Viroja: Siku ya kwanza kupanda ndege (ushamba mzigo)

tujitahid tupandishe watoto wetu ndege mapema jamani maana ni aibu kwa karne hii unakuta mtu kupanda basi tu anatapika je ndege akianda si ndo itakuwa hatari?
 
Ila jamani kiukweli nilichojifunza usije kupanda fastjet nawewe ukasema umepanda ndege. Halafu ukaenda kupanda ndege zenyewe za kimataifa na maconfidence yako uloyatoa fastjet ni utaumbuka!!!!!!

Yani zile ni ndege, halafu fastjet ni mabasi yanayosafiri angani. Wenzetu wana state of the art facilities ambazo huzikuti fastjet. My 1st experience from fastjet kwenda ndege nyingine niliumbuka sana..
 

Eehe uliumbukaje mkuu? Eleza kidogo basi!
 
mie nasafiri karibia kila siku na changamoto kubwa ninayoipata hadi asaiv ni kwamba nashtuka toka usingizini nipo kitandani chumbani kwangu.
 
Mkuu kuna ka story eti Mwalimu alienda na kawawa london kwenye mkutano wa jumuiya ya madola sasa ilivyofika muda wa kulala kila mtu akaenda kwenye chumba chake. Kawawa akaingia kwake akakuta room iko empty hamna kochi kitanda wala meza.

Wazee wetu wa zamani walikuwa hawataki shari mzee akatandika koti lake akauchapa usingizi kwenye sakafu. Asubuhi Mwalimu akaja kumpitia akashangaa mtu yupo chini room iko empty hakuna mabadiliko.

Ikabidi mwalimu amfundishe kumbe mambo yalikuwa ya ku switch tu kitanda hicho mara meza enhee makochi kawawa aliumia sana kwa ushamba wake
 
Cjui nitakuja panda hilo pipa.Ikitokea tu chance faster nitakuja kwenye huu uzi kisaka mzoefu nimpm kabla
 
tujitahid tupandishe watoto wetu ndege mapema jamani maana ni aibu kwa karne hii unakuta mtu kupanda basi tu anatapika je ndege akianda si ndo itakuwa hatari?


Kuna dalili nikafa kabla ya kupanda ndege ha ha
 


Unalaana www ha ha ha aha ha te te s
 
Binafsi mara ya kwanza ilikuwa mwaka huu na fast jet.. Thank yu fast

kiukweli namshukuru Mungu ktk process zote nilikiwa mwelewa.. Sikuwa mshamba... Nilifata taratibu zote.. Na nilienda mda wa kuripoti kama ulivyotajwa.. Maana ikiwa mara ya kwanza kiukweli inabd uache swaga uheshimu muda ili nxt time uwe unajua cha kufanya


shughuli mda wa kuruka ule jamani dahhh roho ilipaaaaaaaa paaaa nadhan hii inawatokea wengi

lakini baya zaidi huko angan nikawa na mawazo mengi sana nilikiwa siamini kama tunapaa angani mithili ya kunguru khaaa


kana kwamba haitoshi safari nzima nikawa nawaza dahhhh sasa pipa likifeli hapa likadondoka itakuwaje ahahahahhaahhaahahahahahah

nilijikuta nasali safari nzima.. Dahhhhh ndege bhana
 
Hahaaa hapana waliniambia ngoja tuwagaie wengine vikibaki watanipa naona walinipa jibu kistaarabu kwamba ni no


Te te te bila shaka msosi ulikuwa wa maana mpaka ukaomba round te lol
 
Daah Shikamoo fast jet wengi wetu tumeanza kupand hiyo tena kwa bei chee. hope itaendelea kuwepo hata baada ya uchaguzi wa 2015 maana nasikia prince amewekeza humo mbali na UDA
 
Cjui nitakuja panda hilo pipa.Ikitokea tu chance faster nitakuja kwenye huu uzi kisaka mzoefu nimpm kabla

Utakuja panda tu. nafahamu wengine hawajapanda kutokana na uhitaji mf. jamani kwenda nchi za mbali ndege haiepukiki, lakini kama una nia ya kupata experience wakati ndio huu. Book mapema Fast Jet nasikia bei zake si ghali kwani you never know wakati mwingine hizi arrangement zinaishiaga. Nakumbuka Eagle Air ilivyoanza mbona tulisema Byebye Mabasi dah tahamaki haipo tena!

Experience ya siku ya kwaza takuja tena siku nyingne ila nlifadhiliwa ndege ya KLM kwa kuwa ilikuwa kuna kutua Uholanzi faster nikaomba kubadilishiwa na kukata British Airways nikijua nikipanda hapa (DSM) kituo kinachofuata Heathrow , UK. Jamani tulipofika, kutokana na maelezo ni kuwa tutatoka nje ya uwanja wa ndegetutakuta mabasi mbalimbali basi tuchukue basi numbe x ( I cant recall thenumber) jamani tunatoka hivi tunaona bado tuko ndani kwani maana ya nje bongoni mpaka uone mawingu , mweee. Dah tukasema isiwe tabu tulikuwa wa3 wakati huotuna mipaund ya shulen si ndio mwanzo tena.

Tukachukua Cab yetu haooooHeathrow mpaka College! Tukatumiagharama sijui mara mia. Kuhusu ndani ya ndege next time.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…