Viongozi wa Yanga mmetutia aibu huko Botswana

Hizo ni tafsiri zako kwa mujibu wa walivyoripotiwa viongozi hao. Lisilopingika ni kwamba hakukuwa na tatizo kwa wachezaji hao kuondoka Dar bila ya Visa, wala hakuna tatizo kwa wachezaji hao kutakiwa kulipia Visa Gaberone. Mtoa mada aliyataja hayo kuwa ndiyo kiini cha udhalilishaji aliouzungumza. Wewe unahisi kwamba udhalilishaji ni kwa viongozi kufananisha Wazimbabwe wa BDN na Warundi, Waliberia na Wanyarwanda wa Yanga. Naweza kukubaliana nawe iwapo itathibitika viongozi hao wamefanya hivyo, ingawa hiyo ni mada tofauti. Siwezi kukubaliana na mtoa mada kwa sababu kasoro ya dhana yake iko kweupeni, haihitaji tochi!
 
Mimi sizungumzii kiongozi gani kasema nini au anajua nini, nazungumzia mtoa mada kakosea nini kwenye dhana yake kwamba kuondoa wachezaji Dar bila ya Visa ni udhalilishaji. Kwa sababu ikishathibitika kwamba alikosea kwenye dhana ya hoja yake ya msingi, mjadala wote uliosalia ni jamvi la ushabiki na utani wa wapenzi wa Yanga dhidi ya watani wao wa Simba.. Mimi si miongoni mwa yeyote kati ya hao.
 

Anaefanabisha kuingia kwa wachezaji wa sadc bila viza ana shida ya uelewa.


“Hizi ni siasa za mpira, Yanga tumeshangazwa na hili tuliuliza mapema kule katika ofisi zao za ubalozi wa Botswana jijini Dar es Salaam hatukuambiwa kama kuna hili la viza tunatakiwa kulifanya.

Hata wao wakati tunawapokea kule kwetu walikuwa na wachezaji wageni kutoka Zimbambwe, hawakufanyiwa haya, tumelazimika kutoa fedha nyingi ili kuwaondoa wachezaji wetu pale uwanjani,” alisema Tiboroha.
 
Kama kweli kiongozi huyo alisema hivyo, narudia tena kwamba nakubaliana na wewe. Ila mimi binafsi huwa sizipi uzito taarifa za baadhi yavyombo vyetu vya habari, hasa vinaponukuu watu. Bila ya kusikia mahojiano yenyewe, nitalazimika kwanza kumsikia mnukuliwa anasemaje juu ya hili.
 
Reactions: RR

Heeeeee...makubwaaaa...Jamaa katoa fact na bado unadai ni fitna
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…