔𝐃𝐇𝐀𝐌𝐈𝐍𝐈

➪Tunasikitika kuwajulisha kwamba Makubaliano yetu ya Ufadhili ya tarehe 23 Novemba 2021 yatakatishwa.

➪Barua hii inatumika kama notisi rasmi ya kutimiza madhumuni yaliyowekwa chini ya kifungu cha 5 cha makubaliano hayo.

➪Tafadhali fahamu kuwa tunakatisha Mkataba huu kutokana na yafuatayo.

1. Mechi zote za ligi kuu ya nyumbani zinazohusisha Simba SC zimechezwa bila ya kuonyesha nembo ya GSM kwenye mbao za pembeni hii ni kinyume na kifungu cha 4.1 na 4.4 cha Mkataba wa Udhamini.

2. GSM imenyimwa kwa makusudi haki yake ya kuonekana kwenye bango la nyuma kwa habari zote zinazohusu Simba SC kinyume na kifungu cha 4.8 cha Mkataba wa Udhamini.

3. GSM imenyimwa kwa makusudi haki yake ya kuonekana kwenye mabango ya Pre and Post conference conference inayohusisha viongozi wa Simba SC kinyume na kifungu cha 4.9 cha Mkataba wa Udhamini.

4. GSM imenyimwa kwa makusudi haki yake ya kuonekana kwenye mkono wa kushoto wa jezi za Simba SC kinyume na kifungu cha 4.12 cha Mkataba huo wa Udhamini.

5. TFF imeshindwa kujibu barua zetu na kushindwa kurekebisha ukiukwaji kama ilivyoainishwa kwenye notisi ya uvunjaji wa tarehe 14 Desemba 2022. 6. TFF imeshindwa kutekeleza kanuni zake kuhusu Wadhamini.

7. Nembo na chapa za GSM mara kwa mara zimekuwa zikidharauliwa na maofisa wa TFF.

8. TFF imeshindwa kuweka viwanja vya haki kwa mechi za ligi kuu.

➪Mwisho tunapenda kuitaarifu ofisi yako kuwa Bwana Ghalib Said Mohamed ameamua kujiuzulu nafasi yake ya Uenyekiti wa Kamati ya Ushindi ya Taifa Stars kwa maslahi ya soka la Tanzania.
 
Hiyo hapo juu ni masharti yaliyovunjwa kwenye mkataba na nimetafsiri kwa Kiswahili ili wajinga wengine muelewe
 
Niimejiridhisha pasi na shaka kuwa, wengi waliokuwa wanapinga udhamini wa (GSM) kwenye ligi na wote wanaosherehekea kujitoa kwake, wamegawanyika katika makundi makubwa mawili.

1. Hawajui katiba ya (TFF) hasa kuhusu suala la mkataba wenyewe unaotajwa kuwa ni wamagumashi.

2. Wanajua katiba ya (TFF), ila wanaendeshwa na hisia za ushabiki maandazi wa Usimba na Uyanga.

Kwanza kabisa hakuna sehemu yoyote ambayo (GSM) anamakosa kuhusu suala la udhamini mwenza kwa sababu yeye kama Muwekezaji alifuatwa na (TFF) akiombwa kuidhamini ligi kuu Tanzania bara na sio kwamba yeye alilazimisha kuja kuidhamini ligi.

- Jambo hilo lilithibitishwa na Rais wa (TFF) Wallace Karia ambaye alikiri kwamba wao kama (TFF) ndio walimuomba (GSM) aidhamini ligi kuu.

Baada ya (GSM) kuhakikishiwa na (TFF) + Bodi ya ligi kwamba logo yao itavaliwa na vilabu vyote (16) vya ligi kuu upande wa kushoto wa mkono wa jezi, na mabango yao yatawekwa kwenye viwanja vyote, (GSM) akakubali kuidhamini ligi....

... GSM kama kampuni wakakaa na (TFF) na bodi ya ligi wakafikia makubaliano ya kimkataba kuwa (GSM) watatoa Tsh 2.1 Billion kwa misimu (2) kwa awamu tofauti kulingana na makubaliano ya mkataba.

Kwa nini vilabu havikushirikishwa au vilishirikishwa? Hilo sio jukumu la (GSM). Kwa mujibu wa katiba ya (TFF) wenye jukumu la kuingia Mikataba yote inayohusu Udhamini wa ligi, haki za matangazo ya Tv na radio nk ni (TFF)...

(TFF) Wao ndio wanapaswa kusimamia vilabu ikiwemo kuwashirikisha na kuwajuza nini makubaliano ya Mikataba waliyoingia, japo katiba haiwalazimishi kufanya hivyo pia.

