Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Huyo hakai dar ni mkazi wa pwani [emoji61] mimi nadeal na madealer wa dar tu[emoji40]Riz two hayipo???? Dah makubwa
nilimsikia akisema "karatu Pakistan" badala ya "karachi pakistan"[emoji23][emoji23][emoji23]
Kuna lugha ya kisanii imetumika wachache tumeielewa: Kuna wengine wanatumia, Kuna wengine wana taarifa by Makonda. Hapa Kuna hatari ya kushangilia chenga za mazoezini!.Hii ni vita ya kisiasa ,mimi siamini Mbowe awe mjinga kiasi hicho awe anajihusisha na madawa ya kulevya
Kumekucha!!Ni siku nyingine tena,Mkuu wa Mkoa na Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wa mkoa wa Dsm,ndugu Paul Makonda ataongea leo na waandishi wa habari kuhusu muendelezo wa vita ya madawa ya kulevya ktk jiji la Dsm.
Mkuu wa Mkoa atakuwa mubashara Azam Tv mara ifikapo saa 05:00 asubuhi leo hii.
Tetesi ni kuwa,mkutano huo unaweza kuwa ni kujibu tuhuma za kuwa anawakabili "dagaa" na wakati "mapapa" wa biashara hiyo wapo.Na majibu ya mkuu wa mkoa yatakuwa ni kuwataja hao mapapa na kuelezea hatua zitakazochukuliwa...
Tega usikie....(Stay Tuned)
=======
UPDATE:
=======
ORODHA KAMILI:
View attachment 468414
View attachment 468415
View attachment 468416
View attachment 468420
Ameanza kwa Kumshukuru Rais wa Jamuhuri.
Paul Makonda asema anataka wauzaji wa dawa za kulevya wajulikane hadharani na hakuna sababu ya kuficha.
Paul Makonda asema vita vya dawa za kulevya vilianza muda mrefu kwa kufutilia hali ilivyo mitaani.
'Kuna watu nilitaka nikutane nao polisi, kuna tofauti kati ya kukamatwa na kuitwa, unapoitwa unapewa nafasi ya kusikilizwa'-RC Makonda
'Kampeni hii dawa ya dawa za kulevya si ya kufanyika kimyakimya tunataka hata watoto wadogo wajue dawa hizi ni hatari kwa afya'-RC Makonda
'Asante kwa watu kama TID, nawapongeza kwa kukiri na kusema kuwa wanatambua namna walivyoingia na kuomba serikali kuwasaidia'-RC Makonda
'Tumemaliza awamu ya kwanza vita ya dawa za kulevya, sasa hii ni awamu ya pili ambayo itakuwa si nyepesi itakuwa na mawimbi mengi-Makonda
'Awamu ya 2 ya vita ya dawa za kulevya tunaianza leo na tunaianza tukiwa tumekamilika, nimekuwa kwenye operesheni usiku na mchana- Makonda
'Watu wanafanya biashara za dawa za kulevya na meli zinazokuja na mafuta'-RC Makonda
'Kuna mama kazi yake ni kusafirisha watoto wa kike ambao wanapewa dawa za kulevya, wawili wako jela China na amewatelekeza'-RC Makonda
'Tukiendelea kuvutanavutana tutapoteza lengo la kupambana na dawa za kulevya'-RC Makonda
'Tukishindwa vita hii ya dawa za kulevya, hajashindwa Makonda au Rais Magufuli tumeshindwa wote'-Rais Makonda
'Tuko na majina 65, nitahitaji kukutana nao ijumaa, wako wanaosemekana wanatumia, wako wanasemekana wanazo taarifa zitakazotusaidia-Makonda
'Nawashukuru wenyeviti wa mitaa wameanza kuleta majina ya watu ambao wanawasiwasi nao kuhusu dawa za kulevya'-RC Malone's
'Kila tunayemuita tunamfahamu kuliko mnavyofikiri kazi yetu ni kuwasikiliza'- RC Makonda
'Zile nyumba mnazozitilia shaka, hamuelewi hata kinachoendelea ni wajibu wetu wananchi kutoa taarifa na taarifa zitakuwa ni siri-RC Makonda
'Kuna ambao tuliwaita wako nje ya DSM, wapo waliotoa taarifa na watafika ila wapo waliokimbia tunawafuatilia na tutawapata wote'- RC Makonda
'Nawashukuru ndugu zangu walioko nchi mbalimbali kwa kunipigia simu na kunipa taarifa mbalimbali'-RC Makonda
Hamna kitu hapo
Wangapi CCM ......!?Mwana CBE kumbe wewe ni kielelezo tosha cha vijana na wafuasi wa BILICANAS club walivo wachovu wa kufikiri, Makonda kamtaja mtu mmoja tu waupinzani leo mnakuja kusema anatka kuua upinzani hahahahahah duh Mungu wa nchi hii tunampa kazi kwelikweli inabidi aanze upya kupitia baadh ya bongo zao
Kuna mmoja nadhani alionekana akimfunga kamba za viatu.M
Makonda ni kijana wa vuijiweni, hana ushahidi hata tone zaidi ya kutafuta misifa
Angetakiwa ajibu tuhuma za Jana bungeni kwanza na katika list hiyo ameshindwaje kuwataja watoto wawili wa marais wastaafu?
Huyo hakai dar ni mkazi wa pwani [emoji61] mimi nadeal na madealer wa dar tu[emoji40]
wakati anataja alisema kabisa kaka yangu freeman mbowe tena akaongeza mbunge wa hai lakini makazi yake ni hapa DarHilo ndio swali langu pia. Aliyeorodheshwa kwenye orodha iliyowekwa hapa ni Philemoni Mbowe. Clearly, huyo hawezi kuwa Freeman Aikaeli Mbowe. Sijamsikiliza Makonda wakati anataja haya majina. But it will be interesting to know kama alitaja Freeman Mbowe wakati orodha inasema Philemoni Mbowe. Kama wamekosea makusudi, basi watakuwa na lengo la kui-confuse jamii. Je, kuna mtu anafikiri jina la Freeman Mbowe linaweza kukosewa? Kwamba mtu aandike Philemoni Mbowe badala ya Freeman Mbowe? Maybe. Kukosea makusudi ni siasa.
Maswali ni mengi mnoo..Hata huyo Mbunge Msukuma anautajiri wa kutisha sana na taarifa zinasema nayeye ni alikuwa/muuza poda thus why ameng'aka na hii vita ya Makonda..
Na kwanini Msukuma akae kimya kipindi chote hicho mpaka baada ya Makonda kuanza hii vita ya madawa ndiyo yeye alipuke? Where is his moral Authority?
Mwacheni Makonda amalize vita yake then tutakuja kujadili hizo tetesi zenu.
# Hakuna kiunga cha dsm ambacho hakitafikiwa.
Lakini jina limeandikwa Philemoni Mbowe.Amesema Mbunge wa Hai
Umelipia sh ngapi we bibi.