Viroja: Siku ya kwanza kupanda ndege (ushamba mzigo)

Viroja: Siku ya kwanza kupanda ndege (ushamba mzigo)

Sijui kwanini nilichukulia kawaida saana

Same wit me, nliona kawaida tu ingawa ki ukweli nlikua na mchecheto sanaa nlijitahidi kuificha. Kuna ushamba mwingine wakijinga sanaa...kuna ndugu yangu flan alipata a trip to malaysia na organisation flan for like 4 days..

Bas nakwambia aliaga ukoo mzima that anaenda Malaysia....unajua unakuta watu hawajawahi panda pipa before but alivyokua anajitapa tapa alikua anaonekana mseng* sanaa. He was like 25 of age. Ukimkumbusha leo mnaweza mkagombana.
 
kazi zaidi ipo kwenye ukaguzi watu kibao huacha mi-poafyumu, dawa za mswaki pale na wale wakaguzi hawakuelekezi uweke kwenye begi kubwa (la kucheck-in) wao wanafurahi maana baadae wanagawana. USHAMBA GUNIA LA KONO KONO
 
Ulikuwa ukitegemea kusindikiza hadi ndani ya ndege ndio uendelee kutoa maagizo ya kule aendako
 
kwa mara ya kwanza nilipanda mwaka 2012 south africa airways...basi kikafika south sasa natakiwa kubadilisha ndege kwenda zimbabwe..duuu sisahau ilikuwa ni muda mfupi sana wa kubadilisha ndege na mm ni mshamba mpaka napata ndege ya zimb jasho limenitoka balaa mana ile airport ya south africa ni kubwa balaaa...ila thanks kwa sasa nimezoea
 
Duh nimepanda juzi wakuu nimetoka dar kuja mwanza asee pale inapaa nilidata na ile kuyumba yumba kwenye mawingu na hali ya hewa juu haikuwa poa nusura ushuzi utoke ila nashkuru mungu tulifika salama japo sikuwa na uoga sana nilijifnya mjuzi kwenye baadhi ya mambo kama kufungua meza na kwenda chooni...ila fast jet huu utaratibu wakuuza vicoca cola elf 3 sio ishu me nilijua tunapewa bure hahahah dah niliinjoy nangoja return kurudi dar asee
 
ndege aisee ina utamu wake hasa kwa majirani yaani wk kabla ya kuondoka lazima ujisemeshe stori za kusafiri na ndege ili uonekane bab kubwa
 
Ingia www.fastjet.com halafu nenda kwenye plan your trip ama book a flight. Hapo utaje tarehe mbali mbali na kuangalia bei manake zinatofautiana. Usisahau kucklick return ili upate ya kwenda na kurudi. Ukikata ticket mapema kama wiki 2 ama 3 kabla nauli inakuwa chini sana
Jambo sana ndugu zangu.Kuna mtu anae jua gharama za kusafiri kwa fast jet from Dar to mwanza.Msaada please, hasanten
 
Huu uzi ni darasa tosha ila wakuu naombeni msaada kucheck-in online kwa fastjet unafanyeje?
 
Sina tofauti na Dennis Bergkamp yule legendary wa Arsenal naogopa kusafiri na ndege hadi basi.. . nilishautoa akilini huo usafiri. ..sijui naogopa nn
 
Mara ya kwanza kupanda ndege dk 2 kabla nilikula ugoro ili nisiskie chochote kinachoendelea! ilikuwa kutoka dar kwenda kenya
 
Sijawahi panda ndege ndo natarajia kupanda kwa mara ya kwanza, Je! Ni vitu gani vya msingi kuzingatia ni muhimu kweli kufika masaa mawili kabla?
 
HAHAHAHAAA
Mimi day one ilikua natoka kilimanjaro kwenda Mwanza na Precision air,sasa ninejipanga kabia mabegi yangu maana before safari nlishapewa miongozo na waru mbalimbali.

