Super Sub Steve
JF-Expert Member
- Jul 9, 2011
- 17,404
- 10,900
Sasa jamani mtu akisema ukweli ndo anakuq mpuuzi.??tatizo walilo nalo yangu lipo pia kwa baba yenu ccm,nyote mmetia pamba maskioni amtaki kuskia ukweli..!!sie yetu macho.!!
Mbona basi hukujibu swala langu la pili? Au huko unakosema uko umefika kwa ungo?
Mimi sio Simba wala Yanga, lakini kwa mtazamo wangu mleta mada kaelezea ukweli mtupu wala si ushabiki, Kuna wakati tunatakiwa tuweke ushabiki pembeni tuukubali ukweli, hata kama jamaa wana madigrii ya Havard kwa hili wamechemka.
Swal lako umeuliza Botswana hawana utaratibu Wa visa on arrival umejibiwa wanao utaratibu Wa visa on arrival au usema ulitaka ufafanuzi zaidi,walihitajika kutoa dola 150 kwa ajil ya wachezaj watatu walipotoa wakaruhusiwa hii ndio maana ya visa on arrivalMbona basi hukujibu swala langu la pili? Au huko unakosema uko umefika kwa ungo?
Kwa anayefahamu hayo kama wewe, swala la umbumbumbu wa viongozi wa msafara linakosa mantiki, sanasana labda iwe ni ubahili ama ukata. Ila undani wa swali langu umeshaeleweka kwa niliyemuuliza, ameshanijibu na nimesharidhika.Swal lako umeuliza Botswana hawana utaratibu Wa visa on arrival umejibiwa wanao utaratibu Wa visa on arrival au usema ulitaka ufafanuzi zaidi,walihitajika kutoa dola 150 kwa ajil ya wachezaj watatu walipotoa wakaruhusiwa hii ndio maana ya visa on arrival
MFUKUZI;
Kabla ya kulumbana kusiko lazima, tujaribu kujibu maswala mawili rahisi lakini muhimu:
1. Yanga wanaweza kuwa mbumbumbu, sawa. Je, na Kenya Airways nao ni mbumbumbu kubeba abiria wasio na hati halali za kisafiria hadi Botswana kutoka Dar, au na wao pia wanawaogopa Yanga?
2. Je, Botswana haina utaratibu wa Visa on Arrival, yaani kupatiwa Visa baada ya kufika Uwanja wa Ndege?
Unataka nawe nikuulize kama umeshawahi kusafiri nje ya nchi kwa ndege? Airline gani itayokuchukua bila ya kuwa na Visa au uhakika wa kuipata kwenye airport unayoenda? Wanaorejeshwa airport huwa si kwa kukosa Visa, bali ni utata/kasoro kwenye visa hizo au utaratibu wa kuipata kwa walioahidiwa airport, maswala ambayo ni nje ya uwezo wa airline inayohusika wala Uhamiaji wa kiwanja walivhoondokea.Usichanganye mambo!!.. masuala ya viza hayahusiani na Airline. Unaweza ukasafiri na ndege lakini ukaishia Airport..
Wangapi wameshafiri kwenda Marekani au Ulaya na wakarudia Airport!!!?
Sometime ni busara kukubali kwamba kuna sehemu mambo hayakwenda sawa lakini si kuendelea kubishana kisa tu unatetea uongozi wa timu yako..!!
Unataka nawe nikuulize kama umeshawahi kusafiri nje ya nchi kwa ndege? Airline gani itayokuchukua bila ya kuwa na Visa au uhakika wa kuipata kwenye airport unayoenda? Wanaorejeshwa airport huwa si kwa kukosa Visa, bali ni utata/kasoro kwenye visa hizo au utaratibu wa kuipata kwa walioahidiwa airport, maswala ambayo ni nje ya uwezo wa airline inayohusika wala Uhamiaji wa kiwanja walivhoondokea.
