Viongoiz jifunzeni kufuata utawala wa sheria! Mkuu wa mkoa manyara huna mamlaka ya kuzuia Uhamisho wa Watumishi wa Umma

Viongoiz jifunzeni kufuata utawala wa sheria! Mkuu wa mkoa manyara huna mamlaka ya kuzuia Uhamisho wa Watumishi wa Umma

kichongeochuma

JF-Expert Member
Joined
Jan 21, 2024
Posts
1,669
Reaction score
2,864
Nchi hii ifike mahali tuwe na chombo kinacho wasimamia hawa viongozi maana nikama wakisha kuwa na madaraka ya juu basi wapo overall, Haya ya kuendelea kuwaacha waongoze kwa utashi wao na sio kuzongatia sheria kuna siku yatatokea ya Dr. Kleruu na mwamwindi

Mkuu wa mkoa kwa utashi wake anasimama kutangaza kufuta uhamisho wa watumishi wa umma kunyume kabisa na sheria za utumishi wa umma hayo mamlaka anayatoa wapi?

Kwani hakuna sheria zinazo simamia na kuongoza utumishi umma na maswala haya ya uhamisho wa watumishi wa umma ?

Kwamba kwa sasa tanzania ilipo fika ni kwamba utashi wa kiongozi ndio utaamua aendeshe vip eneo lake la utawala na sio kwa mujibu wa sheria?

Tanzania inatatizo sana la kiutawala kiasi kwamba kila kiongozi mwenye mamlaka ya juu anajisikia yeye kuruhusu au kuzuia jambo kwa utashi wake na hakuna mamlaka inayo pinga hii ni kutokana na madhara ya kikatiba na kulindana

Kwa nchi hii ilivyo inawezekana kabisa mkuu wa mkoa akasimama na kutangaza wananchi wote ndani ya mkoa wangu kuanzia kesho mvae kaptula na kukawa hakuna chombo cha kumpinga

Viongozi zingatieni na mfuate sheria kama mnavyo taka mnao waongoza wafuate sheria acheni kuongoza kwa utashi wenu.

Nilitegemea kama kuna vyombo vinavyo simamia hawa watumishi kama vyama vyao vya wafanyakazi vingemrekebisha mkuu wa mkoa manyara na kumwambia bayana asivuke mipaka yake ,ni haki ya mtumishi kuhama na akihamishwa anatakiwa kulipwa kwa mujibu wa sheria na sio utashi

MKUU WA MKOA MANYARA AZUIA UHAMISHO

👇👇👇👇👇👇👇👇👇

 
Vip unaona kama kuna kiyahudi hapo hujakielewa ?
Kubali ushauri kujua kuandika Kiswahili,sio kigezo prkee kuwa unaweza kuwadilisha hoja Kwa kiswahili na ukaeleweka...
Mkuu wa Mkoa kavunja Sheria gani,amevunjaje hiyo Sheria...fafanua!
 
Mkuu..!! hua kinaandikwa kisa kwanza, maoni, malalamiko na mitazamo binafsi baadae.

Binafsi naona unalalamika lakini sijui unalalamikia nini, eleza kisa choke kwanza tuelewe kero yako.
 
Mkuu..!! hua kinaandikwa kisa kwanza, maoni, malalamiko na mitazamo binafsi baadae.

Binafsi naona unalalamika lakini sijui unalalamikia nini, eleza kisa choke kwanza tuelewe kero yako.
Ukiona hivyo ujue uelewa wako ni mdogo sana, katajwa mkuu wa mkoa manyara , kimetajwa kisa chake ,hujaelewa nini?
 
Nchi hii ifike mahali tuwe na chombo kinacho wasimamia hawa viongozi maana nikama wakisha kuwa na madaraka ya juu basi wapo overall, Haya ya kuendelea kuwaacha waongoze kwa utashi wao na sio kuzongatia sheria kuna siku yatatokea ya Dr. Kleruu na mwamwindi

Mkuu wa mkoa kwa utashi wake anasimama kutangaza kufuta uhamisho wa watumishi wa umma kunyume kabisa na sheria za utumishi wa umma hayo mamlaka anayatoa wapi?

