Vinyago/midoli vina roho

Vinyago/midoli vina roho

Sasa dubwana kama hili nalo mtu analiweka ndani mwake la nini?

Kuna watu hawana uwezo wa kuishi maisha yao wenyewe kwa kumtegemea Mwenyezi Mungu hivyo hutafuta support ya madubwana kama hilo!kwa haraka utadhani ni pambo lakini nyuma yake kuna siri kubwa
 
Huyu naye alikuwa na roho wachafu wenye mikosi
kwa sasa yuko jumba la makumbusho
unaweza kum....google
''Robert the doll''.
 

Attachments

  • doll.jpg
    doll.jpg
    9.5 KB · Views: 171
Mi niliambiwa midoli vinyago si mizuri kuweka ndani nikawaga siamini mana nilikua naipenda kuiweka sebuleni. Sasa siku moja nikiwa nimelala nimeiweka pembeni nikaona mdoli una nyanyuka na kunirukia nilipiga makelele ya hatari na kutetemeka juu. Tangia siku hyo nimekoma hata kuibeba. Kweli vinyango ni ma spirits machafu kabisa na inaweza ikawa inaleta mikosi.
haiwezekani....
 
Mi nakataa haiwezekani mudoli umeunua halafu ubadilike. :sad:ya kweli hayo:sad: :A S-rap::A S 100:

haiwezekani....

Ili nitokea kabisa hii issue live bila chenga kabisa. Hakuna lisilowezekana chini ya jua. Mwanzo nilikua mgumu siku yaliyonipata ndo nikaelewa. Dunia ina mambo mengi sana yanaendelea kwenye ulimwengu wa kiroho sema sio binadamu wote hufunuliwa na kuona yanayoendelea.
 
Popote ulipo mshana jr, unashtakiwa kwa kosa la kusababisha hawa mabinti washindwe kuvipumzisha vikojoleo vyao kwa usiku wa leo.

Jiwasilishe makaburi ya kinondoni kwa ajili ya toba. (tafazali, sijasema mochware, staki hawa mabinti washindwe kuamka)

Vigezo na masharti kuzingatiwa.

Nimeolewa kwa uji...kwanini nivipumzishe?
Acha viteseke
 
Last edited by a moderator:
huwa tunafuga majini, vinyamkera, madogoli na roho chafu majumbani kwetu bila kujua. Tunanunua vinyago na midoli ya gharama kwa ajili ya kupendezesha sebule zetu na wakati mwingine kama kampani vitandani mwetu...

Hatutishani lakini ni hatari, vina roho hivi vitu!

Wengi wetu tumeshawahi kuona zana za waganga wa kienyeji na wachawi, hawakosi vinyago na midoli, pia tumeshawahi kuona wale wenzetu waabuduo miungu wana masanamu mengi sana...! Yale yote yamebeba roho na ndio hizo wanazoziabudu.

Kuna roho zinatangatanga duniani hazina makazi baada ya majumba (miili) yao kuharibika (kufa) hivyo huwayawaya huku na kule zikitafuta makazi. Kwa kuwa roho haiwi na nguvu mpaka ipate pa kukaa. Sasa ndugu yangu unajaza midoli nyumbani au kwenye gari au ofisini unavutia na kukaribisha mapepo.

Zipo shuhuda mbalimbali za watu waliofanyiwa mambo au kuona mambo ya ajabu kutoka kwenye midoli na vinyago....

Punguza kuhifadhi hivi vitu vyaweza kuwa na roho zenye madhara makubwa..

naona hata wale wenye imani wote wameyumba kwa bandiko lako hili,ulichokiandika ni kweli kabisa lakini siyo kwa extent hiyo.siyo kila kinyago kina roho chafu.roho chafu hukaa hata kwa binadamu,je ni sahihi kusema kila binadamu ana roho chafu?hapana.nakubaliana na wewe kuwa kuna vinyago hukaa roho chafu kama walivyo binadamu vile kuwa kuna watu wana roho wachafu kama vile majini na wengine hawana roho hao.

Nikupe mfano mmoja mdogo tu bro,ukisoma historia ya yesu kuna sehemu alimtoa mtu mapepo na kuyaamuru yakawaingie nguruwe.kuna watu wengine mpaka leo hii hawali nguruwe kwa kuamini kuwa wana mapepo.ukiangalia kwa haraka utaona kuwa nguruwe walioingiliwa na mapepo na kufa siku ili walikuwa wale tu waliokuwa eneo lile na siyo nguruwe wote wa israel.

Hii mkuu tunaita stereotyping yaani unachukua tabia moja ya kitu kimoja na ku generalize kuwa jamii nzima ya vitu hivyo vina tabia hiyo.hapa umewakamata watu kwa uoga na hisia tu.hata wale wenye imani zao zimeyumba.ukiwauliza wote waeleze ni kisa kipi walishawahi kupata kuhusu midoli kati ya elfu utakuta ni mmoja tu ndiyo mwenye stori aliyoishuhudia zaidi ya stori za kuambiwa na kusikia
 
naona hata wale wenye imani wote wameyumba kwa bandiko lako hili,ulichokiandika ni kweli kabisa lakini siyo kwa extent hiyo.siyo kila kinyago kina roho chafu.roho chafu hukaa hata kwa binadamu,je ni sahihi kusema kila binadamu ana roho chafu?hapana.nakubaliana na wewe kuwa kuna vinyago hukaa roho chafu kama walivyo binadamu vile kuwa kuna watu wana roho wachafu kama vile majini na wengine hawana roho hao.

Nikupe mfano mmoja mdogo tu bro,ukisoma historia ya yesu kuna sehemu alimtoa mtu mapepo na kuyaamuru yakawaingie nguruwe.kuna watu wengine mpaka leo hii hawali nguruwe kwa kuamini kuwa wana mapepo.ukiangalia kwa haraka utaona kuwa nguruwe walioingiliwa na mapepo na kufa siku ili walikuwa wale tu waliokuwa eneo lile na siyo nguruwe wote wa israel.

Hii mkuu tunaita stereotyping yaani unachukua tabia moja ya kitu kimoja na ku generalize kuwa jamii nzima ya vitu hivyo vina tabia hiyo.hapa umewakamata watu kwa uoga na hisia tu.hata wale wenye imani zao zimeyumba.ukiwauliza wote waeleze ni kisa kipi walishawahi kupata kuhusu midoli kati ya elfu utakuta ni mmoja tu ndiyo mwenye stori aliyoishuhudia zaidi ya stori za kuambiwa na kusikia

Umeenda vizuri lakini hukuzingatia kwa kina andiko langu sikumanisha kila mdoli Pasco naye alitahadharisha kuhusu hilo na tukaeleweshana na akanielewa
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom