Mara baada ya kifo cha Magufuli Chadema walishangilia Sana wakazani Magufuli alikuwa mbaya wao akina Tundu Lisu walikuwa waongo Kuja Tanzania wakisema hakuna Amani Sasa Magufuli hayupo tena kinachowakalisha huko ughaibuni ni nn au umasikini wenu ndio mlioutimia kutaka kutajirika kisiasa
mimi ninawauliza Chadema Kuna nn cha maana mmekipata? mmeishiwa kusalitiwa kila kona katiba mpya haipo yaani mmekoswa kila kitu kiufupi mmechanganyikiwa Sana
Katala Kikaja na Ng'hulima Lilanga walikua mawakala wa Chadema kwenye uchaguzi mkuu 2020, kata ya Dutwa, Wilaya Bariadi mkoani Simiyu. Usiku wa 27 Oktoba 2020 walipewa vitisho na viongozi wa CCM kwamba wasiende kusimamia kura za Lissu, kwa sababu wanataka Magufuli ashinde kwa 100% eneo hilo.
Wakapuuza vitisho hivyo. Oktoba 28, 2020 waliwahi vituoni alfajiri, mmoja akisimamia Dutwa A na mwingine Dutwa B. Wakiwa hapo walisikia taarifa kuwa kuna mawakala wamezuiwa kuingia vituoni na wengine wameingia lakini wakatolewa kwa nguvu na polisi.
Lakini wao wakaendelea kubaki vituoni, wakisubiri zoezi la kupiga kura lianze. Ghafla wakaja polisi wenye silaha ambao walitumia nguvu kuwatoa na kuwafunga pingu. Wakapelekwa kituoni bila kuwaeleza kosa lao. Uchaguzi ukamalizika na matokeo yakatangazwa wakiwa bado rumande.
Mwezi mmoja baadae wakapandishwa kizimbani kwa tuhuma za ubakaji na unyang'anyi wa kutumia silaha. Wakastaaajabu sana. Wakajiuliza wamembaka nani? Lini na wapi?
Hati ya mashtaka ikaeleza kuwa alfajiri ya 28 October 2020 walipoenda kituo cha kupiga kura, walimkuta msimamizi msaidizi wa uchaguzi, ambaye walimbaka kwa zamu, kisha wakampora pesa taslimu TZS 300,000/=. Baada ya kufanya tukio hilo wakabaki kama mawakala wa Chadema wakisubiri kusimamia kura.
Jambo la ajabu hati ya mashtaka haikumtaja huyo aliyebakwa wala hakuitwa mahakamani kutoa ushahidi. Aliwasilisha ushahidi wake kwa maandishi kwa kile kilichoelezwa kwamba ni kumlindia utu wake. Mahakama ya Hakimu Mkazi Bariadi ikawahukumu KIFUNGO CHA MAISHA JELA.
Baada ya kusota jela kwa miaka miwili, wakakata rufaa. Hatimaye leo Mahakama Kuu kanda ya Shinyanga imewaachia huru. Jaji Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Athuman Matuma amesema ushahidi uliowatia hatiani ulikuwa DHAIFU, UNAOTIA MASHAKA na USIOKUBALIKA KISHERIA.
Miaka miwili ya mateso, miaka miwili ya kupakaziwa kesi, miaka miwili ya kutumikia adhabu bila hatia. Kama si kukata rufaa vijana hawa wangemalizia maisha yao yote gerezani na kuacha familia zao zikiteseka. Na dunia nzima ingewahukumu kama majambazi na wabakaji [emoji24] maana mahakama ilishawa-label hivyo. Hivi ndivyo serikali ya awamu ya 5 ilivyosaidia kuimarisha Demokrasia nchini. Subhanallah.!