Kwani hakuna sheria zinazo simamia na kuongoza utumishi umma na maswala haya ya uhamisho wa watumishi wa umma ?

Kwamba kwa sasa tanzania ilipo fika ni kwamba utashi wa kiongozi ndio utaamua aendeshe vip eneo lake la utawala na sio kwa mujibu wa sheria?

Tanzania inatatizo sana la kiutawala kiasi kwamba kila kiongozi mwenye mamlaka ya juu anajisikia yeye kuruhusu au kuzuia jambo kwa utashi wake na hakuna mamlaka inayo pinga hii ni kutokana na madhara ya kikatiba na kulindana

Kwa nchi hii ilivyo inawezekana kabisa mkuu wa mkoa akasimama na kutangaza wananchi wote ndani ya mkoa wangu kuanzia kesho mvae kaptula na kukawa hakuna chombo cha kumpinga

Viongozi zingatieni na mfuate sheria kama mnavyo taka mnao waongoza wafuate sheria acheni kuongoza kwa utashi wenu.

Nilitegemea kama kuna vyombo vinavyo simamia hawa watumishi kama vyama vyao vya wafanyakazi vingemrekebisha mkuu wa mkoa manyara na kumwambia bayana asivuke mipaka yake ,ni haki ya mtumishi kuhama na akihamishwa anatakiwa kulipwa kwa mujibu wa sheria na sio utashi
Mbona unalalamika tu bila kuweka vifungu vinavyomzuia RC kufanya hivyo?
 
Ukiona hivyo ujue uelewa wako ni mdogo sana, katajwa mkuu wa mkoa manyara , kimetajwa kisa chake ,hujaelewa nini?

Ngoja nifanyie kazi uelewa wangu kwanza, ndio uniulize sijaelewa nini, saivi itakua bure tu!!
 
Hili li nchi linajiendea tu. Kila mwenye mamlaka ana sheria zake.
 
MGAWANYO WA MAJUKUMU

1.1.1 Mkuu wa Mkoa

  • Kifungu 61 (4-5) cha Katiba Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kifungu cha 5-7 vya Sheria za Tawala za Mikoa Na. 19 ya 1997 Mkuu wa Mkoa atasimamia kazi na shughuli zote za Serikali ya Muungano wa Tanzania katika Mkoa. Sheria husika ni pamoja na:
  • Sheria Na. 19 ya mwaka 1997 ya Uanzishwa ji wa Tawala za Mikoa, Mkuu wa Mkoa ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC)
  • Sheria Na. 24 ya mwaka 1966 ya Ulinzi na Usalama wa Taifa, Mkuu wa Mkoa ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama (KUU), Katibu Tawala wa Mkoa atasimamia Maagizo ya KUU.
  • Sheria Na. 16 ya mwaka 1964 ya Utumishi wa Umma, Mkuu wa Mkoa ni Mwenyekiti wa Kamati ya Uteuzi wa vijana Jeshi la Taifa (JKT)
  • Sheria Na. 7 na 8 ya mwaka 1982 ya Mamlaka za Serikali za Mitaa, Mkuu wa Mkoa anawajibika kusimamia Halmashauri za Wilaya.
  • Kutoa ushauri wa kitaalam kwa Halmashauri ili ziweze kutoa huduma bora kwa wananchi.

1.1.2 Katibu Tawala wa Mkoa

  • Katibu Tawala wa Mkoa ana Jukumu la kumshauri Mkuu wa Mkoa na kuwa mtekelezaji Mkuu wa shughuli za uongozi wa Sekretarieti ya Mkoa kulingana na sheria ya Tawala za Mikoa Na. 19 ya 1997. Pia ni mshauri Mkuu wa Mkuu wa Mkoa katika masuala ya sheria, kanuni na taratibu za uendeshaji wa shughuli za Serikali za Mitaa. Aidha Katibu Tawala wa Mkoa anawajibika kwa kwa fedha zote za Sekretarieti ya Mkoa.

Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC)

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) ipo kwa mujibu wa (Kifungu cha 9 cha sheria ya Tawala za Mikoa Na. 19 ya 1997). RCC ni chombo cha kutoa ushauri fasaha utakaomsaidia Mkuu wa Mkoa kutoa miongozo ya utekelezaji Mkoani. Pia ni sehemu pa kujadili mambo yote ya Mkoa na kutoa fursa nzuri zaidi ya kushauriana na kuratibu mipango ya maendeleo na utekelezaji wake.

1.1.3.1 Wajumbe wa Kamati ya Ushauri ya Mkoa

  • Mkuu wa Mkoa (Mwenyekiti)
  • Wakuu wa Wilaya
  • Wenyeviti wa Halmashauri
  • Wakurugenzi wa Halmashauri
  • Wabunge wote wa majimbo
  • Wabunge viti maalum wote
  • Katibu Tawala wa Mkoa (Katibu)

1.1.4 Sekretarieti ya Mkoa

Majukumu ya Msingi ya Sekretarieti ya Mkoa:

  • Sekretarieti ya Mkoa ina wajibu wa kumshauri na kumsaidia Mkuu wa Mkoa kutekeleza majukumu yake, hususan:-
  • Kudumisha Ulinzi na Usalama
  • Kutoa ushauri wa kitaalam kwa Halmashauri ili ziweze kutoa huduma bora kwa wananchi.
  • Sekretarieti ya Mkoa inatoa aina nne za huduma za kuzisaidia Halmashauri kama ifuatavyo:-
  • Huduma za usimamizi wa kazi (management supportive services) katika fani za Serikali za Mitaa, sheria,Uchumi, takwimu, Maendeleo ya jamii na ukaguzi wa hesabu
  • Huduma za Maendeleo ya Kiuchumi (economic development support services) katika fani za kilimo, mifugo, biashara, Maliasilisi na Ushirika.
  • Huduma za Mipango ya ardhi na uhandisi (physical planning and engineering support services) katika fani za uhandisi, mipango miji na upimaji.
  • Huduma za jamii (Social Sector support services) katika fani za Elimu, Afya, Ustawi wa Jamii na Maji.

1.2 Ofisi ya Mkuu wa Wilaya

  • Madaraka yake yanatiririka kutoka kwa Rais kupitia kwa Mkuu wa Mkoa
  • Madaraka kwa mujibu wa sheria Na 19 ya 1997 (kumweka mtu kuzuizini masaa 48 mfulilizo)
  • Sheria Na. 7 ya 1982 kusimamia halmashauri
  • Sheria ya Ndoa Na. 5 ya 1971 kufungisha ndoa (civil marriages)

1.3 Katibu Tawala wa Wilaya

Ni mshauri na mtekelezaji Mkuu wa shughuli zote za Serikali katika Wilaya

Kumshauri Mkuu wa Wilaya katika masuala yahusuyo

  1. Ulinzi na Usalama
  2. Utekelezaji wa majukumu ya sherehe na dhifa
  3. Malalamiko ya wananchi
  4. Kuandaa makadirio ya matumizi
  5. Msajili wa ndoa
  6. Kusaidia Halmashauri kutekeleza majukumu yake kwa mujibu wa sheria

1.4 Afisa Tarafa

  1. Ni mshauri na msaidizi wa Mkuu wa Wilaya katika kutekeleza shughuli za Serikali katika eneo la Tarafa yake.
  2. Kuhimiza utekelezaji wa Sera za Serikali tarafani
  3. Amani na UTULIVU
  4. Kuratibu shughuli za maafa na dharura
  5. Kushughulikia malalamiko ya wananchi
  6. Kusimamia na kuhimiza shughuli za maendeleo
 
Back
Top Bottom