Viongozi wa dini hamjashtuka bado suala la usajili wa miaka mitano?

Viongozi wa dini hamjashtuka bado suala la usajili wa miaka mitano?

mshunami

JF-Expert Member
Joined
Feb 27, 2013
Posts
4,256
Reaction score
1,942
Kwamba tangazo limetoka kuwa mrudishe vyeti vya usajili vya kudumu mpewe vya miaka mitano mitano! Hamjashtuka bado? Mpo usingizini bado?

Mkiamka mtakuta mmefutwa. Serikali inaona njia rahisi ya kufuta usajili wa Kanisa kama la Gwajima na makanisa yale wasiyotataka ni hiyo.

Waliwahi kutishia Kanisa Katoliki wakati walipotoa waraka wa Kichungaji, wakatishia KKKT nao walipotoa waraka wao wa Pasaka.

Maana yake kama wangelikuwa wameshafutia makanisa yote usajili wa kudumu kama wanavyotaka kufanya na kutoa vibali vya miaka mitano, makanisa hayo yangelishafutwa.

Kuna wakati walikuwa na mgogoro mkubwa na Kanisa la Askofu Kakobe. Kwa mtindo wa vibali vya miaka 5 lingeshafutwa kirahisi. Unanyimwa tu kibali kipya.

Nilikuwa nafikiri ningesikia makelele kutoka kwa maaskofu lakini kimya.

Sio taasisi za dini ya Kikrsto tu, hata Waislamu pia. Taasisi kama za Shehe Ponda itakuwa rahisi kuzifuta kwa kuwanyima kibali cha miaka 5 mingine.

Huu ni mpango muovu sana kwa taasisi za dini. Ni mpango wa kidikteta wa hali ya juu sana ambao sijausikia hapa Afrika. Watumishi wa Mungu mnatishwa muogope kuikosoa serikali kwa kuogopa kuwa mtanyimwa vibali vya miaka 5.

Ukishafutwa kusajiliwa tena itakuwa ngumu.

Nilikuwa nategemea kusikua TEC, CCT, CPCT, BAKWATA, n.k. wakilisemea hili kwa nguvu zote.

Usajili ubaki kuwa wa kudumu, sio kuufuta na kutoa vibali vya miaka 5. Nilimweleza Padre wangu hilo akasema atalipeleka ngazi za juu lakini sijasikia likisemwa.

SHITUKENI!
 
Yote haya yamesababishwa na haka kadudu ka 19.

Hii chanjo imekuwa mjadala wa kidunia.

Hivi sasa mpaka waganga wa kienyeji wanajifanya wataalam kuliko wanasayansi wabobezi.
 
Waziri Simbachawane amekwisha toa ufafanuzi.

Imeisha hiyo.
 
Hapo ulipoandika wangefuta RC na KKKT umeandika future impossible tense.

Binafsi sitegemei TEC itoe tamko Kwa jambo dogo linaloeleweka na halina madhara Kwa RC.
Nadhani in the long run it will!
 
Hiyo miaka mitano inatafutwa loophole ya kunyima kibali baadhi ya huduma watakapoenda ku renew, hasa kama hujajifungamanisha na matakwa ya viongozi wa chama kikuu kuu.
 
Mfano wafungie kkkt je ndio watu hawatasali jumapili, tutazikana kama wapagani, tutaoana bila mafundisho, tutaenda kutubu kwenye ofisi za mtendaji , na jumapili wataifuta?
 
Mh. Waziri ametoa ufafanuzi mpya. Amesema taasisi zitakazohusika ni za kijamii tu, za kidini hazitahusika tena.
Ni hekima ya pekee sana imetumika hapa kwa sababu taasisi korofi kwa upande wa zile za kidini mpaka muda huu mimi nafahamu Kanisa moja tu. Ulikuwa ni usumbufu kwa taasisi zingine
 
AQEifm.jpg
 
Mh. Waziri ametoa ufafanuzi mpya. Amesema taasisi zitakazohusika ni za kijamii tu, za kidini hazitahusika tena.
Ni hekima ya pekee sana imetumika hapa kwa sababu taasisi korofi kwa upande wa zile za kidini mpaka muda huu mimi nafahamu Kanisa moja tu. Ulikuwa ni usumbufu kwa taasisi zingine
Huu siyo ufafanuzi bali ni kubadilisha tamko la awali. Walipima maji wakakuta kina kirefu ikabidi warudishe majeshi. Hizi serikali zetu ni za hovyo kweli kweli. Badala ya kujishughulisha na mambo makubwa wanakimbilia kutafuta namna ya kudhibiti uhuru wa wananchi.
 
Mh. Waziri ametoa ufafanuzi mpya. Amesema taasisi zitakazohusika ni za kijamii tu, za kidini hazitahusika tena.
Ni hekima ya pekee sana imetumika hapa kwa sababu taasisi korofi kwa upande wa zile za kidini mpaka muda huu mimi nafahamu Kanisa moja tu. Ulikuwa ni usumbufu kwa taasisi zingine
Noted!
 
Huu siyo ufafanuzi bali ni kubadilisha tamko la awali. Walipima maji wakakuta kina kirefu ikabidi warudishe majeshi. Hizi serikali zetu ni za hovyo kweli kweli. Badala ya kujishughulisha na mambo makubwa wanakimbilia kutafuta namna ya kudhibiti uhuru wa wananchi.
Huwezi kujua ni nini walikuwa wanatafuta kutatua, lazima kuna kitu walikuwa wanajaribu kushughulikia, tena kikubwa. Tafadhali usiwatukane.
 
Back
Top Bottom