0_0
Unafahamu kazi ya sayansi? Mtu anayepata taarifa kutoka kwenye mamlaka fulani kwamba kuna jambo fulani huenda likatokea, anachukua tahadhari. Nafahamu vyema Labda nikuulize wewe, unafahamu maana ya prediction based on percentage?
Kwa ujumla, Urastafari hupinga mifumo japo mapokeo ya namna hii ama ile kiroho—mambo kama yale ya ‘jamii za kikuhani’ na ‘ibada’ ni yenye asili ya jamii za Kiafrika na pia ‘Mashariki ya kati’ yaani Uyuda—na Uhindu vilevile. Nyumba ya Nyahbinghi kwa mfano, ina asili ya ‘ngoma za maruhani’ za kimakabila ya Afrika, ambavyo vilevile mna desturi ya kuambatana na matumizi ya ‘mimea’ ama ‘pombe’ kwa ‘matambiko’. Urastafari, kupitia muingiliano wake na mapokeo kutokea kwa jamii ya Kihindu kule karibia ndilo limeleta ‘sakramenti’ ya matumizi ya ‘Ganja’ katika jamii inayoshiriki wakati wa miditisha ya kikundi cha watu wanaokaa pamoja. Kwa hivyo mahala pa ‘tambiko’ katika urasta huwa si tena jambo la ‘kupunga maruhani’ bali kutafuta ‘utulivu’ na amani ya JAH Rastafari kupitia sakramenti ya ‘Ganja’ na kushiriki furaha kwa wandugu katika Rastafari.
Kwa jicho la Uono na Ufikirifu Mifumo, jamii ya Kihindu huwa na ‘zikri’ ya kusema JAI JAI pale Mhindu anapoonja na kulifurahia lenye kumpa faraja moyoni. Haya hufahamika kuwa ni matendo ya ‘utakaso’ kupitia nidhamu ya ‘kukumbuka’--kumkumbuka ‘Mungu’ katika kila jema unaloliishi—Yoga Bhakti. Hili ndilo linachangia JAH JAH kuwa sehemu ya urithi wa mapokeo ya Kiyuda na hapo hapo Uhindu. Na ndivyo hivi, mlima Sayuni, kwa wahindu ungalitajwa ni >
‘Mlima Meru’<; Zaburi ya Daudi kwa Mhindu ingalikuwa si jingine bali muktadha wa Bhakti Yoga-->
JAI OM NAMA SHIVAYA<. Kutokuchana nywele na uvijitari pia vinaasili ya ‘maisha ya upweke’ na kujitenga ya mtu wa kutafuta ‘Utakaso’ isivyo kufuatisha mazoea na mkumbo wa jamii pana-->
Sannyasi<.
Kwa mtu-Rasta, ‘Dreadlocks—Misokoto ya asili ya Nywele’ ni alama ya ‘upekee’ wake, kujinasibu na uzuri wa asili, na imani yake kwa muambata wa mambo mengine yote, kuitwa ni ‘I-tal Livity’-- muungano na neno ‘Vital’--’uhai pumzi’ na ‘Livity’--’Uisho’. Iwe ni mazingira ya mjini ama shamba, utambulisho wa mtu-Rasta ni maisha rahisi katika kilimo ama kazi huku akiishi nadhiri yake ya Pendo Moja, Amani na Utangamano kati ,yake na dunia na walimwengu.
Sasa tunawezaje kuyashahibisha na dhana nzima ya Utaifa, tuseme labda taifa la Tanzania?
