Vita dhidi ya Dawa za Kulevya awamu ya Pili: RC Makonda awataja Mbowe, Manji, Gwajima, Idd Azzan...

MANJI AVAE KOTI LAKE AACHANE NA KOTI LA YANGA. PIA GWAJIMA AVAE KOTI LAKE LA YESU ALIACHE KANISANI.
 
mi sioni ubaya wowote kwa wao kujitetea hata kama kweli ni mapapa maana kujitetea ni haki ya kila mmoja pindi anapotuhumiwa
 
Halafu pengine penye Mushkeli ni pale aliposema ya kwamba RAID itafanyika Nyumba hadi Nyumba.

Unajua kwanini nasema pana Mushkeli?

Kwasababu inakuwa Anawasanua/Anawaamsha Magwiji, sasa hapo kama wanapigilia Mizigo yao, Mazabe yao, si ndio inakuwa rahisi kwa wao Magwiji kuyahamisha Mazabe yao!

Hata kama umepewa fununu Mazabe wanayahifadhi Majumbani mwao, au kwenye Machaka yao wanayohifadhi KAZI zao, hutakiwi kumwaga Mchele hadharani.

Unapotaka kufanya RAID inatakiwa uibuke kiOSAMA, sio kutangaza Mbinu zako.

Watu wa Ngada wana mipango, mbinu, na ni wajanja kuliko unavyofikiria.

Sio Watu wa kuwachukulia kiwepesi wepesi hata kidogo.

Kwahiyo utakapotaka kupambana nao inabidi ujidhatiti haswa
 
Nia njema nnayo, na namuunga Mkono, nawaunga Mkono wote wenye Nia ya kutokomeza, au naweza sema kupunguza Kasi ya Madawa ya Kulevya Bongo.

Lakini penye mapungufu tuseme ili Mistari inyooke/Twende sawa.

Kumbuka huyohuyo Masogange alishawahi kamatwa na Madawa ya Kulevya, na Vizibo ubaoni.

Na yeye Mkuu wa Mkoa hapo kwa Masogange kachemka mara mbili.

Suali la kwanza, alijibu "kujuana sio tatizo". Jibu unapata kwamba Wawili hawa wanafahamiana/wanajuana.

Suali la Pili, alishikwa na Kigugumizi cha ghafla na akawa mzito, na kama amenyong'onyea fulani, na kufikia mpaka kujikuna Taya yake. Pale Suali lilikuwa zito na lilimuingia haswa.

Hata kama tufanye ndio Propaganda, kwa hadhi yake pale mbele ya Waandishi alitakiwa ajibu kihadhi yake, sio kujibu kama vile yuko Kitaa, Skani, au Pande zozote zile ambazo za kujiachia, ukijibu Kisela sio Kesi. Ila si kwa pale
 
Na hitilafu nyingine ni pale alipojibu Suali la Mdau mmoja , "hayo mambo ya Mikoani (Nje ya Dar-es-Salaam) wana wakuu wa Mikoa yao", yeye ni kwa DAR tu.

Sasa anawezaje kutangaza Vita dhidi ya Madawa ya Kulevya mpaka Nje ya Mipaka na iweje iwe ngumu ndani ya Nchi, iwapo Magwiji wanafahamika, au Raia ametoa ushirikiano.

Pale inabidi kufanya Ushirikiano na Wakuu wa Mikoa wenzako, iwapo wewe Muhusika umepewa taarifa ukiwa ndani ya Mkoa wako.

Sio mambo ya kusema wao wana Wakuu wa Mikoa yao.

Kama umepewa wewe taarifa wa DAR ni kwamba, DAR ndio makao makuu, na wewe umeonesha ndio mwenye Nguvu ya kupambana na hii Vita, Piga Kazi na wenzio.

Na kumbuka Mateja DAR ni wengi kulinganisha na nje ya DAR, kwahiyo inapotokea kupewa taarifa Magwiji Nje ya Dar, suala ni kuwajibika tu bila kujali mipaka
 
Mkuu wa mkoa unaendelea kulisaidia taifa kuondokana na biashara ya madawa ya kulevya.

Na umeonyesha ujasiri na ukomavu pale ulipotaja majina yao kwenye vyombo vya habari, na kuwataka uliwataja kufika polisi.

