Vipi mtu asiyejua kusoma na kuandika, aliyeishi miaka 1400 iliyopita akajua haya?

Vipi mtu asiyejua kusoma na kuandika, aliyeishi miaka 1400 iliyopita akajua haya?

Toa ushahidi wako kimaandiko.
MAANDIKO YAPI?! Kama ya dini mimi sina coz siyo mfia DINI! Kuhusu Uislam na vatican now sina mdaa mpaka nitakapo pata likizo kazini! Coz wengi wAtakuw na maswali mengi kutokan na ufia dini!
 
Na kuandikwa kwenye Quran hakufanyi hizo dhana kuwa ukweli, mi silazimishi bali wewe na kitabu chako mnataka kulazimisha ili kuficha makosa yaliyomo kwenye hicho kitabu
Huyo Mtoa maada kasema kuna mwili wa pharaoh umeokotwa baharini na kuthibitisha ukweli wa Quran na ndio mimi nikamwambia huo ni uongo, hakuna Mwali wa pharaoh uliowahi okotwa baharini
Ili uwe na constructive urgument lazima uje na references na ushahidi wa ku support hoja yako. Pendekezo lako halina uzito. Na unakataa ushahidi wa pekee unaosadikika na mabilioni ya watu. Hivi unategemea watu wakisikie wewe???
 
Ili uwe na constructive urgument lazima uje na references na ushahidi wa ku support hoja yako. Pendekezo lako halina uzito. Na unakataa ushahidi wa pekee unaosadikika na mabilioni ya watu. Hivi unategemea watu wakisikie wewe???

Ninachokieleza hapa na kilichoelezwa humo kwenye kitabu kipi kina ushahidi?
 
Naona kwenye Quran kuna dhana na copying ya bitu vilivyokuwepo
Kaka umesema uongo wa kimatabaka.Naona wengi wanakizungumia kitabu cha Qur'an pasi na elimu.Bali wengi wanakizungumzia kwa chuki,na chuki ukungu katika ile njia ya kuitafuta haki.Kwa ufupi ngoja nikupe habari kwa uchache juu ya kitabu hichi kitufu.

QUR'AN ni :

1.Ni kitabu cha Mola mlezi,Mola ambaye yeye tu ndiye apasae kuabudiwa kwa haki.

2.Ni kitabu kinacho bainisha haki na batili.

3.Ni kitabu kinacho amrisha mema na kukataza mabaya.

4.Ni kitabu kinacho watoa waja kwenye giza na kuwapeleka kwenye nuru kwa idhini yake Mola muumba.

5.Si kitabu cha sayansi.Sayansi inafata Qur'an kamwe Qur'an haifati sayansi.

6.Ni maneno ya Allah aliyetukuka wala si kiumbe.

7.Ni kitabu kilichoteremshwa kwa muda wa miaka 23 kupitia malaika Jibril amani ya Allah iwe juu yake.

8.Ndani yake imeelezea visa vya nyumati za kale na mitume wao,kadhalika imeelezea ahdabu waliyopata waovu baada ya kuasi,imeelezea sheria,kumpwekesha Mola mlezi na makatazo juu ya kumshirikisha yeye.

9.Ni kitabu kilichobashiri mambo yajayo.

10.Ni kitabu ambacho kinajitafsiri kwa chenyewe na kinatafsiriwa kwa maneno ya mtume Muhammada sala na salaamu zimfikie.

11.Ni kitabu ambacho Mola mwenye nguvu amechukua ahadi juu ya kukilinda na kamwe hakitoingizwa uchafu na yeyote awaye kwani alishawapa changamoto wale wa mwanzo katika wapingaji kwa kuwaambia walete walau mfao wa aya moja kama wao wanasema ukweli,hakika hali wa shani walishindwa na hakuna atakaye weza.

12.Ipo katika vifua vya wanaume.Hakuna utakalo zua na kulibabatiza isipokuwa wanaume watakwambia hili si katika Qur'an.

13.Ni kitabu kilichoteremshwa kwa lugha ya kiarabu.

14.Ni kitabu kwacho kina elimu mahususi ya zinazoelezea jinsi ya kukisoma na jinsi ya kukitafsiri.

Mkamilifu ni Mola pekee,Mola ambaye amezisimamisha mbingu bila nguzo,Mola ambaye amefanya usiku kuwa wa kupumzika na mchana kwa ajili ya kutafuta,Mola ambaye kila kitu amekiweka mahala pake na makusudi na ukikuta makosa katika andiko langu hilo ni juu yangu na ni udhaifu wangu.
 
Qur'an ilikuwa imeandikwa kwenye ngozi,unajua jua lilivyo kuwa kali huko jangwani,na qur'an ilikuwa imeandikwa kwenye magome,baada ya kifo cha nabii muhammad s.a.w,maswahaba wakaona nibora kukusanya ngozi na magome na kuzitengenezea folder."wahyi" kutoka kwa muumba ukawa katika kitabu. qur'an kareem.
Kaka Qur'an haikuandikwa katika magome ya miti wala ngozi.Iliandikwa kwenye karatasi tena kwa maelekezo ya mtume Muhammad alayhi salaam baada ya kufariki rasul amani ya Allah iwe juu yake ndio maswahaba Allah awaridhie wakaikusanya sehemu moja na kuwa msahafu.Upangiliaji wa aya na sura ulikuwa unafata maelekezo kutoka kwa mtume wa Allah amani juu yake.Hii ni kwa sababu kwanza Qur'an ilikuwa inashuka kwa matukio na mtume amani iwe juu yake sababu alikuwa hajui kusoma wala kuandika,pale aya inapo teremka alikuwa ana muamuru mmoja kati ya waandishi waandike aya fulani sehemu fulani.Mathalani labda leo hii kutokana na tukio fulani Allah akamtuma malaika Jibril amani ya Allah iwe juu yake kumfikishia mtume amani iwe juu yake,basi mtume anamuita muandishi wake anamwambi aya hii nenda kaiandike pale ambapo aya fulani ilipo ishia.Kwa ufupi hivyo ndivyo Qur'an ilikuwa inaandikwa.

Kwa ufupi kwa wale wasiojua kuhusu Qur'an,ni kuwa Qur'an imeteremshwa kidogo kidogo kutokana na matukio na sababu husika wala haikuteremshwa kama kitabu kamili na Allah ndio anajua zaidi.
 
Back
Top Bottom