Kiuono na ufikirifu mifumo, ujenzi wa taifa lolote huhitaji ‘nguzo ya imani’. Hili ndilo linalobayanisha ukomo wa ELIMU 1.0 katika jitihada na harakati la ‘kujenga Taifa’. Maarifa ya mambo yakikosa na mzizi wa ‘metafizia na ontolojia’ huishia kutuletea >
‘ism’ na ‘schism’<, vile kwenye Urastafari husemwa -- Bob Marley kupata kuimba katika wimbo >
‘Get Up, Stand Up’<; vile huja kuwa kutokana na maarifa yanayowatenganisha watu kutokana na makambi ya mafikara na mlengo wa vitendo katika kuwatazama watu na kuwakadirisha hivi ama vile--kwa labda jinsia, umri, rangi ya ngozi, ni wapi anatoka n.k
Fikra na mawazo kuhusu jambo si ukweli wa mambo hasa—haijalishi watu wenye kushiriki fikra hizo ni wengi ama kidogo… Kufuatishwa kwa wazo ama fikara na watu wengi hukufanyi jambo linaloshikiliwa kusadikiwa na wao kuwa ni sahihi ama kweli. Katika dunia ya leo, Elimu 1.0 inatumika hata >
‘kuwajaza watu mafundisho’< ama hata ‘propaganda’ pasipo na watu kuhoji mapokeo yao ikiwa ‘yana vina vya tafsiri’ isiyo na chembe ya shaka ama vipi. Falsafa ya elimu ya leo mashuleni si lolote bali ‘ufikirifu’ wa juu juu wa mambo usio na ‘msaada’ katika ‘kuwaunganisha watu’ kweli kweli.
Shule zote za leo duniani, katika mikondo rasmi ya mifumo ni ‘nyumba za vifungo’--vifungo vya namna zote za ustaarabu wa kileo ambao nao pia ni ‘Kifungo cha Mfumo Babiloni’. Mtu anahitaji kujikwamua na fikra na mawazo yote ya ‘kufikia’ katika jamii yake, ambavyo ni liberiti’ katika mtu. Uhuru wa kwanza wa mtu upo kwenye kuondoa ujinga, huu unaweza kumpatia mtu ELIMU 1.0 lakini uhuru wa pili ni liberiti—huu huja na huku kwa mtu kujinasibu na Elimu 2.0. Kwa kuwa Elimu 1.0 bado humtengenezea mtu ‘Utumwa wa Kiakili’; jambo ambalo Bob Marley aliliimba katika wimbo >
‘Redemption Song—Wimbo wa Ukombozi’<…
‘Elimu 2.0: Uono na Ufikirifu Mifumo’ ndicho kile kinachokadirisha jambo la kusema ‘Hekima ni Uhuru’, kwetu Tanzania, kutaasishwa kupitia Chuo Kikuu cha Kwanza cha Dar es Salaam kwa kauli mbiu hiyo… Chuo hichi kimeanza, na hata sasa kinaendelea kwa Elimu 1.0; lakini kusudi na azimio, kwa mujibu wa Maono ya Taifa—kadri lilivyoasisiwa na waasisi wake, akiwamo Mwalimu Kambarage Julius Nyerere, ni siku moja hichi kiwe ni ‘Mwenge wa Liberiti’ kupitia Elimu 2.0…
Kiouno na ufikirifu mifumo, wasomi wote ambao ‘wameelimika’ kwa muktadha wa Elimu 1.0 lakini hawajafanya jitihada zozote za kuhama kutoka Elimu 1.0 kuelekea Elimu 2.0 anayoadha ya ‘Utumwa wa Kiakili’. Dhamira na Matendo yao, juu ya utaasisi wowote, hayatoakisi chochote tofauti, ama tuseme kuzidi, ya yale wanayofundishwa mashuleni na vyuoni -- hali hayo yote yana asili ya kujenga mifumo piramidi—nasibu ya wachache kuwatawala wengi, yaani >
u-Eliti<.
