Wildchild
JF-Expert Member
- Aug 29, 2018
- 19,411
- 21,938
Ulizoeshwa kunyimwa uhuru ndio maana wewe😂Huu Uhuru wa kujieleza unafanya hii Nchi inakuwa Ngumu sana..,
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Ulizoeshwa kunyimwa uhuru ndio maana wewe😂Huu Uhuru wa kujieleza unafanya hii Nchi inakuwa Ngumu sana..,
Kwa mujibu wa yeye na familia yakeKwa mijibu wa... nani?
Labda huyo Mkwawa tu ila hao wengine mmh!
'Some people see things and say why I see things and say why not'?
Why number 5 and 9?
Why not Tundu Lissu and Mtikila?
Sidhani kama hao uliowataja wamewahi kuwa Viongozi katika mamlaka, Bali ni wanasiasa.Why number 5 and 9?
Why not Tundu Lissu and Mtikila?
🤣🤣🤣🤣Mh Tungu Lisu
Mh Mbowe na Nyerere
Wanaofuatia ndio mama Samia, mzee Mwinyi, Kikwete nk
Rais gani uchafu uleKwani Tundu alipokuwa Rais wa TLS alikuwa messenger? Au mtikila alipokuwa Mwenyekiti hakuwa kiongozi mwenye mamlaks?
Nani alikuambia kuwa kifo ni adhabu?!, watu wajinga mbona mnaendelea kuzaliwa?,Na wote wamekufa?. Malipo ni hapa hapa dunian watendeee wema binadamu wenzio bila dhuluma utaishi umri mrefu
Kwahiyo Babu zako, babaako, mamaako na wewe mwenyewe hamtakufa? PUMBAVU!!!Na wote wamekufa?. Malipo ni hapa hapa dunian watendeee wema binadamu wenzio bila dhuluma utaishi umri mrefu
Toa yule muuaji wa tatu! tupa kule! asituharibie hii list. Weka Aboud Jumbe afadhaliTanzania imebahatika kuwa moja ya nchi iliyopata kuwa na viongozi bora kabisa Afrika na hata duniani kwa ujumla.Viongozi hao wamepata kuwa na mchango mkubwa Tanzania na hata kwa bara la Africa. Tunaona mifano ya Mwl. Julius Kambarage Nyerere ambaye amepigania uhuru si kwa nchi ya Tanzania tu bali amekuwa na mchango mkubwa katika harakati za uhuru kwa nchi jirani kama Afrika Kusini, Zambia na Msumbiji.
Tanzania pia imepata kuwa na wanaharakati na wapigania uhuru mahiri walioweza kuitwaa nchi kutoka katika kucha za wakoloni. Tunaona wapigania uhuru na wanaharakati kama Kinjekitile Ngwale, Bwana Abushiri na Bibi Titi Mohammed. Viongozi kama Mtemi Isike, Chifu Mirambo, Mangi Meli na wengineo wengi ambao walikuwa viongozi wa kimila walikuwa mstari wa mbele katika mapambano ya uhuru na hatimaye kuikomboa na kutupatia Tanzania hii tunayoifurahia leo.
Bila kupoteza muda, Naomba niweke orodha fupi ya viongozi waliopata kuongoza Tanzania walioacha alama kubwa na historia ya kipekee kwa ubora wao na uwezo wao wa kiuongozi ambao pasi na shaka uliacha alama kubwa kwa watanzania.
Kwa sasa nitaweka orodha tu kwa kifupi ila nitarejea kuelezea kila mmoja kwa undani zaidi.Pamoja na kuongeza orodha mpaka kufikia kumi (10) Bora.
Updates; Moderators naomba mnibadilishie Title iwe Kumi (10) Bora badala ya Tatu (3) Bora. Ahsante
Viongozi Kumi (10) bora kuwahi kuwepo Tanzania.
1. Mwl.Julius Kambarage Nyerere (Rais wa kwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania)
View attachment 1752017
2. Edward Moringe Sokoine ( Waziri Mkuu wa Tanzania 1977–1980 na 1983 - 1984)
View attachment 1752018
3. John Pombe Magufuli (Rais wa Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania)
View attachment 1752024
4. Chief Mkwavinyika Munyigumba Mwamuyinga (Mkwawa) - Chifu wa kabila la Wahehe
View attachment 1752828
5. Benjamin William Mkapa (Rais wa Tatu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania)
View attachment 1752030
6. Rashidi Mfaume Kawawa ( "Simba wa Vita" - Waziri mkuu wa Tanzania 1972 - 1977" )
View attachment 1752641
7.Ali Hassan Mwinyi ( Rais wa Pili wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 1985 - 1995 )
View attachment 1752648
8.Oscar Salathiel Kambona ( Waziri wa Mambo ya Nje 1963–1966 )
View attachment 1753512
9. Jakaya Mrisho Kikwete ( Rais wa Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 2005 - 2015)
View attachment 1753513
10. Abeid Amani Karume ( Rais wa kwanza wa Zanzibar 1964 - 1972 )
View attachment 1753522