Sesten Zakazaka
JF-Expert Member
- Sep 10, 2017
- 10,559
- 19,101
Sizungumzii matokeo ya juzi kati ya Simba na mtani wetu Yanga bali hizi ni lawama za muda mrefu kwamba kocha mkuu hua anaingiliwa majukumu yake, kwanza ya kuchagua wachezaji wanaosajiliwa na pili hata kupanga timu kwenye baadhi ya mechi.
Malalamiko ya Patrick Aussen kuhusu jambo hilo sio ya kwanza lakini angalau yeye alijitokeza wazi kusema. Kuna baadhi ya wachezaji kama James Kotei hakutaka waondoke na wengine kama Mbrazil aliyevunjiwa mkataba yeye kama mwalimu hakushirikishwa kwenye kumsajili.
Nina wasiwasi hata huyu jamaa kutoka UD Songo hakua pendekezo la mwalimu Sven kwa sasa bali ni katika kulekule kukurupuka na kupiga dili kwa viongozi wa Simba kusajili wachezaji tofauti na mahitaji ya timu tena pengine kwa vile tu waliisumbua Simba pale ilipokutana na timu zao.
Mapungufu kwa Simba yapo kwa strikers, tena orthodox stickers, wale wanaojua kumalizia na wanaojua nyavu na nyavu zinawajua kama Kagere. Sijui ni kiasi gani Simba walilazimika kulipa ili kuvunja mkataba na yule Mbrazil lakini ni kweli walishindwa kupata mtu kama Makambo?
Kuna harufu ya ufisadi kwenye usajili. Haohao kina Manara na viongozi wengine wa Simba wanafaidika na pesa za Mo kwa namna moja au nyingine wanapofanya usajili na Board isiposhtuka mapema Simba SC itabakia kua timu iliyotumia pesa nyingi kwenye kusajili Tanzania lakini inajaza wachezaji wasiotumika wala kuhitajiwa kwenye timu
Malalamiko ya Patrick Aussen kuhusu jambo hilo sio ya kwanza lakini angalau yeye alijitokeza wazi kusema. Kuna baadhi ya wachezaji kama James Kotei hakutaka waondoke na wengine kama Mbrazil aliyevunjiwa mkataba yeye kama mwalimu hakushirikishwa kwenye kumsajili.
Nina wasiwasi hata huyu jamaa kutoka UD Songo hakua pendekezo la mwalimu Sven kwa sasa bali ni katika kulekule kukurupuka na kupiga dili kwa viongozi wa Simba kusajili wachezaji tofauti na mahitaji ya timu tena pengine kwa vile tu waliisumbua Simba pale ilipokutana na timu zao.
Mapungufu kwa Simba yapo kwa strikers, tena orthodox stickers, wale wanaojua kumalizia na wanaojua nyavu na nyavu zinawajua kama Kagere. Sijui ni kiasi gani Simba walilazimika kulipa ili kuvunja mkataba na yule Mbrazil lakini ni kweli walishindwa kupata mtu kama Makambo?
Kuna harufu ya ufisadi kwenye usajili. Haohao kina Manara na viongozi wengine wa Simba wanafaidika na pesa za Mo kwa namna moja au nyingine wanapofanya usajili na Board isiposhtuka mapema Simba SC itabakia kua timu iliyotumia pesa nyingi kwenye kusajili Tanzania lakini inajaza wachezaji wasiotumika wala kuhitajiwa kwenye timu