Kama ni msafiri wa kimataifa, inshalla utakuwa unaelewa pia kwamba mbali ya airline husika, ofisi ya Uhamiaji ya uwanja wa ndege wa kuondokea nayo hawezi kukuruhusu kuuondoka bila ya Visa ya unakoenda au uthibitisho wa kuipata utapofika. Hata ungekuwa sahihi kwamba maswala ya Visa hayahusiani na airline, je hayahusiani na Afisi ya uhamiaji ya kiwanja cha kuondokea? Na kwa hili swala la Visa za Botswana tuseme na Uhamiaji JNIA nao hawakuwa wakijua kazi zao?
Hupaswi kuwa mpenzi wa Yanga, Simba wala timu yoyote nyengine kupata jawabu ya swala hilo.
Wasomi ambao hawafahamu protocol za SADC na nchi ambazo si wanachama wa SADC kama Rwanda na Kenya. Huenda wasomi walipitiwa!Haya mapenzi niue yanashida yake... Hebu acheni ushabiki wa kijinga. Katika hali ya kawaida unaposafiri nje ya nchi kuna nyaraka za kusafiria kwa abilia yoyote.. Vitu vya lazima ni Passport na Visa. Viza inaweza isitumike kama nchi zinamakubaliano ya kutokutumika kwake.. Ndivyo ilivyo kwa nchi za SADC..
Sasa issue iko wazi Rwanda, Cameroon na Burundi si wanachama wa SADC... Kucheza kwao YANGA haimaanishi wameshakuwa watanzania..
Lazima mkubali uongozi wa YANGA umekurupuka,, na huwezi ukasema eti waliwaachia wachezaji wa Zimbambwe.. Yaan mnataka kutuambia viongozi wa Yanga hawajui kwamba Zimbabwe ni mwananchama wa SADC...
Uswahili wetu tuuachage hukuhuku kwenye soka la bongo!!..
Kama hivi ndivyo unavyoamini, maana yake ni kwamba tatizo halikokwa viongozi wa msafara kama mtoa mada anavyotaka watu waamini. Kama ni tatizo, kwa mujibu wa maelezo yako haya, ni la Uhamiaji JNIA. Wenye akili zao timamu hawana sababu ya kuamini hivyo.Sielewi unachibishania kwa kweli!!...
Suala la kujiuliza Uhamiaji wa Botswana walikuwa na haki ya kuwazuia wakina Niyozima au la..? Kama ndiyo ni kwanini kama hapana ni kwanini.
Kama wanahaki jibu liko wazi kwamba Uhamiaji wetu ni wamagumashi period!!!
Kuhusu suala la Airline nadhani umeshijijibu mwenyewe... kwamba hata kama wakikubeba mpaka Marekani kama visa yako inamatatizo hawana namna ya kukusaidia utarudishwa tu. So wanaangalia just for formalities tu kuangalia yule anayetakiwa kusafiri ndiye yeye according to your passport na other documents.. Visa ikiwa fake au inamatatizo wao hawasiki utaenda kupambana na uhamiaji..
Naamini umeelewa..!!
Kama nchi unayokwenda hauitaji viza shirika la ndege hawahusiki mfano mtanzania akienda Hong Kong.Ulishawahi kusafiri nje ya nchi? Ni shirika gani litalokuruhusu kupanda ndege yake kwenda kwenye nchi ambayo huna viza yake, wala hairuhusu kukupatia viza hiyo utapotua kiwanjani kwao?
Wanahusika kujiridhisha kwamba ni kweli Visa haihitajiki; na kwa maana hiyo ni sawa na kuwa msafiri huyo anayo Visa.Kama nchi unayokwenda hauitaji viza shirika la ndege hawahusiki mfano mtanzania akienda Hong Kong.
Ha haa haaa! kabla haujakata tiketi lazima wakuulize unakwenda nchi gani.Wanahusika kujiridhisha kwamba ni kweli Visa haihitajiki; na kwa maana hiyo ni sawa na kuwa msafiri huyo anayo Visa.
Labda nawe unisaidie kumwelewesha hivyo mtoa mada na wafuasi wake; hicho ndicho ninachokieleza mimi. Kwamba viongozi wa msafara hawakufanya makosa kuondoka na wachezaji wasio na Visa, madhali imeshathibitika na airline husika pamoja na Uhamiaji wa JNIA kwamba wachezaji hao wangepata visa zao baada ya kufika Gaberone Airport. Tatizo liko wapi?Ha haa haaa! kabla haujakata tiketi lazima wakuulize unakwenda nchi gani.
