Viroja: Siku ya kwanza kupanda ndege (ushamba mzigo)

Viroja: Siku ya kwanza kupanda ndege (ushamba mzigo)

Duuuu ntakuja kutoa ushuhuda nikishapanda around this year[emoji1][emoji1][emoji1][emoji1][emoji1]
 
Mimi ilikuwa 2007 nilipata ride ya kwenda serengeti, nikapiga suti na scaf; kuingia kwenye ndege (hizi ndogo za watu 12) nakuta watu wamevaa simple sana kwa kuwa wanaenda bush; nilijisikia vibaya sana...
Hahahahahaha

Sent from my HUAWEI Y300-0100 using JamiiForums mobile app
 
Mara ya kwanza kusafiri nilikuwa naenda Sehemu hivi kupitia Paris. Ila siku hiyo ndege ya Air France ikawa imeharibika na hivyo ikaja ndege ya Madagascar Airlines Boeng 747, mzinga wa pipa.

Uzuri ni kuwa nilipigwa shule nyumbani nzuri sana jinsi ya kufunga mkanda, kulaza kiti na kukirudisha, kufungua headphones na kuzitumia na wapi zipo tundu za kuchomeka.

Ila nakaa, pembeni kuna Dada wa Kiganda na Mudhungu wake, akawa anahangaika jinsi ya kufunga mkanda, bwana wake akamsaidia kufunga. Sijui siku hizi anajisikiaje akikumbuka ushamba huo wa siku ya kwanza.

Kasheshe ilikuwa wakati wa kula. Ila Mungu bariki nilishaambiwa kuwa kuna vikaratasi vya kufuta uso na asubuhi mnaletewa taulo za motomoto kufuta uso pia. Msosi kufika, maajabu matupu kwani nusu ya vyakula navifahamu na nusu sivifahamu. Mie na kundi langu lote tukawa tumekubaliana tutakula kila kitu na hatubakizi hata kama watakuwa CHURA wa Kifaransa maana hawa jamaa WALA VYURA hawakawii kumlisha mtu nyama zao.
Kila kitu kilienda safi ila ikawa kasheshe kuzila OLIVE ila nikajikaza nikazila. Kulikuwa na nyama nyeusi nyeusi, sikujali ni nini, nikazila bila huruma. Mwisho vikabaki vipaketi vitatu. Kimoja kukifungua ni Sukari, nikaibugia. Kingine kufungua ni jibini, nikaila bila huruma. Cha mwisho kufungua (nilikuwa nafahamu unafungua kwa kuvunja ncha iliyochomoza) ikawa kumbe maziwa ya kwenye kahawa ambayo nilishaimaliza mapema sana bila sukari wala maziwa. Basi nikaangalia kushoto kulia hakuna anayeangalia, nikabugia. Mwisho nikasema hata kama Mjinga fulani kaniona, sijali maana hatakuja kuniona tena. Mwisho sahani yote ikawa tupu na wakaja akina dada kuchukua makasha matupu.

Kuna jamaa alikuwa anawasumbua akina dada kuagiza pombe basi ilipofika saa 9 usiku, wakamuita na kumuonyesha Friji la Pombe lilipo na wakaenda kulala. Jamaa alipofika Paris, alikuwa anatambaa kutoka ndani ya ndege.
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Mimi sikumbuki vizuri,ila nina zaidi ya masaa laki moja hewani
Hahahah hata ile Tanker inayojaza mafuta ya Stealth bomber sijui kama zimefikisha masaa laki moja hewani

Au wewe ni Jakaya?

Wewe ni kiboko
 
Duh mm nlikuwa natoka mwanza kuja dar. Na nlikuwa na familia yangu yote tulikuwa tunakuja likizo. I was very happy ila ndege ikiwa juu ndo nikajiuliza why if ndege iki crash maana tye whole of my family is gone na nitafutika ktk uso wa duia without leaving a mark kwamba huyu mtu alikuwepo. Baadae nikazoea tu. Ila nikasafiri international. Serioua it was stressfully nlichange ndege mara tatu sasa maudhi ni kutafuta mageti ya kwenda kuboard

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nilikuwa nakwenda TURKY na jamaa yng mmoja hivi..MIMI NDY FIRST TIME KUPANDA MWEWE...ila Yeye ni Mzoefu.....basi muda wa chakula Ukafika nikala kumaliza jamaa AKANAMBIYA inabidi NIMPE DOLA 30 US akalipie CHAKULA nilichokula...Jamaa alitoka kwa MUDA NA ILE PESA muda KIDOGO akarudi...na mimi niliamini SABABU WATU WENGINE NAO WALIKUWA WAKIAMKA MARA WANARUDI..KUMBE WANAKWENDA CHOONI..MIMI SIJUWI....YEYE ALINIDANGANYA NDY WANAKWENDA... KULIPA VILE........BALAA lilianza BAADA YA KUMWITA muhudumu ANIONGEZE KINGINE......akanambiya mbona ni BURE TU?jamaa ilibidi ateme KIBUNDA CHANGU CHOTE ..na HATUKUONGEA hadi Tunafika....INSTANBUL...lakini nilijiona MJINGA SN kulipishwa Chakula WAKATI NI BURE KABISA...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom