Vipindi vya dini katika shule za msingi na Sekondari za Serikali vifutwe

Vipindi vya dini katika shule za msingi na Sekondari za Serikali vifutwe

China, Japan, Korea, Vietnam, Sri Lanka, Thailand na nchi nyingi za Asia hazijawahi kuwa na habari na kitu kinaitwa Biblia au Quran ila zina sheria na wanaishi kama binadamu waliostaarabika kwa kiwango cha juu sana.
Satan agents kumbe mpo jf?
Mungu kwanza mengine baadae, hayo maarifa yanatoka kwa Mungu, sheria zote zimetoka kwenye Biblia tukaziboresha, mtito akikulia dini hawoi mwovu, acha upuuzi wako wa kumdharau Mungu wa Israel.
 
Mimi nafikiri vingefanyiwa maboresho zaidi kwa kuangalia sifa na ufanisi wa wakufunzi wa vipindi hivi.
Kwani kwa sehemu kubwa vimekuwa vikipoteza muda wa watoto kujifunza kutokana na kutotiliwa maanani katika mitaala.
Pengine vingetumika kama psychotherapy na maswala mengine yanayohusisha mental health wellness pamoja na imani vingekuwa na manufaa sana katika kuwajenga watoto kiakili na ukuaji.
 
Wale waliofanikiwa kupata elimu ya darasani angalau ya darasa la saba na kuendelea watakumbuka vipindi vya dini ambavyo vilitengwa rasmi kulingana na madhehebu mbalimbali na wanafunzi wote ni lazima kuhudhuria katika vipindi hivyo.

Mara nyingi vipindi hivi huwa Ijumaa kuanzia muda wa saa nne ili kuwapa fursa waislamu kwenda msikitini kwa sababu mara nyingi wao huwa hawatumii madarasa kuswali katika vipindi vya dini kama wenzao Wakristo.

Wakati mjadala wa tija elimu yetu ukiwa mkali bungeni na mtaani ipo haja ya kuliangazia pia jambo hili na kuona kama kuna tija yeyote kuwa na hivi vipindi.

Ukiangalia kwa makini utagundua vipindi hivi vya dini havina tija yoyote kwa wanafunzi zaidi ya kuwachukulia muda wao ambao ungweza kutumika katika mambo mengine muhimu kama sanaa za uchoraji, uchongaji, kuimba, kuogelea, ushonaji n.k

Ni wakati sasa mamlaka zinazohusika na elimu zitoe muongozo wa vipindi hivi kufutwa na kuongeza mambo mengine secular au kupunguza muda wa wanafunzi kukaa darasani.
Wale waliofanikiwa kupata elimu ya darasani angalau ya darasa la saba na kuendelea watakumbuka vipindi vya dini ambavyo vilitengwa rasmi kulingana na madhehebu mbalimbali na wanafunzi wote ni lazima kuhudhuria katika vipindi hivyo.

Mara nyingi vipindi hivi huwa Ijumaa kuanzia muda wa saa nne ili kuwapa fursa waislamu kwenda msikitini kwa sababu mara nyingi wao huwa hawatumii madarasa kuswali katika vipindi vya dini kama wenzao Wakristo.

Wakati mjadala wa tija elimu yetu ukiwa mkali bungeni na mtaani ipo haja ya kuliangazia pia jambo hili na kuona kama kuna tija yeyote kuwa na hivi vipindi.

Ukiangalia kwa makini utagundua vipindi hivi vya dini havina tija yoyote kwa wanafunzi zaidi ya kuwachukulia muda wao ambao ungweza kutumika katika mambo mengine muhimu kama sanaa za uchoraji, uchongaji, kuimba, kuogelea, ushonaji n.k

Ni wakati sasa mamlaka zinazohusika na elimu zitoe muongozo wa vipindi hivi kufutwa na kuongeza mambo mengine secular au kupunguza muda wa wanafunzi kukaa darasani.
Mimi vipindi vya dini vilinisaidia sana kuwa mwanafunzi mwenye tabia nzuri. Nilikuwa mkorofi shuleni, lakini Neno la Mungu (kupitia kwa walimu wa dini waliokuwa wanakuja kufundisha) lilinisaidia kubadilika na kuwa mwanafunzi mtulivu. Kizazi cha sasa ni cha dotcom. Usipowafundisha wanafunzi mambo ya dini watafundishwa na ulimwengu; wataokota mambo machafu kutoka kwenye mitandao then tutaendelea kulia lia kwamba siku hizi kuna mmomonyoko wa maadili.
 
Taifa au familia yoyote bila misingi ya dini (haijalishi Ni dini ipi)

Iyo familia itageuka familia ya hovyo Sana.
- Kuua
-kubaka
-wizi
-Chuki
-unafiki
-mapenz na Ndugu
-mapenz ya jinsia moja
-mapenz kinyume na maumbile
-mapenz na wanyama
-ukatili
- ulevi na madawA
-ushirikina
-umalaya na ukahaba
-Nidhamu mbovu
-uzalendo sifuri
-utii hamna

Ndo maana serikali
imeruhusu na inazilea taasisi za kidini (hazilipi Kodi) ili kuisaidia serkali kujenga mshikamano, Aman, utulivu na kutunza ustaarabu wa wananchi wake.



Sent using Jamii Forums mobile app
Umenena,iliyo kweli tupu.
 