- Katiba ya (TFF) ndiyo iliyotoa LOOPHOLE ya baadhi ya vilabu kupinga Udhamini na sio (GSM)... Kwa kuwa (GSM) ni muungwana yeye ameamua kujitoa kwa sababu (TFF) imeshindwa kutekeleza makubaliano ya kimkataba waliyokubaliana.....

GSM angeamua hata kuishitaki (TFF) kwa kumchafua au kwa kutotekeleza mkataba ambao uko kisheria. Lakini yeye akachagua kujiweka kando tu.

- GSM hapa anatumika kama kichaka cha kujifichia, lakini ukweli wa mambo ni kuwa Uyanga wake ndio unamponza kwa sababu kuna Mikataba mingi tu inayoingiwa hapo (TFF) bila kuvishirikisha vilabu kwa kutumia katiba hiyohiyo iliyopo lakini hakuna klabu hata moja ambayo ilishawahi kuhoji au kulalamika kuwa haikushirikishwa.

- Mimi naamini, kama huu huu mkataba wa Udhamini mwenza ungekuwa umeingiwa na kampuni nyingine tofauti na (GSM) kusingekuwa na hoja zoote hizo zilizoibuliwa kuupinga.

- TBC wameingia mkataba wa miaka (3) kwa Tsh 300 Milioni pekee, lakini hakuna klabu inayoyapinga mabango ya TBC kwenye viwanja kwa kusingizia kuwa pesa ni ndogo,, Lakini kwa GSM aliyetoa 2.1 Billion mabango yake uwanjani yalipigwa vita sana kwa madai pesa ni ndogo !!!!
Fact
 
Mkuu kuna vitu ukisikia uwe watulia na kutafakari...

GSM alikuwa anadhamini ligi ya NBC, na jezi anazotumia Simba kwenye ligi ya Bongo sio zile anazotumia kwenye mechi za CAF...

Sasa Simba angemtangaza vipi GSM kimataifa?
Mkuu Kuna watu wengine ni mabongo lala mkuu ishue iko wazi kabisa kwamba gsm ni mdhamini wa ligi kuu hiyo kimataifa anafuata nn kwa mkataba upi na kwa mandate ipi kuwa watu ni wajinga wa akili
 
Sasa vilabu vingepata vipi mgao wakati kulikuwa na mgogoro wa kimkataba?

Simba hakuwa tayari, hadi hapo GSM asingeweza kuendelea na mkataba na TFF...
hivyo aliingia mkataba kwaajili ya simba?
 
Mkataba wa GSM na TFF umeingia wakati ligi tayari imeanza na takribani mechi 7 zimechezwa

Wakati ligi inaendelea na masharti ya mkataba hayatekelezwi, GSM akawa anawaandikia barua TFF kuhusu kutotimizwa kwa masharti yake na TFF wala hakujisumbua kujibu

GSM wasingeweza kusitisha mkataba wakati ligi inaendelea na wakasubiri mzunguko wa kwanza uishe ili wavunje mkataba wao ili tukirudi round ya pili basi kila iwe imetoa nembo ya GSM kwenye mabega yao

Just simple as it
u
Mkataba wa GSM na TFF umeingia wakati ligi tayari imeanza na takribani mechi 7 zimechezwa

Wakati ligi inaendelea na masharti ya mkataba hayatekelezwi, GSM akawa anawaandikia barua TFF kuhusu kutotimizwa kwa masharti yake na TFF wala hakujisumbua kujibu

GSM wasingeweza kusitisha mkataba wakati ligi inaendelea na wakasubiri mzunguko wa kwanza uishe ili wavunje mkataba wao ili tukirudi round ya pili basi kila iwe imetoa nembo ya GSM kwenye mabega yao

Just simple as it
anacholilia mtu wenu hajatangazwa na Simba kwenye jezi na pre/post match na sio tff
jamaa wenu hana pesa.

FCFAB0CF-67B4-4670-AE0B-A02D963C50D0.jpeg
 
Mkuu kuna vitu ukisikia uwe watulia na kutafakari... GSM alikuwa anadhamini ligi ya NBC, na jezi anazotumia Simba kwenye ligi ya Bongo sio zile anazotumia kwenye mechi za CAF... Sasa Simba angemtangaza vipi GSM kimataifa?
Sasa iweje avunje mkataba uliotekelezwa na vilabu 15 kati ya 16 sababu ya klabu moja tu aliyoitaja mara nne kwenye malalamiko yake? Kwa nini hazungumzii kuwalipa waliotumikia mkataba ila anazungumzia kuvunja?
 
Back
Top Bottom