MTANGAZAJI wa Kipindi cha Mitikisiko ya Pwani kinachorushwa kupitia Radio Times, Hadija Shaibu Dida amefunguka kuwa kamwe hawezi kufanya kazi Ikulu kutokana na vimini anavyovitinga .
Akizungumza na Amani, Dida, alisema kuwa anafurahia sana kazi anayofanya kwa sababu inamruhusu kuvaa nguo yoyote anayojisikia vikiwemo vimini . Kufanya kazi Ikulu ningeshindwa kwani kuvaa nguo ni kwa sheria , huwezi kujivalia tu , kazi yangu nipo huru naweza kuvaa kitu chochote kile nikajisikia nina amani , lakini Ikulu lazima utinge koti na kuchomekea , alisema Dida.