Kwanini usi ishaur serikali ianzishe hayo masomo ya sanaa unayo yataka, kwan hujui dini ina msaada mkubwa kwa watoto bila dini cjui tu mambo yatakuaje.

umewaza vizuri lakini sio kwa kutumia akili
 
Baada ya kusoma huu Uzi,
Kuna Mambo kadhaa nimegundua kwa mtoa mada

1. Ana umri mdogo bila Shaka
(huenda Ni mwanafunzi bado)

2. Hana familia
(Hata Kama anayo Basi inalelewa na Ndugu,wakwe au wazazi wake)

3. Ana upeo mdogo Sana wa kufikiri.
(Haiwazii kabisa athari ya Jambo kabla ajalitekeleza, Anaendeshwa na mihemko)

4. Hana hofu ya Mungu kabisa







Sent using Jamii Forums mobile app
Kwani kuwa na vipindi vya dini ya kiislam au kikristo ndiyo hofu ya Mungu?
 
Hata wapagani ni raia kamili na wana haki zote katika hii nchi. Kuna shule zinalazimisha kwa viboko wanafunzi wote waende kwenye vipindi vya dini. Hii sio sahihi.
Sio kweli,hakuna mwanafunzi anayelazimishwa kwenda kwenye vipindi vya dini.
 
China, Japan, Korea, Vietnam, Sri Lanka, Thailand na nchi nyingi za Asia hazijawahi kuwa na habari na kitu kinaitwa Biblia au Quran ila zina sheria na wanaishi kama binadamu waliostaarabika kwa kiwango cha juu sana.
Aliyekudanganya,kakudanganya sana,hizo nchi,zina watu wengi wanaomini uwepo wa Mungu,kuliko nchi zote duniani.
 
Mimi vipindi vya dini vilinisaidia sana kuwa mwanafunzi mwenye tabia nzuri. Nilikuwa mkorofi shuleni, lakini Neno la Mungu (kupitia kwa walimu wa dini waliokuwa wanakuja kufundisha) lilinisaidia kubadilika na kuwa mwanafunzi mtulivu. Kizazi cha sasa ni cha dotcom. Usipowafundisha wanafunzi mambo ya dini watafundishwa na ulimwengu; wataokota mambo machafu kutoka kwenye mitandao then tutaendelea kulia lia kwamba siku hizi kuna mmomonyoko wa maadili.
Umesema kweli tupu.
 
Wale waliofanikiwa kupata elimu ya darasani angalau ya darasa la saba na kuendelea watakumbuka vipindi vya dini ambavyo vilitengwa rasmi kulingana na madhehebu mbalimbali na wanafunzi wote ni lazima kuhudhuria katika vipindi hivyo.

Mara nyingi vipindi hivi huwa Ijumaa kuanzia muda wa saa nne ili kuwapa fursa waislamu kwenda msikitini kwa sababu mara nyingi wao huwa hawatumii madarasa kuswali katika vipindi vya dini kama wenzao Wakristo.

Wakati mjadala wa tija elimu yetu ukiwa mkali bungeni na mtaani ipo haja ya kuliangazia pia jambo hili na kuona kama kuna tija yeyote kuwa na hivi vipindi.

Ukiangalia kwa makini utagundua vipindi hivi vya dini havina tija yoyote kwa wanafunzi zaidi ya kuwachukulia muda wao ambao ungweza kutumika katika mambo mengine muhimu kama sanaa za uchoraji, uchongaji, kuimba, kuogelea, ushonaji n.k

Ni wakati sasa mamlaka zinazohusika na elimu zitoe muongozo wa vipindi hivi kufutwa na kuongeza mambo mengine secular au kupunguza muda wa wanafunzi kukaa darasani.
Acha mzaha
 
Kuna faida nyingi za kulea watoto ktk misingi ya hofu ya Mungu kuliko kutofanya hvyo.
 
Misingi ya imani/dini wajengee nyumbani kwako, kanisani, msikitini au kwa waganga wa kienyeji. Hiyo haipaswi kuwa kazi ya serikali. Zaidi sana kuna shule za seminary na za mashirika ya dini, wafanye hiyo kazi.
Mimi nafikiri uende shule za watoto wako ukawaambie walimu kuwa wanangu ni wapagani kwahiyo msiwalazimishe kuingia vipindi vya dini kwasababu wewe baba yao huamini katika Mungu..na sio kutaka vijana/watoto wetu wapotee kwa kukosa misingi mema ya imani/dini..
 
Misingi ya imani/dini wajengee nyumbani kwako, kanisani, msikitini au kwa waganga wa kienyeji. Hiyo haipaswi kuwa kazi ya serikali. Zaidi sana kuna shule za seminary na za mashirika ya dini, wafanye hiyo kazi.
Kwani wewe unaumia wapi mkuu,.??naona jambo hili linataka likutoe machozi ya uchungu,..
 
Kuna wengine wengi walikuwa na tabia mbovu sana, tena wakiwa viongozi wa dini shuleni.
Shule inaendeshwa kwa sheria na taratibu kama mwanafunzi hazifuati kuna adhabu zake zimeainishwa, sio kazi ya vipindi vya dini kudumisha amani, utulivu na utaratibu shuleni.
Mimi vipindi vya dini vilinisaidia sana kuwa mwanafunzi mwenye tabia nzuri. Nilikuwa mkorofi shuleni, lakini Neno la Mungu (kupitia kwa walimu wa dini waliokuwa wanakuja kufundisha) lilinisaidia kubadilika na kuwa mwanafunzi mtulivu. Kizazi cha sasa ni cha dotcom. Usipowafundisha wanafunzi mambo ya dini watafundishwa na ulimwengu; wataokota mambo machafu kutoka kwenye mitandao then tutaendelea kulia lia kwamba siku hizi kuna mmomonyoko wa maadili.
 
Back
Top Bottom