Vioja vya watoto wadogo (0-5years), tuambie vioja vya mwanao

Vioja vya watoto wadogo (0-5years), tuambie vioja vya mwanao

Watoto katika hatua zao za ukuaji na kujifunza wanakuwa na mambo flani flani ya kufurahisha sana yaani mwanao anaweza kukuvunja mbavu balaa.
Mfano
1. Mwanangu (1.5years) anaweza kuwa anatazama TV akisikia unaongea na simu au umeweka music kwenye simu anakimbia kuja kuangalia simu hata kama TV ilikuwa na TV program ya katuni nzuri kiasi gani[emoji23] [emoji23] [emoji23]

2. Ukitaka alale we nenda kitandani weka music kwenye simu yako atakuja mwenyewe hata kama alikuwa anakwepa kulala[emoji23]

3. Anaheshimu simu yangu kama kituo cha polisi ila ya mama yake kashaipasua ukiiona utajua mama yake anafanya kazi idara ya miamba (geology)[emoji23]

4.Kupenda safari akiona mtu anatoka tu anaanza kuaga bye bye akijua nayeye anahusika na safari[emoji23] [emoji23]

5. Chakula kikiwa tayari, kabla sijaitwa kula yeye akiona mambo yako tayari anakuja kunipigapiga mgongoni(hajajua kuongea) akiashiria msosi tayari basi ukipotezea anaenda anarudi mpaka utakapoinuka[emoji23] [emoji23]

6. Mwanangu anatabia flani kama wivu, akiona naongea na mama yake mara nimemshika mkono tunaongea kama jambo la siri anakuja fasta analia anataka mama yake ambembe[emoji23]
Nadhani hajajua kwamba mama yake ni mke wangu[emoji23] [emoji23] [emoji23]

Hivi ni baadi ya vituko vya watoto mdau ongeza vya mwanao
Watoto wanaleta raha sanaaa
View attachment 521347
Nilitoka nae nje mida ya usiku alipouna mwezi akasema Baba nataka ileeee (mwezi)alilia usiku kucha
 
Mi wa kwangu balaa natamani akue kidogo labda nitapata zuri la kueleza, leo ni wiki ya tatu sijalala nakesha, dogo analala mchana wakati mimi nipo job, usiku halali na akilala mikononi ukimuweka kitandani tuu yani kabla hata hujakiacha kitanda kishaamka na kelele nyingi, kingine asee usikae karibu na mamaake ugomvi wake c mdogo atalia hapo hadi utashangaa, kingine tangu wiki iliyopita hajacheka sijui ndo kutabasamu hakuna. Ana miezi 4. Hataki kulazwa kama watoto wengine anapokuwa macho, yeye anataka kukaa na anakaa...huyo ni mdogo, kakayake yeye anapenda ngumi, anajua bunduki zote kwa majina, hili nimejaribu kumuonya mamayake asiwe akimuwekea movie za mapigano zaidi ya cartoon lakini sijui huyu kijana anajifunzia wapi maana hakawii kukwambia anataka awe mwanajeshi sababu hapendi majambazi, huyo Ana miaka mi 4, anajua kikorea, kajifunza wapi mi sijui...ila ana shida moja anapenda tambi tuu, vyakula vingine kula mpaka mpigizane kelele sana na husingizia anataka kukojoa akienda harudi..ana huruma sana na mamayake, mjanja mjanja sana ukikasiririka atajua jinsi ya kukufanya ucheke tuu, shida usimuache na mdogo wake peke yao, unaweza kuta mtoto analishwa ugali.
Anataka kukojoa, akienda harudi. Nimeipenda

Sent from my SM-J700F using JamiiForums mobile app
 
IMG-20170609-WA0008.jpg
 
Siku ya Jumamosi alfajir mwanangu 5yrs aliamka saa kumi na moja. Akasema wanamitihani ya kufunga nusu mwaka.
Mke wangu akamuomba alale kidogo kwamba muda bado. Akaamka around saa mbili kasoro. Akagundua ilikuwa weekend

Jumatatu akaingia darasani kama kawa ile narudi jion nakuta taarifa alirudishwa ada sh 20000/ Roho iliniuma sana malaika huyu. kutoka Mil 1.2 kwa mwaka 20 elfu unamfukuza mtoto?

Kwa sasa namuhamishia shule nyingine
Ina maana hata paper hakufanya kisa 20k/-?