Urastafari unalingania ‘Utaifa’, na kunasibu Taifa hili na bara la Afrika na Watu wake; ni jambo hili lilikuwa kwa waasisi wa Taifa letu la Tanzania na viongozi walijitoa kidhamira na matendo ili uhuru dhidi ya ukoloni usiwe tunu ya hapa na pale ndani ya bara. Uono na Ufikirifu wa Waasisi hawa juu ya Dhamira ya hawa waasisi ilikuwa ni kuwa Taifa Moja ‘haliwezi kuwa huru’ na hali jingine pembeni yake ‘likiwa si huru’. Jitihada za Mwalimu Kambarage Julius Nyerere katika kuunga mkono harakati za ukombozi wa nchi za Kusini mwa Afrika kwa vitendo, na tena kwa hali na mali, ilikuwa ni moyo mkuu kwenye kuziishi kauli na kutekeleza azma. Hata leo hii, labda tu watu ni wenye kusahau—ama labda kutozingatia?; wimbo wa Taifa wa Tanzania, unaoimbwa mara kwa mara mashuleni na kwenye matukio makubwa ya Kitaifa, huazimisha Nia ya kusimama kwa Bara la Afrika na Kisha Tanzania…
Kauli za imani, shauku na Matazamio katika ‘wimbo wa Taifa’ zinashahibiana na maudhui ya utamaduni wa Kirastafari. Bob Marley alivyoimba ‘Africa Unite—Afrika Ungana’ alikuwa akisadifu mashauri yale yale ya kulingania watu wa Afrika kuungana ili waweze kusogea kutoka kwenye mfumo mmoja wa ‘kibabiloni’ na basi kuuendea ule wa ‘Baba’. Kwamba, Waafrika waamke na kuungana kwa manufaa ya watu wake na watoto—la leo lisisubiri kesho… Na basi ‘Baba’, kwenye >
Wimbo wetu Taifa< ndivyo twataja ni ‘Mungu’… Mungu Ibariki Afrika, Mungu Ibariki Tanzania… Kwamba, sisi tu ni watoto wa Afrika--watoto wa Tanzania… Hekima, Umoja na Amani iwe ndiyo ‘Ngao’ ya Viongoza njia kuelekea kulijenga Bara la Afrika; na kutokea kwetu hasa--Tanzania, Kudumisha Uhuru na Umoja, katika jamii ya wake, waume na watoto viwe ni njia ya baraka na uzima kwa Taifa...
Kiuono na Ufikirifu Mifumo, nguvu za ushawishi wa jamii kukaa pamoja asili yenye kufangamana na ‘muundo mkuu’ wa watu, nyakati na taasisi. Haya, walau kupitia Elimu 1.0, tunayafikia kupitia mashauri ya kisosholojia -- kuhusiana na fanusi jamii, nadharia migongano na muingiliano wa alama oanifu. Kutokea kwenye ‘Elimu 3.0: Ilimu ilivyo ni metafizikia ya Elimu’, ndiyo twaja kubaini ni namna gani ‘muundo mkuu’, ‘nyakati’ na ‘taasisi’ ni muktadha wa ‘Metafanusi’ kwa sura na miendendo ya jamii…
Kwa hivi, kwa neema ya Elimu 3.0, Mungu ni ‘Metafanusi’ ya jamii yoyote, kiumbe chochote sentienti—iwe mtu-ardhini, nyangumi-majini, vinyamkera-hewani, majini-plazmani, sayari, mfumo wa Jua na hata ulimwengu wote mzima. Ikiwa mtu hana Elimu 2.0 yenye kukirimika neema za Elimu 3.0 basi atabaini ukweli wa ‘Metafanusi’ hata kwa ‘upofu wa kiroho’--kuamini ama kusadiki chochote alhali hicho ni chenye kufanania na ‘imani’ yake kwa wakati, ‘upeo wake wa uono’ na ‘uwezo na vina vyake vya tafsiri akilini mwake’ kwa yale mambo yajitokezayo katika mazingira yake…
