Viongozi wa Klabu ya Simba mna maswali ya kujibu, michango ya Ujenzi wa Uwanja imeshia wapi?

Viongozi wa Klabu ya Simba mna maswali ya kujibu, michango ya Ujenzi wa Uwanja imeshia wapi?

Boran Jakutay

Senior Member
Joined
Apr 8, 2023
Posts
110
Reaction score
259
IMG_20230502_102511.jpg
Desemba 17, 2021, Klabu ya Simba ilizindua kampeni ya kuchangia ujenzi wa uwanja wao uliopo Bunju, Dar es Salaam.

Malengo ni kujenga uwanja wenye uwezo wa kuingiza watazamaji zaidi ya 30,000.

Ofisa Mtendaji Mkuu wa Simba kwa wakati huo, Barbara Gonzalez, ndiye aliyekuwa akizungumza zaidi siku ya uzinduzi huo akiwa sambamba na Mwenyekiti wa Simba, Murtaza Mangungu.

Tangu mchakato ule umeanza hadi leo ni takribani miaka miwili, hakuna tulichoambiwa nini kinaendelea.

Mara ya mwisho niliona viongozi wa Simba wakienda kuangalia eneo la uwanja huo na kuanza mchakato wa kuzungushia uzio baada ya kuwepo kwa mvutano baina yao na majirani zao huko Bunju.

Kinachonishangaza zaidi, zile fedha zilizokuwa zinachangwa, haijatoka figure kamili ya kwamba kilipatikana kiasi gani kwa sababu mashabiki na wanachama wa Simba walikuwa wakichanga kuanzia Shilingi 1000 za Kitanzania.

Projekti ya uchangiaji ikafa kihuni bila ya kuwepo kwa maelezo, hapa ni wazi kuna upigaji umefanyika.

Sasa kama kuna viongozi wanaanzisha vitu kwa kutumia rasilimali za klabu kisha wanajaza matumbo yao, inabidi tuwe nao macho kwani hawana faida katika maendeleo ya soka letu.
 
Ndio zimesajili Okra , sawadogo na Mohamed Qottara.

Kuna muda mo Alikuwa anajitoa timu ilikuwa na Hali ngumu.

WANASIMBA wenzangu Mo anatuchezea sana.
 
View attachment 2606991
Desemba 17, 2021, Klabu ya Simba ilizindua kampeni ya kuchangia ujenzi wa uwanja wao uliopo Bunju, Dar es Salaam.

Malengo ni kujenga uwanja wenye uwezo wa kuingiza watazamaji zaidi ya 30,000.

Ofisa Mtendaji Mkuu wa Simba kwa wakati huo, Barbara Gonzalez, ndiye aliyekuwa akizungumza zaidi siku ya uzinduzi huo akiwa sambamba na Mwenyekiti wa Simba, Murtaza Mangungu.

Tangu mchakato ule umeanza hadi leo ni takribani miaka miwili, hakuna tulichoambiwa nini kinaendelea.

Mara ya mwisho niliona viongozi wa Simba wakienda kuangalia eneo la uwanja huo na kuanza mchakato wa kuzungushia uzio baada ya kuwepo kwa mvutano baina yao na majirani zao huko Bunju.

Kinachonishangaza zaidi, zile fedha zilizokuwa zinachangwa, haijatoka figure kamili ya kwamba kilipatikana kiasi gani kwa sababu mashabiki na wanachama wa Simba walikuwa wakichanga kuanzia Shilingi 1000 za Kitanzania.

Projekti ya uchangiaji ikafa kihuni bila ya kuwepo kwa maelezo, hapa ni wazi kuna upigaji umefanyika.

Sasa kama kuna viongozi wanaanzisha vitu kwa kutumia rasilimali za klabu kisha wanajaza matumbo yao, inabidi tuwe nao macho kwani hawana faida katika maendeleo ya soka letu.
Hudhuria mkutano mkuu wa mwaka, utasomewa mapato na matumizi, utapewa kitini ambacho utakuwa na fursa ya kukisoma kwa utulivu. Hapo unaweza kuibua hoja iwapo kuna mahali pana utata.
Kama hukupata fursa ya kuhudhuria mkutano huo, basi walau jitahidi upate kitini, ili hoja yako unayoiibua iwe na rejea nzuri, kama vile ukurasa fulani, kifungu namba fulani, kifungu kidogo namba fulani nk. Vinginevyo ni kama unataka usomewe taarifa ya mapato na matumizi upya ukiwa peke yako
 
Ndio zimesajili Okra , sawadogo na Mohamed Qottara. Kuna muda mo Alikuwa anajitoa timu ilikuwa na Hali ngumu.
WANASIMBA wenzangu Mo anatuchezea sana.
Tusaidie kumtafuta mwekezaji mwingine basi kwanza
 
Ndio zimesajili Okra , sawadogo na Mohamed Qottara.

Kuna muda mo Alikuwa anajitoa timu ilikuwa na Hali ngumu.

WANASIMBA wenzangu Mo anatuchezea sana.
Unataka kusema ile bilioni 1.5 aliyotoa mwekezaji wenu kwa ajili ya usajili wa hao wachezaji haikutosha, kiasi cha kwenda kukwapua tena hela za ujenzi wa uwanja!!!
 

Viongozi wa Klabu ya Simba mna maswali ya kujibu, michango ya Ujenzi wa Uwanja imeshia wapi?​

Ungeuliza na kwa Yanga pia kwani wakati huo nao wachangisha kwa wapenzi,mashabiki na wanachama wao!
 

Viongozi wa Klabu ya Simba mna maswali ya kujibu, michango ya Ujenzi wa Uwanja imeshia wapi?​

Ungeuliza na kwa Yanga pia kwani wakati huo nao wachangisha kwa wapenzi,mashabiki na wanachama wao!
Yanga hatuja wahi kuchangishana kujenga uwanja
 
Back
Top Bottom