Sent from my SM-J700F using JamiiForums mobile app
 
Wakwangu ana miaka 4 ila me nikifika hom Dogo anakua na jeuri kama walikua wanaangalia movie na Dada wa kazi basi nikisha ingia anajiamini ye ndo anachagua movie ya kuweka kama NI katuni lkn nikiwa spo anakua mtulivu utamsikia mama ake anamwambia we ukishamuona baba ako unakua msumbufu coz UA naumia nikimuona anapgwa nampenda sana chalii yangu maana nlimpata kwenye vurugu za ujana na yy anajua
 
Wa kwangu ana miaka 3, kuna siku nimetoka safari nimekaa sebuleni akanifata na kuniuliza "baba leo unalala na mkeo?"
Siku ingine naongea nae kwenye Simu nikamtia mkwara ili ale chakula nae akanambia " baba ntakufumua" Daaaahh nkaona sasa hapa ipo haja ya kununua bunduki mapema.
Ikitokea akaona nimemshika mkono tu mama ake anakasirika sana na kwakua anajua mi haniwezi inabidi aanze kumpiga mama ake ili atoke hapo nilipo (Huyu jamaa anajionaga kama ye ndo ana hati miliki kwa mama ake)
Watoto ni raha sana, wana mambo yao ambayo ni ya kushangaza na kufurahisha kwa pamoja.
Ajui kwamba mamake ni mkeo
 
Mimi ka bint kangu karembo sana kana timiza mwaka keshokutwa, toka mama ake alipokuwa mja mzito nilikuwa nikimwambia unaenda kuni zalia GENIUS akawa anacheka ,ilikuwa tukiwa tumekaa tuna watch movie namlalia miguuni af namshika tumbo naongea na mtoto namwambia " hv unajua ww ni GENIUS ? " mke wangu anacheka af ananiambia nimeshamwandalia karai la maparachichi atakuwa anauza basi ananicheka maana mm nakasirika namwambia mwanangu ni Genius, sasa nilikuwa natamani sana mtoto wa kike na kweli nashukuru Mungu akanipa wa kike (GENIUS) basi akazalia sasa ni mjanja kiasi flani sijui nani kamfundisha ila akiwa na miezi nane mwishoni hapa alipoanza kusimamia kwenye kochi au kitandani ,ukimpa kalama anashika kabisa kama anataka kuandika ,siku moja nikamuuliza mama ake huyu akaniambia ww siulishamwambiaga yy ni GENIUS toka akiwa tumboni? Basi nafurai sana akisema vile ,mtoto huyu nimeanza kumuona anatumia ma left kila nikimpa kitu ashike mkono wa kulia anaamishia wakushoto ,namnyang, anya namuhamishia wakulia ananipiga anarudisha wakushoto, sasa sijui nimwache tu atumie ma left, kingine akiniona natoka ananililia anajua ni safari anampungia mama ake anamwambia "aiiii" akimaanisha baii ,anajua kuita baba ,mama na pia sasa ameanza kurusha hatua moja moja .anapenda remot sana na simu ,akiona naongea na simu yy anachukua remote anaweka sikiona anapiga kelele kama anaongea na mtu ila umuelewi, akinikitu nimekaa na laptop anachukua mouse yan anashika kama vile inavyoshikwaga vizuri kabisa na anaizungusha anafurahi akiona kale kamshale ka mouse ila ku click hawezi maana kimkono kidogo, nikimpokonya anaamia kwenye keybord anabofya na kakidole kamoja sasa nikimtoa hapo ni vita, nampenda sana mwanangu, nikiwa namkiss mama ake au namnong, oneza af yy alikuwa anacheza ataacha af atanikata jicho ilo kaah mpka naacha ,af nakauliza nini wewe unaniangalia. Af anacheka. Anapenda kunyonya na kunyonya kwake kama vile vita maana ananyonya kwa sarakasi atulii atabinuka hv kama amelala ananyonya ataweka mguu juu mara abinuke mara hv ukimshika atulie analia yani kama uko karibu utakanyagwa utawekewa miguu mpka basi ,nakumbuka siku mama ake ananiambia mja mzito nilitaka kukimbia maana mtoto wa soja umempa ujauzito ilikuwa kasheshe ila nashukuru nilijikaza kiume nikajitoa na hakika watoto ni Baraka sana kwa Mungu na hata kama ulikuwa huna kitu utashangaa tu pesa ujui zinatoka wapi yani unaona tu vitu vinatirirka kama vile ww tajiri kumbe tu mtoto kaja na baraka zake nampenda mke wangu kwakuniletea sweet baby girl. Nawashauri jamani usikatae mimba kama ni yako uwezi jua huyo mtoto atakuwa nani,.


