Viongozi ndiyo wanaokwamisha mchakato wa mabadiliko, FCC yatoa taarifa leo. Mashabiki na wanachama wa Simba mtadanganywa hadi lini?

Hivi unadhani Mo na GSM wanafaidika sana na hayo matangazo ukilinganisha na wanachokitoa? Jiulize Vodacom wanadhamini ligi nzima kiasi gani?
 
Mbona hausemi usajiri na mishahara?
Au unataka kutuaminisha kuwa MO anapata zaidi kuliko simba inavyopata kwa Mo?
 
Yanayoendelea katika klub yetu hii hata Mangungo asingediriki kukubali lakini kwa sababu watu wametanguliza matumbo acha miaka mitatu baada mahakamani itakuwa ofisi klub.

Lets say mo ameacha timu now je kuna mwanaichi anaweza kuchangia timu mpaka ifanye usajiri mkubwa kama huu na mishahara?
 
Ha ha ha ha jezi imejaa ma Mo!
 
Mwaka huu huu alisema hawezi shindwa kuweka billion 20
 
Mo Simba Arena, Mo Simba foundation, Mo energy, Barbra jamaa ndo anapata sana kuliko simba
Gharama za camp na mishahara na usajili unavijua?

Miaka mingapi Simba imekaa hata uwanja wa kucheza rede hawana ?
 
Kanjibay mjanja mjanja sana yaani ukisoma hapo no.6 utagundua kiasi kilichopo kwenye mkataba sio hiyo billion 20 inayotajwa mitandaoni.
20B ni kudanganyia mbumbumbu kwenye vyombo vya habari. Hela halisi ni ndogo sana.

Inaelekea kuna kitu Kigwangala anajua. Mo angemkopesha zile piki piki lisengebumburuka.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…