Viroja: Siku ya kwanza kupanda ndege (ushamba mzigo)

Viroja: Siku ya kwanza kupanda ndege (ushamba mzigo)

sitasahau nilipopanda KLM hadi schipol/amsterdam uholanzi, nilikuwa naunganisha kwenda nchi nyingine ya ulaya. wiki hiyo kuna kijana gaidi wa nigeria alikamatwa anataka kulipua ndege ya delta ya wamarekani, hivyo mwafrica yeyote akionekana alikua akapekuliwa vilivyo.

huwezi amini, tulikuwa tumeongozana na wazungu wengi, lakini walipoona ngozi nyeusi tena inatoka africa, waliniweka pembeni wakaanza kukagua doc zangu zote polepole. they really humiliated me, askari mmoja akamwambie mwenzie "mwache uyo dogo hana tatizo", ndio nikaachiwa, lakini hata hivyo hawakuamini, mizigo yangu badala ya kupakiwa kwenye ndege yangu (kwasababu nilishachelewa ndege niliyotakiwa kuunganisha interval ya lisaa limoja) mizigo ilibaki, nilipata extension ya shirika lilelile la ndege bila malipo lakini kwa kupitia ufaransa na nikafika kwa kuchelewa masaa matano, ratiba yangu yote imevurugika.

nilipofika airport yangu yamwisho nilikuwa kuna kifurushi wameweka dawa za mswaki, tshirt ya shilika la ndege na kisuruari wakaniambia nitatumia kuvaa, ila niache address ya wapi nitakaa. drive from the airport hadi mtaa niliokuwa naenda kuishi ni nusu saa. nikaondoka. kesho yake, askari walileta mabegi yangu yote. kuangalia, kumbe waliyachelewesha ili wayakague.

HAPO NDIPO NILIPOONA UBAGUZI na ukatili wa wazungu. Mungu awasamehe......
Pole sana mkuu
 
Baada ya graduu yangu chuo.Tukarudi mkoa na maza. Fastjet ndo imeanza, mara yetu ya kwanza wote.
1. Mama anataka kukaa akakuta juu ya siti sehemu ya mizigo kuna mtu kashaweka wake. Akatia,"wee kondaa,we kondaa wéeh, hebu njoo kwanza"

2. Nikajaribu kwenda choóni japo sijabanwa alimradi tu nione pakoje

3 .Facebook page yangu iliomba poo. Mara checkin in at JKİ Airport. Mara nitupie picha alimradi kila mtu ajue.

4. Tulivyofika madreva tax wakaanza kututukana eti "hamna lolote nyie mtakuwa fastjet tu" hapo kisa ni baada ya wao wanatugombania sie hatuna time tunaenda kwenye daladala.

5. Jioni napokea simu toka kwa mjomba: "ah mjomba nimeamini ushamba mzigo wa mwiba".Nkamuuliza kwanini? Akasema,"leo sina raha. mama yako kutwa nzima anantambia kwenye simu kisa kapanda ndege"
Hahaha hii komesha eti we konda wee 😂😂😂😂
 
Back
Top Bottom