Hili litupe daraja ya kuanza kujinasibu na mambo yaliyositirika…
Kiufundi, hauwezi kuunda taifa thabiti ‘kwa maneno’ na maelekezo rahisi. Walau, kinachowezekana ni kuijenga jamii kutoka nje, kwa kutumia amali za nchi huku ukitaasisha ‘alama’ za utaifa na kuzienzi ‘tunu’ zozote zinazoweza kubayanika katika jamii inayoelekea kudumu kukaa pamoja. Kwa ukweli huu huu ni vigumu kuwaunganisha watu na huku kumbe kila mtu katika jamii hiyo anasadiki lakwake—kuhusiana na ‘muundo mkuu’ wenye nasibu ya kutawala ustawi wa maisha yake. Hili ndilo kati ya mambo magumu ambayo waasisi wa Taifa la Tanzania walishughulika nalo, na Mwalimu Kambarage Julius Nyerere alikuwa akilifahamu hata kwa ‘Jicho la Ziada’…
kuliinua taifa kutoka umma wa makabila zaidi ya 120, yenye mila na desturi mbalimbali; huku ukijitahidi kabisa kuepusha ‘ukabila’ katika taifa jipya ama kasumba ndiko kulitatuliwa na ‘lugha ya Kiswahili’ pia utayari wa nidhamu/uwajibikaji kwa ‘Elimu na Utumishi’ kokote. Katika siku zetu za awali Kitaifa, mtu kutoka Dodoma kwenda kusoma Moshi, tuseme kutoka elimu ya msingi kwenda Sekondari; na huko Moshi kukutana na wenzake kutoka Mikoa mingine mbalimbali—labda Kagera, Mara, Tabora n.k si kulipunguza ama kuondoa ukabila na ukanda—hili ni sehemu ya uhandisi jamii. Haya mawili si tu yametuletea utangamano, pia yametuletea ‘kuoleana’ na ‘muingiliano’ wa kimakabila usioendekeza kasumba na ubaguzi… Vile Mwalimu Nyerere alikuwa akipiga marufuku kasumba za kuulizana makabila—kana kuwa je, tunataka kutambika?
Kwa mtu wa Kiuono na Ufikirifu Mifumo, Mafanikio ya jitihada za Mwalimu Kambarage Julius Nyerere katika kulijenga Taifa la Tanzania, kwa kipindi cha miaka 60+ ya hii leo, ni mkubwa sana na tena ya kipekee sana katika historia yeyote ya karibuni hapa Duniani; ipo namna ya kuona pia alilolianzisha bado linaendelea—halikufika mwisho.
Kutoka kwenye stawi za kimakabila na kuelekea ‘Utaifa’, katika nchi ya Tanganyika na kisha Tanzania, ni jambo lililohitaji maarifa na sanaa ili kukadirisha muktadha wa sura ya mienendo na maendeleo ya jamii. Kuzibuni na kuzitaasisisha mila, desturi na mapokeo mapya ya utaifa, kwetu Tanzania, busara na hekima vilitumika kwa matatu yaliyo ni fasaha, dhamira na makusudi yake—‘Dhana ya Uhuru’, ‘Ukombozi wa kifikra na Maendeleo’ na ‘Kuujenga Umoja wa Kitaifa’… Haya matatu, kwa sanaa ya utaasishaji wa alama oanifu, ndiyo huwakilishwa kwa alama ya ‘Bendera’--usovereini wa nchi-taifa, ‘Mwenge wa Uhuru’--Mwangaza kwa Maendeleo na kujichagulia; na ‘Wimbo wa Taifa’-- nadhiri katika watu kuhusiana na utaifa wao na mustakabali…
