Kwani wanaruhusu kufungua madirisha na kupiga kishokaMie mara ya kwanza kupanda ndege nilitoka Dsm kwenda Mwanza. Process nzima hadi niingie kwenye ndege ilikuwa 'shughuli'. Nilikaa upande wa dirishani, tulipopita Ngorongoro crater eti sikuthubutu kuchungulia nje. Kisa? Niliogopa eti nikichungulia naegemea upande mmoja hivyo nikaona kama vile ndege italalia upande ule na kuanguka! Ama kweli ushamba ni kazi!
Mkuu kwa fastjet mbea dar bei gan na mm nitoe washShukrani kwa fastjet, Mbeya - Dar, mwe!!
Robo ya mwaka imeisha una $200! Ulaya utaisikia! Halafu ukitaka kuichukia Ulaya kama unaenda mara ya kwanza nenda December,utajuta.Mpaka sasa nina 200 USD ili DECEMBER na mimi nikwee pipa lolote la ULAYA (Swiss Air au KLM)
Ndege imejaa uswahili hio balaa!Na mnyama emerates wa saa tano usiku hayupo tena
Mimi nilihakikisha napanda ndege zote za mashirika ya Ulaya. First trip Dar-London nilipanda KLM kwa kweli nili-enjoy sana Amsterdam kwasababu connection yangu ilikuwa kama masaa sita baadae.Mi pia kwa sasa nataka nipande SwissAir hata kama sio kwenda Afrika japo tu nitoke nilipo kwenda nchi nyingine ila ndani ya Europe nipaone tu na hapo Zurich maana hawa jamaa nauli zao mhhh ni juu sana ukilinganisha na KLM
Katika hiyo orodha hapo juu [emoji115] [emoji115] mi nahitaji Swiss tu..... Na naimani kama sio mwaka huu basi next mwakaMimi nilihakikisha napanda ndege zote za mashirika ya Ulaya. First trip Dar-London nilipanda KLM kwa kweli nili-enjoy sana Amsterdam kwasababu connection yangu ilikuwa kama masaa sita baadae. Then nikapanda British Airways wala siku-enjoy kwasababu unatoka London mara asubuhi unakutana na mabati yana kutu! Baadae nikapnda Swiss, aisee ile airport ya zurich ndio ilikuwa mpya,Loungee inaface runway bonge la view, then kubadili terminal moja kwenda nyingine unapanda vitreni havina dereva unabonyeza tu kinaondoka mpaka kwenye terminal yako chini kwa chini,ila shughuli nilivyopanda emirates, from London mpaka Dubai ndege kubwa nzuri mpya,kasheshe from Dubai Dar, ndege imechoka, imejaa waswahili ni kelele kama basi la mbagala,yaani pale pale dubai unajihisi tayari uko kariakoo! sasa hivi nachanga nipande ile A380
Kitu kilichonitoa ushamba ni Moving Walkway bado kidogo nidondoke Amsterdam mwaka 2000
Nakumbuka ilikuwa Mwaka 2008 mwezi Juni nilikuwa naenda kikazi Lusaka, Zambia basi sijui hili wala lile kwenye tiketi iliandikwa saa ya ndege kuondoka mimi nikajipa kama dakika 20 hivi ndo niwe Airport duuh ile kufika nikaambiwa muda umeisha daah! Nilichoka. But taratibu nikajifunza muda wa kufika airport, vitu visivyoruhusiwa kubeba kwenye ndege.
**NEW DEVELOPMENT
Mwezi Juni 2015 nilipata safari ya kwenda CAMEROON (kwa hisani ya Watu wamarekani USAID) sasa tukiwa huko tukalipwa posho kwa hela ya huko Central African Franc sasa nikazibana nije kubadilishia Bongo nafika bongo Bureau De Change zote hawabadilishi hizi pesa yaani nmepagawa sijui nikazitupe Coco maana....
HAKIKA USHAMBA MZIGO!
hahaha hii komenti sijui kwa nini haiishi utamu, sio kwa suti ya sarafina aisee...Niko Primary dadangu akapata safari ya uingereza.(Kipindi hicho tunasema ulaya v haijalishi hata kama umeenda Marekani). Hakuna yeyote alowah kusafir na ndege kwetu mpk muda huo achilia mbali kwenda nje ya nchi tu. Bana weh,
1.Alishonesha suti kwa fundi kama ya sarafina pale wakati movie inaisha.
2. Tulikodi tax tatu kumsindkiza airport.
3. Mzee alituma nauli kwa shangazi na bibi wiki moja kabla ili watoke Mbeya kuja kumsindikiza dada airport.
4. Pale airport tukajipanga warefu nyuma, wafupi wachuchumae, tukapga picha. Ni moja kati ya picha dada hazipendi sana leo akikumbuka tulivokuwa washamba.
Wenzetu mnafaudu....[emoji12]Katika hiyo orodha hapo juu [emoji115] [emoji115] mi nahitaji Swiss tu..... Na naimani kama sio mwaka huu basi next mwaka
Sifa sifa sifa!Mimi sikumbuki vizuri,ila nina zaidi ya masaa laki moja hewani
Ulimuomba mchezo?Mimi nakumbuka ilikuwa mwaka 2012 nilipopanda Qatar Airways wakati naelekea chuo nje ya Tz.
Kwavile ndio ilikuwa mara ya kwanza sikutaka hata mbwembwe nyingi,nilikuwa nacopy na kupaste jinsi alivyokuwa anafanya mdada flani wa kifaransa pembeni yangu.
Safari ilikuwa nzuri tu.
Hapana aisee. Lugha ilikuwa gongana siku hiyo,kingereza na kifaransa.Ulimuomba mchezo?