Vipi likitokea tetemeko la Ufa au Tsunami Dar? Ghorofa za mji zitahimili?

Vipi likitokea tetemeko la Ufa au Tsunami Dar? Ghorofa za mji zitahimili?

Wewe nyumbani kwako una hata first aid kit? au fire extinguisher? ukiendesha gari unafunga mkanda? wengi tunadharau mkanda japo tunajuwa mkanda unaweza kuokoa maisha yako ukipatwa na ajali, lakini kwanini watu wanadharau, sababu anadhani hawezi kupata ajali yeye dereva mzuri au haamini mkanda ila siku likimpata ndio atakumbuka muhimu wa mkanda au fire extinguisher. Kiuhalisia hakutakiwi jumba kuanguka labda livunjwe kusudi lakini kwetu yanatokea sasa tujiulize kwanini? Nyumba haitakiwi kuongezwa kitu ikishajengwa na kupitishwa shida kuu kwetu kuvunja vunja kuongeza vyumba sijui maduka hapo ndio shida. Unataka kubadilisha matumizi ya nyumba vunja yote jenga upya huwezi marufuku.
Hapa tunaongelea jambo la public wewe unaongelea jambo la mtu binafsi kufunga mkanda kwenye gari yake sasa kwani mimi nisipofunga mkanda kwenye gari yangu nikadhurika nitamlaumu mtu mwingine au unadhani nitailaumu serikali kwa kutofunga mkanda?Na ukija kwenye suala la miundombinu au ujenzi holela bado watu wa mipango miji hawafanyi kazi yao ipasavyo kama watu wanajenga bila mipango sasa hao watu wa mipango miji kazi yao ni nini?
Unachokitetea hata hakieleweki unazungukazunguka tu
 
Vifaa gani unaongelea hapa? wewe unalaumu kijumla jumla tu vifaa gani unaongelea. Tuache tabia za kulalamika tu. Sasa sema wewe ni jumba la ngapi kuanguka toka tupate uhuru? chukua majanga yote nchi angalia vitu hivi Potential + Frequency + likelyhood + financial loss utapata jibu unahitaji nini.
Hebu nipe mfano wa majanga yenye frequency kubwa na potential ambayo ndio yanafanyika kwa ufanisi mkubwa nchini kwetu?
 
Hebu nipe mfano wa majanga yenye frequency kubwa na potential ambayo ndio yanafanyika kwa ufanisi mkubwa nchini kwetu?
Nchi yetu tumebarikiwa hatuna majanga kama wenzetu ya vimbunga sijui tuko stable. Ajali za barabarani zinauwa sana nchi hii na huko barabara zinatanuliwa, Traffic police wako kila sehemu inapunguza kidogo iliyobaki na uzembe wa watu tu lakini sio tena barabara mbaya.
 
Majanga ya asili duniani yapo na yanaweza kutokea muda wowote. Kuna maeneo mfano Asia nchi kama za Japan, China, Indonesia, Uturuki, Iran n.k wao matetemeko ya ardhi ni sehemu ya maisha, nchi kama Marekani wao vimbunga ni sehemu ya maisha. Hizi nchi wanajipanga sana kupunguza madhara ya haya majanga muda wowote endapo yatatokea.

Sisi inawezekana hatuko kwenye ukanda wa majanga ya aina hii lakini haimaanishi kwamba hayatatokea kabisa. Sasa tujiulize endapo siku moja tetemeko hata la wastani tu litatokea Dar haya maghorofa ambayo watu wana mashaka na viwango vyake vya ujenzi, nondo hazielweki, yataweza kuhimili kweli hali hiyo? Hii miundombinu ya Kariakoo ambayo hata sehemu za wazi za kukusanyia watu 3,000 ni kama hakuna itaweza kuhimili? Hizi timu au tume za uokozi za kujivuta zina uwezo kupunguza maafa ya vifo??
Tunaweza kuendelea kufanya maombi na kusema "tusiombee hayo"
Elimu ni muhimu sana na mazoea ni hasara, hakuna tetemeko la ufa, halijawahi kutokea duniani na halitatokea kokote kule.
 
Kuna ujenzi wa foundations you take into account some small or certain level of earthquake.
Ila Kuna tetemeko kubwa no way out Ila hizi ndogo ndogo ujenzi wake upo na utalaamu wake mbona hata wabongo unafundishwa na Dr Nyaoro udsm CoET pale department ya Transportation and Geotechnical
 
Nchi yetu tumebarikiwa hatuna majanga kama wenzetu ya vimbunga sijui tuko stable. Ajali za barabarani zinauwa sana nchi hii na huko barabara zinatanuliwa, Traffic police wako kila sehemu inapunguza kidogo iliyobaki na uzembe wa watu tu lakini sio tena barabara mbaya.
Hujajibu swali,umezungukazunguka tu.
Ni majanga ya aina gani ambayo yakitokea uokozi wake huwa unafanyika kwa wakati na ufanisi mkubwa?Nchi kutokuwa na majanga mengi ya asili ni juhudi za Mungu
 
Hakuna neno linanikera kama kutaja awamu za viongozi kila wakati. Kwani angesema tunaishukuru serikali kwa kufanya ......... angepungukiwa na nini? Uchawa unapunguza kitu kwenye ubongo wa machawa.
Imekuwa too much kwa kweli hadi inaboa
 
Hujajibu swali,umezungukazunguka tu.
Ni majanga ya aina gani ambayo yakitokea uokozi wake huwa unafanyika kwa wakati na ufanisi mkubwa?Nchi kutokuwa na majanga mengi ya asili ni juhudi za Mungu
Hatuna natural dissaster nchi hii na kama kuwahi kutokea miaka 10 mara moja jibu fupi hatuna. Sema wewe majanga gani tunayo nchi hii.
 
