implicit memory
JF-Expert Member
- Nov 14, 2024
- 806
- 926
Thibitisha!!!Ni baada ya TLs ya Mwabukusi Kuhongwa Gari na serikali na mama Abduli
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Thibitisha!!!Ni baada ya TLs ya Mwabukusi Kuhongwa Gari na serikali na mama Abduli
Ni mapema kumtuhumu mwabukusu. Bado sababu hazijajulikana za kuachia ngazi. Tukijua hizo sababu ndiyo tunyoshe kidole kwake kama ni udhaifu wake. Na kama ni matakwa yao binafsi hatunyoshi kidole kwakeDalili ziko wasi kwamba TLS sasa imemshinda Mwabukusi. Kuna mpasuko mkubwa na viongozi wenzake wameanza kumkimbia.
Ukimuona Mwabukusi anavyowananga wengine, unaweza kudhani anaweza hata kujiongoza yeye mwenyewe
====
Baadhi ya wanachama wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) mkoa wa Mwanza wametishia kuandamana hadi Ofisi ya Jaji Mfawidhi Mkoa wa Mwanza iwapo ombi lao la kuitishwa kwa uchaguzi kujaza nafasi za viongozi wa mkoa huo walioandika barua ya kujiuzulu halitozingatiwa.
Mawakili hao 46, wamejaza majina na kusaini fomu maalum (Petition) ya kushinikiza uongozi wa TLS ngazi ya taifa kuitisha uchaguzi wa kujaza nafasi za viongozi walioandika barua ya kujiuzulu nafasi zao ngazi ya Mkoa wa Mwanza.
Viongozi wanaotajwa kuwasilisha barua ya kujiuzulu ni Mwenyekiti wa TLS Mwanza (Chapter Convener), Msafiri Aloys Henga, Makamu wake (Vice chapter convener), Marina Mashimba na Mweka Hazina (Treasurer) wa TLS Mkoa wa Mwanza, Angelo Nyaoro.
Alipopigiwa simu kujua sababu za kujiuzulu, aliyekuwa Mwenyekiti wa TLS Mwanza, Msafiri Henga amethibitisha kuchukua uamuzi huo huku akisema hawezi kutaja sababu kwa kile alichodai hayuko kwenye mazingira mazuri ya kuzungumzia suala hilo.
Kwa upande wake, aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa chama hicho (Mwanza), Marina Mashimba amesema alijiuzulu wadhfa huo Agosti 21, mwaka huu na kuwasilisha barua kwa Mkurugenzi Mtendaji wa TLS.
Kwa upande wake, Rais wa TLS, Boniface Mwabukusi, amekiri kuwa na taarifa ya viongozi hao kuachia ngazi huku akisema tayari imeundwa kamati maalum ya kufuatilia sababu zilizochangia viongozi wa Mwanza kuchukua uamuzi huo.
Awali, Wakili Steven Kitale aliieleza Mwananchi kuwa tayari wamejaza majina na kusaini fomu maalum (Petition) ya kushinikiza uongozi wa TLS ngazi ya taifa kuitisha uchaguzi wa kujaza nafasi za viongozi na isipofanyika hivyo wataandamana kwenda kwa Jaji Mfawidhi Mkoa wa Mwanza.
Ila wewe mjinga ni muongo sn, 1970 wewe ulikuwepo na utapeli wako huu? hahahaNilimkuta hapo Milongo Primary early 1970 chipukizi wa TANU kutoka Dar tulipowatembelea 😂😂
Sijui kama hiyo shule bado ipo 🐼😂
Abaki Mwambugusi na dereva inatoshaWatoke kwani wamelazimishwa hata akibaki mwakabusi peke yake ni sawa
Hatuna muda wa kusubiri maelezo yake, sisi tumemaliza.Ni mapema kumtuhumu mwabukusu. Bado sababu hazijajulikana za kuachia ngazi. Tukijua hizo sababu ndiyo tunyoshe kidole kwake kama ni udhaifu wake. Na kama ni matakwa yao binafsi hatunyoshi kidole kwake
Hivi sasa hata washirika kawatenga!Sana, sijui kama kaacha ulevi siku hizi
Hiyo sio Public Money!Public money inahitaji accountability
Kelele zote za kutaka kuandamana DP World zote kwishaa!Sasa hivi anachota tu pale TLS, makazi yake yako Mbeya, kwa hiyo analipwa posho ya kukaa Dar, na analipiwa hotel ya nyota tano alale. Yuko Dar kwa takribani miezi sita akilala hotel
Shida mnakosa akili wala sio Elimu, Njoo na tafsiri ya neno "Fedha za Umma" usiandike upupu ambao hauulewi!Kama ulisoma Shule ya kata, tafsiri ya neno "public" Itakusumbua
Hakuna neno "Fedha za Serikali" ni Fedha za umma, Usiipe hio shingo mzigo wa kichwa!Unachanganya umma na serikali?
Umeona neno Umma hapo? Serikali inawekwa na Umma kijana, Jaza maarifa hicho kichwa chako!Mengine malizia sasa, nyie watoto wa ku-google mpaka muelekezwe sana ndio mnaelewa. Bila shaka umenielewa sasa