kiuono na Ufikirifu mifumo, kutokea kwenye daraja la Elimu 3.0, Ilimu ilivyo ni Metafizikia ya Elimu, ushiriki wa watu kama kikundi katika matendo, mazoea na tabia, na zaidi ‘kaida’ za imani huleta udumifu wa sura ya jamii na tena kwa wakati wake. Kukongoroa hivi huweza kusambaratisha jamii inayoshiriki hayo, lakini kati ya hivyo vyote--’kaida’ za kiimani ndizo zenye nguvu katika mashikizo ya taasisi za watu. Mfano wa ‘kaida’ za kiimani, ni matambiko…Kwa hivyo, Elimu 3.0 inaweza kuleta ufunuo, ni namna gani ‘mizimu’,’maruhani’, ‘miungu nchi-taifa ama dola-jiji’ n.k hupata ‘pumzi ya uhai’…
Kutoka kwenye ‘mifumo ya kikabila’ hadi ‘mifumo nchi-taifa’ Tanzania kama taifa kuna tunayoyapoteza na kuna mapya tunayoyajenga. Labda ni vema sana kujua tulikotoka ili tujue tunakokwenda… Kwenye fremu-kazi ya uono mifumo kwa ajili ya mambo ya ‘machaguo ya kitaasisi, ‘Jamii’, ‘wakati’ na ‘matukio’, jambo hili huchanganuliwa kitopografu kwa mahusiano ya ‘Kumbukumbu/Uzoefu’…
Kiuono na ufikirifu mifumo, utatu wa mihimili ya imani kwa ‘fanusi mtu/jamii’ hufanywa na ‘Jaala’, ‘Kumbukumbu/Uzoefu’ na ‘Wakati’… Hii ni namna ya kubaini kwamba mtu ama jamii huwa na vipawa vya akili kumfaa yeye/yenyewe na ‘kumbukumbu/uzoefu’ ili apate kujitambua msimamo ama mustakabli wake kiwakati. Wakati una usiku na mchana, asubuhi-mchana-jioni, masika-vuli-kiangazi-kipupwe kulingana na jiongrafia na mazingira. Kumbukumbu/uzoefu wa kuendana na haya mambo ya nyakati ndiyo hadhi ya ‘uwezo au uduni’ wa mtu kuyamudu mazingira yake—Elimu basi, ndiyo shughuli ya ziada inayoweza kuchochewa kwa mtu/jamii kusudi mtu/jamii iweze kujikwamua kutoka kwenye sura duni/hafifu ya ustawi, kulingana na vitendo vya miundo ya jamii yake, hadi ile bora. Hatua kutoka kwenye sura duni hadi sura bora ya ustawi wa jamii ndiyo dhana hasa ya ‘Maendeleo’.
Elimu 1.0: Kujua kusoma na kuandika, kwa mapana ya ujumla wake ndiyo huwa na shabaha kumpa mtu/jamii maarifa ili ibaini uduni wa hali na utendaji wake wa kila siku; kuufuta ujinga kwa kuipatia jamii na wanajamii wake ‘fikra’, ‘ujuzi’ na ‘maarifa’ kwa ‘visomo rasmi’. Kiuono na ufikirifu mifumo, Elimu 1.0 inasaidia sana jamii kupata taarifa na ufahamu wa mambo kufaa ’kumbukumbu la mtu’ na si zaidi. Walau katika hii, Taarifa/Habari ni nguvu… Mtu mwenye elimu, kwa sura hii, anawezakuwa ni mtendaji bora kulingana na maarifa aliyoyapata – pale ambapo huyu alinganishwa na yule asiye na hayo maarifa.
Elimu 1.0: kujua kusoma na kuandika, haina majibu hasa ya ‘ukweli wa mambo’ ila tu kwa habari za kuandikwa, kusimulika, kudadavuliwa na fasihi. ‘Ukweli wa mambo’ kwa Elimu 1.0 ni kitendawili, kila mtu/mwanajamii hubidi ‘hutoa mji’ ili kiteguliwe… Hii ni kwa kuwa Elimu 1.0 hutegemea na ‘kiu ya mtu’ ya mtu kutafuta maarifa, na kama vile tusemavyo Wabantu, ‘kimfaacho mtu ni chake’… Ikiwa mtu/wanajamii wanaridhika na vile vilivyo—kwa maandishi, simulizi na mapokeo, kadri vipatikanavyo katika jamii husika, basi yote yanayoambatana na ‘kujua mambo’ kwa sehemu – iwe ni kwa ‘kina’ ama ‘ujuu juu wa mambo’; basi hivyo ni halali yao.
