Mtoa Taarifa
JF-Expert Member
- Sep 21, 2024
- 213
- 671
Amesema hayo leo katika taarifa yake kwa umma iliyochapishwa kwenye ukurasa wa mtandao wa kijamii wa sekretarieti ya maadili ya umma na kuongeza kuwa, hatua hiyo inalenga kuhakikisha uwazi na uwajibikaji katika usimamizi wa rasilimali za umma, sambamba na kukuza imani ya wananchi kwa viongozi wao.
Katika taarifa yake, Kamishna Mwangesi amesisitiza umuhimu wa kuzingatia masharti ya Ibara ya 132(5)(b) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 na kwamba utekelezaji wa takwa hili ni sehemu muhimu ya kulinda maadili ya uongozi wa umma.
Tamko la Rasilimali na Madeni linatoa taswira ya uadilifu wa kiongozi katika utumishi wa umma na linapaswa kuwa halisi na lenye taarifa sahihi, likijumuisha mali zote pamoja na madeni yanayowahusu moja kwa moja.