Kama nchi unayokwenda inaitajika visa hawawezi kukuuzia tiketi mpaka waone visa kwenye pasi yako.
Lakini kama unaenda nchi ambayo hauitaji visa wao wenyewe wanakuuzia tiketi ya nchi unayokwenda.
Kimsingi siyo kila sehemu unayokwenda mpaka uwe na visa mkuu.
Na kama walijua yote hayo kwa nini walianza kulalamika kwamba wanafanyiwa hujuma na hadi kufikia kuanza kutoa ulinganisho kwamba wao waliruhusu tu pamoja na kwamba kulikuwa na wazimbabwe? hivi hawa Yanga wanahusika na mambo ya uhamiaji kumbe? Na baadaye wakamwaga hela ili waruhusiwe ina maana hao viongozi hawakujua taratibu zikoje?Labda nawe unisaidie kumwelewesha hivyo mtoa mada na wafuasi wake; hicho ndicho ninachokieleza mimi. Kwamba viongozi wa msafara hawakufanya makosa kuondoka na wachezaji wasio na Visa, madhali imeshathibitika na airline husika pamoja na Uhamiaji wa JNIA kwamba wachezaji hao wangepata visa zao baada ya kufika Gaberone Airport. Tatizo liko wapi?
Labda nawe unisaidie kumwelewesha hivyo mtoa mada na wafuasi wake; hicho ndicho ninachokieleza mimi. Kwamba viongozi wa msafara hawakufanya makosa kuondoka na wachezaji wasio na Visa, madhali imeshathibitika na airline husika pamoja na Uhamiaji wa JNIA kwamba wachezaji hao wangepata visa zao baada ya kufika Gaberone Airport. Tatizo liko wapi?
Viongozi wa Yanga wanaripotiwa kulalamika eti wachezaji wao Niyonzima (Rwanda), Tambwe (Mrundi) na Sherman (Mliberia) "wamezuiwa" kuingiwa Botswana kwa kile wanachodai ni "siasa za mpira".
Huu ni uswahili upande wa viongozi wa Yanga, wala sio siasa za mpira. Suala liko wazi sana, kwamba raia wa Rwanda, Burundi na Liberia wanatakiwa kuwa na visa ili kuingia Botswana. Sasa kama Tambwe, Sheman na Niyonzima hawakuwa na visa walitaka maofisa wa Uhamiaji wa Botswana wawaruhusu kuingia Botswana bila visa kwa kuwa tu wao ni wachezaji wa Yanga? Kumbuka Botswana ni kinara cha utawala bora wa sheria Afrika, viongozi wa Yanga msitake kuleta mambo yenu ya uswahilini mnayofanya huku Bongo. Mnadai hamukuambiwa mapema, kwani mliuliza ubalozi wa Botswana ikiwa hawa wachezaji wangeruhusiwa kuingia bila visa?
Na suala la kusema nyie mliwapokea huku kwetu wakiwa na wachezaji wageni kutoka Zimbabwe mnazidi kujionyesha mlivyo watupu kichwani katika mambo ya kawaida kabisa, kwa sababu raia wa Zimbabwe, nchi ya SADC kama Tanzania, hawahitaji visa kuja Tanzania. Na wala suala la wachezaji wa Zimbabwe kuingia Tanzania bila tatizo sio kwa sababu yenu Yanga. Uhamiaji waliwaruhusu wakijua Zimbabwe wanaingia Tanzania bila visa.
Mnadai mlilipa fedha nyingi kwa ajili ya kina Niyonzima, mnataka kutuambia mlitoa hongo au ada ya kawaida ya visa ya airport? Hela gani kubwa ambayo Botswana watadai kwa ajili ya visa pale airport, dola 50 kwa kila mchezaji? Ndio mnaita hela nyingi?
Na kwa wanachama wa hizi timu kama Yanga, chagueni viongozi ambao wameenda shule kidogo ambao mambo kama haya wanayaelewa sio kuokoteza watu mitaani na kuwapa uongozi kama hawa wa Yanga wanavyojidhalilisha hapa. Viongozi kama hawa wanatutia aibu ugenini.