‘Upokeaji’ ama ‘utayari’ kwa Elimu 1.0 katika mtu huratibiwa na ‘hali ya kujisikia’ ama ‘kuhamasika’ katika mtu/mwanajamii. Hili ndilo linaloingiliana na >
‘tabia za kuigana’< kama ‘chachu’ ya mabadiliko ya jamii. Kuna namna ya kuona binadamu kama kiumbe ana ‘matatu katika moja’ ilivyo ni (1)Mwili, (2)Imosha (hisia) na (3)Roho… Vitatu hivi katika moja ni sehemu ya muktadha wa ‘mbegu’ ya kuwa kwamba ‘akipandacho na kukivuna’, mtu ama jamii, katika jamvi la ‘wakati’.
Matukio yote katika maisha ya mwanadamu, ndiyo basi kusema ni ‘kuvuna ama/na kupanda’ yale yote yafanyayo ‘ustawi’ ama/na ustaarabu wa mtu/jamii husika.
Mtu ni mwenye nasibu ya kuiga kutoka kwenye ‘matendo ya asili/dhahiri’ ama ‘matendo ya mwanajamii’ mwingine kama sehemu ya ‘kuotea’ maarifa. Kadiri mtu aridhikavyo na ‘kawaida’ ama ‘kaida’ ya matendo ya jamii, huyu pamoja na wanajamii wenzake hufanya muktadha wa ‘desturi’. Na yale matendo ya kujirudiarudia katika jamii ndiyo visomo vya leo kisosholojia hufahamika kama >
‘nomu mahsusi/nomu jamii’<; nomu, tunatohoa kutoka kwenye neno la Kiingereza ‘norm’--kawaida ya jambo/mambo. Basi ndivyo hivi sisi wabantu husema ‘Kawaida ni kama Sheria’… Kwamba katika jamii, Mazoea hujenga Tabia…
Sehemu ya Maarifa isiyofasaha katika jamii, itokanayo na mambo ya kuigana, ndiyo hufanya ‘mila’ za wanajamii. Mila ni muktadha wa matendo ‘usiohojiwa’ kwa wanajamii, bali kufuatishwa na kuenziwa kutokana na ‘busara’ za ‘wazee’ ama pia ‘Wahenga’. Hili kuwa kana kwamba, mila ni daraja la jamii kupata ‘baraka’, ‘kinga’, ama pia ‘bahati’ kwa kadiri ya kufuatishwa kwake na tena kwa taratibu zake. Kwa hivyo kiufundi, mila ni ‘utaasisi’ juu ya ‘jaala na wakati’ kwa wanajamii. Mila ndiyo msingi wa ‘mema’ ama ‘mabaya’ ambavyo kufuatishwa ama kutofuatishwa kwake huonekana, kwa kusadiki, ni chanzo cha ‘mapatilizio’ ama ‘thawabu’ kwa wanajamii…
Kwa mujibu wa ususi wa Taifa letu la Tanzania, kati ya adha kuu zilizopata kuwa ni kigingi kwa mageuzi ya kijamii ilikuwa ni utitiri wa ‘mila na desturi’ za makabila mbalimbali yaliko katika mipaka ya ‘nchi-dola mpya’. Yumkini watu wengi hata leo hii(2022), hawang’amui wala kubaini mambo ya ‘kiufundi’ yaliyohusika ama/na yaliyopitiwa na viongozi waasisi wa taifa hili, miongo ya awali, baada ya kupata ‘uhuru’. Ikiwa watataka kufahamu basi inawapasa kuwa na mapana sahihi ya maarifa juu ya ‘sosholojia’ na ‘uhandisi jamii’.