Hujajibu swali,umezungukazunguka tu.
Ni majanga ya aina gani ambayo yakitokea uokozi wake huwa unafanyika kwa wakati na ufanisi mkubwa?Nchi kutokuwa na majanga mengi ya asili ni juhudi za Mungu
Sasa huna majanga ya asili unataka pesa zitolewe tununue nini?
 
Hujajibu swali,umezungukazunguka tu.
Ni majanga ya aina gani ambayo yakitokea uokozi wake huwa unafanyika kwa wakati na ufanisi mkubwa?Nchi kutokuwa na majanga mengi ya asili ni juhudi za Mungu
Wewe hapa kukosoa hujui kuna watu wako pale wanaokoa watu kwa kujitolea na maisha mengi yameokolewa. Watu jana walitaka vifaa vimekuja yamesimama tu sababu hakuhitajiki nguvu ni akili inatumika kutafuta njia za kuwatoa watu, oxygen wamepeleka watu wako juani wanapigania kutoa watu wewe uko hapa unapiga kelele vifaa kama USA, kodi tu hulipi unajuwa kulaumu tu. Shukuru wametoka watu wengi wazima 95% huoni mafanikio hayo mpaka sasa.
 
Majanga ya asili duniani yapo na yanaweza kutokea muda wowote. Kuna maeneo mfano Asia nchi kama za Japan, China, Indonesia, Uturuki, Iran n.k wao matetemeko ya ardhi ni sehemu ya maisha, nchi kama Marekani wao vimbunga ni sehemu ya maisha. Hizi nchi wanajipanga sana kupunguza madhara ya haya majanga muda wowote endapo yatatokea.

Sisi inawezekana hatuko kwenye ukanda wa majanga ya aina hii lakini haimaanishi kwamba hayatatokea kabisa. Sasa tujiulize endapo siku moja tetemeko hata la wastani tu litatokea Dar haya maghorofa ambayo watu wana mashaka na viwango vyake vya ujenzi, nondo hazielweki, yataweza kuhimili kweli hali hiyo? Hii miundombinu ya Kariakoo ambayo hata sehemu za wazi za kukusanyia watu 3,000 ni kama hakuna itaweza kuhimili? Hizi timu au tume za uokozi za kujivuta zina uwezo kupunguza maafa ya vifo??
Tunaweza kuendelea kufanya maombi na kusema "tusiombee hayo"
Tuzidi kumtumaini Mungu TU,hata tukisema tunaweza mda WA tatizo ukifika ndio utastaajabu ya Musa
 
boti na ngalawa plus lifebouy jackets
Sasa boti na ngalawa utawanunulia na watu wa Singida? life buouy Dodoma kila mkoa unachangamoto zake hatufanani sio kazi rahisi kama tunavyotaka kusema hili jambo ni pana sana kuliko uwezo wetu wa kipesa.
 
Hili ni tatizo kubwa linaloendekezwa na uongozi ambao sio makini.
Kabisa. Tuna uongozi unaoogopa kuwajibishana. Nadhani kuna aja yakupata katiba mpya ambayo itaruhusu nafasi nyingi za uongozi watu wawe wanaomba wenye sifa kuliko kupeana vyeo kama njugu kwa watu wasio na uwezo.
 
Kabisa. Tuna uongozi unaoogopa kuwajibishana. Nadhani kuna aja yakupata katiba mpya ambayo itaruhusu nafasi nyingi za uongozi watu wawe wanaomba wenye sifa kuliko kupeana vyeo kama njugu kwa watu wasio na uwezo.
Upo sahihi kabisa mkuu maana tulipo tuna hali mbaya na kama tutaendelea hivi hali itazidi kuwa mbaya zaidi.
 
Sasa boti na ngalawa utawanunulia na watu wa Singida? life buouy Dodoma kila mkoa unachangamoto zake hatufanani sio kazi rahisi kama tunavyotaka kusema hili jambo ni pana sana kuliko uwezo wetu wa kipesa.
singida na dodoma mafuriko watayasikia kwa wengine, wao kitisho kikubwa ni ukame utakaopelekea baa la njaa kama mvua ya kutosha haitanyesha. Labda na tetemeko la ardhi lenye kipimo kikubwa litokee kutokana na kupitiwa na bonde la ufa. Maafa mengine ni kama milipuko ya magonjwa
 
Back
Top Bottom