Viroja: Siku ya kwanza kupanda ndege (ushamba mzigo)

Viroja: Siku ya kwanza kupanda ndege (ushamba mzigo)

Siku ya kwanza kupanda ndege ilikuwa 2011, niliwahi kufika Airport nikielekea SA na Baadae Germany, Ushamba kitu kibaya sana niliachwa na ndege OR Tambo kwa kutokufuata maelekezo ya boarding gate, huwezi amini nililala Airport for one day before connecting to Frankfult

Dah.....humu ndan leo vicheko tu
 
Ukitaka kujua ushamba wa wanyakyusa tembelea Songwe international airport mbeya, yaani watu wanatembea yapata 10kms kuja kushangaa fastjet
 
Ulikuwa mzembe wa kusoma hukuiona reporting time.
+Ni kazi especially siku ya kwanza. Aidha wakati mwingine zinachanganya hata kwa mzoefu! Ndio maana kasema kishajifunza!
 
Ukitaka kujua ushamba wa wanyakyusa tembelea Songwe international airport mbeya, yaani watu wanatembea yapata 10kms kuja kushangaa fastjet
Jamani so nice safi sana watu wa Mbeya tena ina mandhari mazuri saaana. Nakumbuka tulivyokuwa wadogo tulikuwa tunaupara na kwenda stesheni, Dodoma.

Mpaka kwenye kichwa cha treni nikiwa na dada zangu, mdogo wangu, kaka yangu aliyekuwa kinara wetu alikuwa na guts mpaka anaongea na dereva wa Treni. No wonder sasa hivi ni Engineer Mahiri!
 
Ukitaka kujua ushamba wa wanyakyusa tembelea Songwe international airport mbeya, yaani watu wanatembea yapata 10kms kuja kushangaa fastjet

Ukome wewe, kichwa chako! Uwanja wa ndege hapa Mafiati umekuwepo miaka na miaka nani anaenda Songwe?
 
Niko Primary dadangu akapata safari ya uingereza.(Kipindi hicho tunasema ulaya v haijalishi hata kama umeenda Marekani). Hakuna yeyote alowah kusafir na ndege kwetu mpk muda huo achilia mbali kwenda nje ya nchi tu. Bana weh,
1.Alishonesha suti kwa fundi kama ya sarafina pale wakati movie inaisha.
2. Tulikodi tax tatu kumsindkiza airport.
3. Mzee alituma nauli kwa shangazi na bibi wiki moja kabla ili watoke Mbeya kuja kumsindikiza dada airport.
4. Pale airport tukajipanga warefu nyuma, wafupi wachuchumae, tukapga picha. Ni moja kati ya picha dada hazipendi sana leo akikumbuka tulivokuwa washamba.

sisi wanyiha hatuna ushamba huo
 
Mimi ilikuwa 2007 nilipata ride ya kwenda serengeti, nikapiga suti na scaf; kuingia kwenye ndege (hizi ndogo za watu 12) nakuta watu wamevaa simple sana kwa kuwa wanaenda bush; nilijisikia vibaya sana...

Dah..... Hiiii kali sna, nmecheka sna leo
 
Siku ya kwanza mimi kupanda ndege sikubabaishwa na mikanda,TV etc ila wakati ndege inapaa ilivyokuwa inatumia nguvu,inaunguruma halafu naona kama haipai in a struggle niliogopa sana! Lakini nikiwatazama abiria wengine wanaendelea na stories Kama kawaida hapo ndio roho kidogo ikatulia! Ila hadi kesho sijawahi kuipenda safari ya ndege if possible natumia usafiri mwingine!

Binafsi pia sijawahi zoea wala kupenda usafiri huu wa ndege, huwa napanda kama nina safari ya kikazi tu, otherwise kitu cha basi kama ni safari binafsi, taking off and landing huwa ni wakati mgumu sna maishani mwangu mana huwa nahisi kila kitu tumboni kinatoka.

Last month this year nlikuwa mtwara nkifanya juu chini mpaka wakati wa kurudi nikapanda basi mana nlikuwa kila nkiifikiria safari nakosa raha kabisa, tena ndo ukiwa kwa vindege vidgo lahaaa ndo balaa zaidi
 
kwikwikwi we utakuwa mpare tu next time mwambie akuandalie chapati unaziweka kwenye handbag

Mimi ilikuwa 1999,uelekeo nairobi, mke wangu akaniambia kwa uzoefu aliohadithiwa na babaake huko hewani mtu lazima usikie njaa sana,akaniandalia hotpot la makande, nasikitika sana maana lilibakia airport,kipindi hicho hakuna vifaa vizuri vya ku-detect madawa,kwa hiyo wakayafananisha na madawa!!! Ushamba gunia la misumari, unarekebisha mmoja, tisa inakuchoma!!!
 