Elimu 1.0: Kujua Kusoma na Kuandika, tokea siku za awali za kupatikana uhuru wa taifa, ilikuwa na makusudi si tu kuwapitia ‘taarifa’ na ‘maarifa’ wanajamii ya Tanzania(Tanganyika) juu ya taratibu za maisha bora—yakuendana na mambo ya walimwengu kungine kote duniani; hii ilikuwa inakusudiwa pia kutokomeza ‘mila na desturi’ potofu za hao hao wanajamii.
Kutokomeza ‘Mila na Desturi’ potofu, haijawahi kuwa jambo rahisi kokote duniani… Mila na desturi ni ‘Utaasisi’; hivi hufangamanisha ‘miundo ya kijamii’, ‘kujisikia’ na ‘ushawishi’… Haya ndiyo kwa mfano, hufanya koo na uchifu kwa makabila yetu ya Kiafrika. Chifu kuwa ndiye >
‘Bwana wa ma-Bwana’< na Baraza lake kuwa ni ‘Wazee wa ki-Mila’. Kazi ya Wazee wa ki-Mila ndiyo kusaidia utawala wa Chifu-- >
Washiriki-kwa-Kina<, kwa ‘mambo ya jadi’ na >
‘Ufundi wa Mizungu’<…
Labda watu wengi, wamepuuzia kama si kujisahau juu ya misingi ya mila na desturi zetu kama watu wa makabila anuai kutoka katika vizazi vyetu humu barani Afrika. Kuna mambo ni vema wanajamii wakayatafuta na kuyadadisi ili wapate vina sahihi vya maarifa na ukombozi wa kifikra. Kutokufanya hivi, wanaweza kujidanganya kufikiri wamepiga hatua na kumbe bado ni ‘wabichi’ katika dhana na tafsiri ya ‘maendeleo na ustaarabu’.
Marja Liisa Swantz, almaarufu 'Mama Maendeleo', ni miongoni mwa wanavisomo wengi ambao wamefaulu kufanya visomo maridhawa juu ya jamii zetu za asili pasi kasumba yeyote, na kuleta hazina ya kipekee ya Kisomo Elimu 1.0, kwa mfano yeye kutuletea:
>'Kaida na Alama katika Jamii Mabadilikoni ya ki-Zaramo--Ritual and Symbol in Transitional Zaramo Society'<. Humu anaeleza mengi, kuhusu maisha yake nchini Tanzania kipindi cha mabadiliko makubwa ya Kijamii, akitumikia jamii ya Mwambao, Bunju. Kutoka katika jamii hii yeye alipata fursa ya kufahamiana na wenyeji kadhaa; na kutoka kwao kujifunza; na pia kufanya kisomo kuhusu mambo ya watu wa kabila la Wazaramo--mila na desturi, imani na mazoea yao... Haya yote akiyabaini katikati ya mabadiliko ya ‘Kitaifa’ kutoka kwenye 'sura ya mienendo ya kiasili' kuelekea katika harakati na pilika za kutekeleza 'Siasa za Ujamaa na Kujitegemea'…
Mama Marja Liisa Swantz, ni mfano wa 'Waafrika' kwa moyo, ‘Wazungu kwa Asili ya Mwili’... Hawa, tunaoweza kuwaita ni ‘raia wa ki-geni’ kwa macho ya juu juu na utaasisi wetu wa kileo juu ya uzalendo, wamekuwepo, wapo, na wengine watakuja, kutokea kote mashariki-magharibi-kaskazini-kusini na 'kuimalizia kazi'... Tutakuja kuyafahamu mengine mengi kuhusiana na hili kupitia Elimu 3.0...