Inamaanisha unaweza kujenga taifa likaondokana na biashara ya madawa ya kulevya ambazo kila mtu anajua madhara yake.

Lengo letu ni taifa lisonge mbele siyo tu kwa kumaliza hii vita ya madawa ya kulevya.

Kwa kuwa umekuwa jasiri wa kutaja majina na tunakupa hongera.

*SIYO MADAWA YA KULEVYA PEKEE YAKE YANORUDISHA NYUMA MAENDELEO YA TAIFA HATA WALIOTUIBIA FEDHA ZA TAIFA LETU WAMETURUDISHA NYUMA*

NAOMBA:-
TUNAKUOMBA UWATAJE MAJINA NA WAJE KITUONI WARUDISHE FEDHA.

1.LUGUMI
2.ESCROW
3.WALIOFICHA FEDHA NJE YA NCHI MAJINA YAPO.

TUNAKUOMBA KUPITIA TV NA VYOMBO VINGINE VYA HABARI WAITE KITUONI KWA KAMANDA SIRO.
 
Awaite kwani yeye anamamlaka gani?
Ni nani katika nchi hii, vita hii ya ufisadi inawatu wake ambao wanalindana tu
 
Hahaha, hana wa kumlinda huko, hana maslahi....huku kwenye sembe kuna wadau wake. Kama alishawahi kwenda hata Nairobi kabla ya kuwa RC, sitashangaa kwenda mapumziko Dubai au Paris
 
Nimesoma kati kati ya mistari, nimekuelewa mkuu.
 
Hivi unayajua majukumu ya RC na mipaka yake wewe, nyie ndo mkipewaga uongozi mnavuka mipaka ya Uongozi....shwaini kabisa
 
Kwetu sisi wenye umri mkubwa kidogo hoja ya wabunge kuita watu bungeni ati kwa kisingizio cha kudhalilishwa hakikuanza leo. Mwanzoni wa miaka ya 2000 kuna Mhariri aliwahi kuitwa kwa sababu gazeti lake lilichapisha 'habari za kudhalilisha wabunge'.

Kwa kipindi cha takribani mwaka mmoja wabunge hususani wa upinzani wamekuwa wakipigania kile kinachoitwa 'udikteta' wa raisi, kwamba hataki kukosolewa. wamesema kila aina ya lugha chafu hadi kufikia 'kupanga njama za mauaji' kwa kisingizio cha unabii lakini haya yote yanaonekana ni demokrasia.

Zitto Kabwe akijenga hoja amesema 'kila muhimili una wivu' sasa kama ni hivyo kwanini hakuna heshima kwa Raisi (mhimili wa dola)? Kila kukicha mmewatukana wakuu wa mikoa,wilaya kuwa ni vibaraka je huu si udhalilishaji?

Kama Makonda eti kwa tuhuma za kusema 'wabunge wanachekesha, wanasinzia' amedhalilisha bunge na wabunge kiasi cha kutoa hoja afutwe kazi basi hatuna uhalali wa kumtetea Lema na Mkewe kwa kumdhalilisha Raisi Dr.Magufuli na RC Gambo tena kwa ushahidi.

wakiwajibika Makonda na Mnyeti basi Lema,Lissu,Mke wa Lema na wengineo hawatapona kwani hukumu hiyo ya wabunge inatengeneza 'rejeo' la mhimili mmoja kutoingilia mhimili mwingine kuwa ni kosa.

Leo wanaojiita wanademokrasia' wanatumia kanuni za bunge kuwaminya wakosoaji wa wabunge, Leo mbunge anaongopa eti kapigiwa simu huku anayemshitaki hayupo bungeni? ni wapi sasa tuna uhalali wa kudai 'natural justice'

Hoja hii ya wabunge sasa inahalalisha ni haki na sahihi kabisa kwa Dola kuwachukulia hatua wabunge wote wanaokosoa na kumdhihaki Raisi nje ya bunge.
 
Kama alishawahi kwenda hata Nairobi kabla ya kuwa RC
Hivi akili yako na wewe ndio ilipo ishia yaani mtu kweli kwenda NAIROBI unashangaa, wangapi kila wiki wanaenda mapumzikoni ughaibuni acha akili zako za kudaka kwa kisimbusi wewe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…