Niko Primary dadangu akapata safari ya uingereza.(Kipindi hicho tunasema ulaya v haijalishi hata kama umeenda Marekani). Hakuna yeyote alowah kusafir na ndege kwetu mpk muda huo achilia mbali kwenda nje ya nchi tu. Bana weh,
1.Alishonesha suti kwa fundi kama ya sarafina pale wakati movie inaisha.
2. Tulikodi tax tatu kumsindkiza airport.
3. Mzee alituma nauli kwa shangazi na bibi wiki moja kabla ili watoke Mbeya kuja kumsindikiza dada airport.
4. Pale airport tukajipanga warefu nyuma, wafupi wachuchumae, tukapga picha. Ni moja kati ya picha dada hazipendi sana leo akikumbuka tulivokuwa washamba.

Hii rekodi yenu haijapatapo kuvunjwa, nyie ni masupa staa wa airport.
 
Ilikuwa 2012 ndo kwa mara ya kwanza napanda ndege niko kwenye FASTJET ya kutoka MWANZA kuja DAR, nilikuwa na mihemuko balaa, niliiwazia hii safari kwa muda wa wk 2, nakumbuka nilipiga picha kila sehemu nilipopata Aiport, nje ya ndege na ndani ya ndege mpaka leo zipo nimezihifadhi kwa ajili ya wanangu, wajukuu na vitukuu.

Photo-2433.jpg


Kali zaidi tulipokuwa hewani ndani ya NDEGE nikamwita mhudumu nimwulize wapi TOILET, akanionyesha, nikaenda japo sikuwa na haja yoyote nikaishia kutema mate kwenye sink la chooni , kuflash, nikanawa mikono, nikasukutua mdomo na kutoka zangu.

Photo-2440.jpg


Tulipotua pale JKNIA asubuhi saa 09:40 akili ndo ikazidi kupagawa baada ya kuyaona yale MADEGE mengine makubwa makubwa yanapaa na kutua, nikaashangaa kama dakika 15 hivi na kutoka zangu nje, pale nje sasa madereva TAX full kushupalia, wapi kaka, twende na hii, bei poa tu, kwenda kuuliza bei toka pale mpaka TEGETA sh ngapi eti naambiwa elfu 35, nikajisemea moyoni shwaiiiiinnn sana, wakati nimetoka Mwanza mpaka Dar nauli elfu 32 tena kwa NDEGE halafu kutoka hapa mpaka TEGETA elfu 35, nikaachana nao na kwenda kupanda zangu daladala kwa nauli ya sh 950 ila nyumbani niliingia 13hr shauri ya foleni.
Photo-2439.jpg
 
ungekuwa kikojozi ungekoma ubishi

mwaka 1999..haaikuwa mara yangu ya kwanza infact, nilienda kuiwakilisha Tanzania kwenye Bunge la watoto(The World Parliament of Children-Paris), sasa ile program ilinifanya nichoke sana manake sikuwa na muda mzuri wa kupumzika mara zote tulikuwa tupo busy sana!! Sasa siku ya kurudi tumepanda Swiss Air mpaka Zurich- wakati tunasubiri connection aisee nilipiga usiingizi wa kufa mtu pale,hadi muda wa ndege umefika mi nimelala tu..wale wenzangu (wawili)wakawa wameshapanda ndege mi nakoroma pale kwenye kochi...sielewi ilikuwaje manake ndege yote bado mm tu kupanda na air hostess wameshaambiwa kwamba kuna mtu mmoja amemiss

Ikabidi ndege isiondoke wakatumwa askari wa airport kunitafuta mule ndani...nikaja kuamshwa nio na lepe la usingizi wakaniambia ndege inakusubiria...wakanipeleka hadi boarding ile naingia tu mlango ukafungwa na kila mdada ananishangaa ulikuwa wapi...!!
Kikubwa mpaka leo sijajua ile ndege kweli ikinisubiri mimi au muda wake wa kuruka ulikuwa bado haujafika.
 
Wanyakyusa watani zangu kwa ushamba mnaongoza nchi hii no wonder joti hafiki kwa mzee mwalubandu huenda huyo mzee kaenda kushangaa ndege airport
 
Wanyakyusa watani zangu kwa ushamba mnaongoza nchi hii no wonder joti hafiki kwa mzee mwalubandu huenda huyo mzee kaenda kushangaa ndege airport. Badilikeni nyie kina mwakifulefule
 
Niko Primary dadangu akapata safari ya uingereza.(Kipindi hicho tunasema ulaya v haijalishi hata kama umeenda Marekani). Hakuna yeyote alowah kusafir na ndege kwetu mpk muda huo achilia mbali kwenda nje ya nchi tu. Bana weh,
1.Alishonesha suti kwa fundi kama ya sarafina pale wakati movie inaisha.
2. Tulikodi tax tatu kumsindkiza airport.
3. Mzee alituma nauli kwa shangazi na bibi wiki moja kabla ili watoke Mbeya kuja kumsindikiza dada airport.
4. Pale airport tukajipanga warefu nyuma, wafupi wachuchumae, tukapga picha. Ni moja kati ya picha dada hazipendi sana leo akikumbuka tulivokuwa washamba.

mkuu umenichekesha sana hasa hii namba nne na namba tatu kwi kwi kwi kwi kwi
 
Back
Top Bottom