Kwa mtu Uono na Ufikirifu Mifumo, Mambo ya ‘Elimu 1.0’ pamoja na ‘Mila na Desturi’ ndiyo huleta muktadha wa ubainufu wa >
‘elementi ya Kiza’< katika jamii yoyote; jana leo na kesho. Elementi ya Kiza ni ile sifa ya mtu kuwa na sehemu ya yeye, >
asiyofahamu ama kujifahamu<, na huku hiyo ikiwa ni sehemu ya ‘uzima’ wa maisha yake na mwenendo wake kama mtu mmoja ama jamii. Hii ni matokeo ya ‘mwangaza’ alionao juu ya ‘hisia zake’ na ‘vina vya tafsiri’ kwa >
‘uono’< wa >
‘ontolojia ya Taasisi’< zake na >
‘Sura na Mienendo’< ya jamii yake… Kukosa mwangaza kamili katika kuyamulika haya, ndiko humfanya mtu >
kujua mambo kwa sehemu<, na basi yeye atayaishi maisha yake kadiri ya vile Elimu 1.0 ya sosholojia itazungumza kwa minajili ya >
‘fanusi jamii’, ‘nadharia migongano’ na ‘Muingiliano wa alama oanifu’<…
Kwa hivyo kwa mtu wa Uono na Ufikirifu Mifumo, suluhu ya adha za ukomo wa manufaa ya 'Elimu 1.0', 'Mila na Desturi' na pia 'Elementi ya Kiza' ipo katika jambo tunaloweza kulibayanisha ni >
'UPENDO'<. Ili mtu kunasibika 'nuru ya ufahamu' juu ya fanusi zake jamii, nadharia migongano na muingiliano wa alama oanifu, huyu hana budi kuwa na 'hisia' na 'vina vya tafsiri' tofauti na makundi ya watu wasio na upeo ama kukosa kujua ilivyobora…
Kama vile tunavyoweza kuona katika Urastafari juu ya ‘Upendo JAH’, ‘Pendo Moja’ na ‘Udugu I’n’I’, Kumuona mwingine kwapasa kuwa ni Kujiona mwenyewe kadri Akuonaye wewe, ndiye amuonaye mwingine – mlivyo wote ni ‘Moja’… Kiufundi hii ndiyo ile asili ya >
‘Jicho la Upaji’< kama alama ‘fumbo’ ya >
jumuiya siri ya Illuminati<, japo alama yenyewe ni ya siku nyingi kupita mwanzo wa Illuminati yenyewe ya kuanza na Adam Weishaupt... Jambo kama hili hili kuwa ni asili ya usemi >
lak'ech ala k'in< kwa staarabu za Mayani, Amerika ya Kati ya Zamani…
Kwa mtu wa Uono na Ufikirifu Mifumo, vile katika sayansi huzungumzwa ya >
'Muona ni Muonwa'< katika ulimwengu wa fizikia ya kikwantumu, ni topografu sambamba na haya yote ya 'utabia wa kichanzo' na basi pia 'Ontolojia ya Taasisi'. Hivi ni sawa sawa na kusema, >
kupitia kila mmoja wetu sentienti, Mungu ni jicho lionalo kote na mote< na hali kumbe >
'ufahamu pofu wa milango sita'< wa kiumbe huwa na 'kibanzi/pazia' katika ile sifa na hadhi ya kukosa ubayanifu wa ukweli wa jambo. Kwamba mtu, si mkamilifu--akipata ukamilifu atang'amua, mambo yake yote--ustaarabu wake wote na ustawi, kabla ya ukamilifu kufika, umepata kuwa ni 'utoto'. 'Atajijua' kama vile 'Ananavyojulikana'--na hili ndilo labayanisha muktadha wa >
'kukumbuka, kujikumbuka na Kukumbukwa'<.…
Wakati mmoja, siku za mbele, ‘Muona ni Muonwa’ ndiyo itakuwa alama yunivasali ya ‘ujuzi na uwezo wa kubaini sura nyingi za mambo kwa wakati’--intelijensia...
Haya yote yanatukaribisha kwenye ‘Elimu 3.0: Ilimu ilivyo ni metafizikia ya Elimu’…
...
-_-