Kikubwa nafurahi kwamba nina video za HD na still picha nikimaanisha documentary za toka mama yake alipokuwa na ujauzito na mpka dogo kazaliwa mpka sasa hv kila mara huwa nashuti video zake nakumuhifadhia so akikuwa ntazi edit nakufanya iwe documentary toka mama yake akiwa mja mzito mpaka hapo zitakapofikia ,huwa nikiwa mbali nao nafungua naanza kuziangalia nakuona kwamba hili jambo nililopitia mpka hapa ni Mungu huwa naenjoy sana nnapo kaa kuona hzo video vituko nk .
 
Mm wa kwangu alikuwa analilia kwenda shule kila siku, alipofikisha miaka miwili na miezi tisa nikamuanzisha shule, alienda siku mbili, siku ya tatu namuamsha anakataa anasema imetosha.[emoji23][emoji23]
Hahahahaaaa duh na ada ulikua ushalipa?watoto hawa jamani
 
Yani naona kila mwenye mtoto utaskia nimtundu mala anaakili sana mala mjanja mjamja mala nini naona sifatu inamaana nyie wenye watoto wote hakuna mwenye mtoto zoba anae lialia nakulamba kamasi mdawote anae pigwa nakila mtoto humu hakuna du!!! Ebu ongeeni ukweli wenu msifate mkumbo
Hakika wewe huna watoto, maana ukiwa mzazi unajua kwa uhakika mdomo unaumba haswa ukimsemea mwanao mambo ya ovyo ovyo kama unavyo dai wewe!
Mtoto ni hazina kutoka kwa MAULANA MOLA WETU, kwa nini nimnenee mambo ya ovyo! Naomba soma Zaburi ya 1 yote!
 
Mwenye Enzi Mungu bariki watoto wa Nchi yangu Tanzania milele yote!
 
Yaani sisi wenye watoto wakubwa zaidi ya hapo mmetutenga, au tusimulie tu vioja vyo vya zamani!?
 
Kuna siku nimerudi home nimekuta Rungu la mgambo mezani sebureni, nikauliza hili rungu la nani na limefikaje? Akanijibu langu, mmh nikamuuliza umelitoa wapi? Akajibu st Mary's, umepewa? Hapana nimelichukua nimekuta mlinzi kalala nimelibeba akiamka nitampa, nikachukua Rungu hadi St Mary's maana niniapoishi nyumba inaangaliana na hiyo shule nikamkuta mlinzi anahangaika kuitafuta silaha yake ya jadi, nikamwambia leo umechukuliwa Rungu kesho atasepa na mkwasa kuwa makini...kweli kesho yake nimemkuta tena dogo yupo na mlinzi mwingine nje ya geti anamuuliza hiyo bunduki gani? Unapiga? Inauwa jambazi? Naomba nione? Nikaona sasa huyu dogo anakoelekea sio kuzuri, maana mkiwa mnatazama movie ikiwa na ngumi utaulizwa maswali hadi kero, baba, yule ndo steering? Utajibu wee na muda mwingine na challenge namwambia hapa yule ni Audi, anasema wewe baba unazeeka vibaya yule sio adui yule ni stering bada unanidanganya, akiona bunduki anastuka kabisa utamsikia enheee hili ni bonge la muvi mi ndo napendaga, dogo anazingua nilichoamua nimempeleka kijijini akake huko japo miezi kazaa ili akirudi awe na akili zingine.....na huko kwa bibiyake alipo ni kesi za utundu tuu...chakula anapenda mrenda na ugali, na Tambi, ila ni mjinga akiwa na usingizi anakuwa kama kiteja flani hivi, hapendi kulala mchana. Ana miaka mi 3 na miezi 10, nimemuanzisha chokechea, ila ilibidi nimuhamishe maana anasema mwalimu wake hamfundishi vizuri na akifanya mazoezi yake mwalimu anamkataza...mtoto wangu mazoezi pekee anayojua yeye ni push ups..na wakati huyu bingwa anaanza kutembea kipindi ana mwaka amenitia hasara sana, alikuwa anakojolea simu na ktk fridge, yaani simu inaweza kuwa kitandani akahangaika akapanda akaishusha chini akaikojolea, Keisha akaitelekeza hapo akasepa zake, na ktk fridge ukiweka chakula unaweza kula mikojo anafungua anakojolea kisha anafunga anasepa....Namshukuru mungu sasa amekua na ninateseka na mdogo wake ambae yeye ni mabundi halali usiku.
 
Back
Top Bottom