Nafika KIA nabanana na watu wanaongojasame ndege from nairobi,Nilikaa na mwarabu mmoja ye ndo kwanza kavaa simple chini ana ndala na mabuti kabeba kwenye mfuko wa rambo nkaduwaa mmhh huyu na rambo ndani ya ndege zinaruhusiwa??

Nawaza atarudishwa tu uyu kumbe mi ndo ushamba umenilemea kule ndani kama kwenye bus tu hamna kipya
Kingine ule uoga wangu nilisoma magazeti yote yaliyokuwa apo kwenye siti ya mbele yangu

HAHAHAHAA nasahau niliogopa kunywa chochote coz nmewaza kale ka glass kanaweza kakatikisika nikajimwagia soda bure, nlikuwa nawaza ndege inatikisika muda wote
 
Mama yangu alikuwa hajawahi panda ndege hata mara moja so akapanga mi na mwanangu(akiwa na miezi 6)tumsindikize nairobi asafishe macho

Eeh bwana eeh ndege ilikuwa ya saa nne asubuhi lakini alinichukua kwangu saa kumi na moja asubuhi..huko njiani sasa kuelekea airport ni shida..eti tutachelewa ndege bureee

Ile tumepanda ndege tu,mwanangu akalala fofofo halafu tukatangaziwa kwamba kuna mvua huko tuendako so hali ya hewa si nzuri..sasa vile ndege inavyokuwa kama inapita kwenye makorongo,nilitamani nihame seat.mama alisali sala zote anazozijua mpaka toba eti tunakufa

Halafu mdogo wangu anasomea hayo mambo ya aviation,mama akasema kama mambo yenyewe ndo haya nampiga marufuku dogo kuendelea na hyo kozi "..eeh yesu eeh tusife leo baba ila sipandi ndege tenaa...".sahv kashasahau anataka safari ya mbali zaidi nimemwambia atafute escort mwingine mi siendi nae

Uwiii mbavu zangu mie..
 
Yakwangu sio mara ya kwanza ila ni kioja balaa,ni mwaka 1997 December 22 kutoka Dar kwenda Amsterdam na KLM. Miezi hiyo kwa kawaida Dar ni joto sana so nilivaa kaptura ya jeans na Tshirt na nikisafiri sipendi kubeba mizigo ya mikononi kwani ni msahaulifu,hivyo mizigo yangu yote niliipitisha ipimwe ili nisibaki na kitu mkononi.Safari ilikuwa nzuri mpaka tunafika,sasa karibu tunatua Amsterdam rubani anatutangazia hali ya hewa nasikia outside at ground level is -5 C,sikuwaza wala kushtuka sana coz kwa wakti huo ndani ya ndege ilkuwa pako poa sana.Ile tumefika wenzangu wote wanafungua mikoba yao na kutupia makoti marefu even air hostess mimi nabung'aa macho tu,tukashuka kwenye ndege kwenda ndani ya basi ili tuende terminal watu wote wananishangaa,nikaanza kuwa mweupe ule wa unga,mpaka tunafika lounge,mdomo hauwezi funguka.Bahati nzuri wenyeji wangu kama walihisi manake waliomba ruhusa nikaletewa koti refu la sufi,gloves na Kofia mzula.Nilikuwa kama mfu nusu kuongea siwezi,vidole vya mikono vimekakamaa balaa mabegi nayaona yanapita ila siwezi kuyachukua,pale Amsterdam kuna sehemu wenyeji wanawaona arrival kwenye kioo,so waliniona the way nilivyoganda wakaomba waingie kunisaidia mizigo.Mpaka naingia kwenye gari siwezi kuongea,hadi tunafika nyumbani heating system ilisaidia baada ya masaa mawili ndo niliweza kunyanyua mdomo.
Siwezi kusahau kioja hiki kwani wakati natoka Dar nilikuwa "Bontown" ila kule nilikuwa zoba (kila mjanja ana mjanja wake)

Aiseee nimecheka mpaka mbavu zinaniuma sasa
 
Back
Top Bottom