Vita dhidi ya Dawa za Kulevya awamu ya Pili: RC Makonda awataja Mbowe, Manji, Gwajima, Idd Azzan...

Vita dhidi ya Dawa za Kulevya awamu ya Pili: RC Makonda awataja Mbowe, Manji, Gwajima, Idd Azzan...

Kutaja hakusaidii kitu so long as hakuna nia ya dhati au hakuna uwezo wa kuyashughulikia. Kikwete aliondoka na majina ya wauzaji kimya kimya. Kuwataja hadharani ni kutafuta uhalali wa kisiasa kwamba ahadi zimetimizwa. Ni sawa sasa tudai kwamba hakuna ufisadi kwasa babu mahakama ya ufisadi imeanzishwa. Is it possible?


Naamini wewe BabM, pia una nia nzuri ya kupambana kwenye vita ya madawa ya kulevya. Kama niko sahihi, basi rekebisha mtazamo wako kuhusu njia sahihi ya kupigana vita hii.

Hakika, kukaa kimya kunaweza kuzaa matunda mazuri, lakini kuna ushahidi kwamba vita hii imekuwa ikiendeshwa kimyakimya, matokeo yake ni lawama kwa waliopewa dhamana ya kusimamia vita hii. Ati ni dagaa tu wanakamatwa!

Hivyo, ni sahihi wanaotuhumiwa kutajwa hadharani ili wananchi tuwajue na majina ambayo hayakutajwa yatajwe na wenye kuwafahamu uhusika wao.

BabM: kama una husika, au wamjua mhusika, salimisha taarifa. Ukitaja/ukitajwa, kwa vita ya madawa ya kulevya, utakuwa umejipunguzia 'pressure' ukawa na amani moyoni.
 
Kitendo cha kumtaja Mwenyekiti wa Chadema, Iddi Azan na Manji ni dalili tosha kuwa maombi yetu ya kuomba kuletewa mapapa wa madawa ya kulevya yamepuuzwa maana wameamua kutulete NYAGUMI.

JAMANI HATA MBOWE??????????????!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
Mwenyekiti wa chadema hajatajwa banaa
 
sipati picha gwajima atakavyofura, akitoka kuhojiwa, atatapika mpaka watajuta kumfahamu
Anaweza kuhojiwa na hapo hapo akawekwa ndani jumatatu akapandishwa mahakama ni Jmosi na jumapili hakuna dhamana hiyo ndio straight ya Makonda mchafua watu.
 
Season Bado Hina Endelea Maana Hime Kua Gumzo Nchi Nzima Hilisakata la Dawa Ya Kurevya [emoji87][emoji87][emoji87]
 
Wakuu Mimi kuanzia Leo siyo mwanachadema tena ni aibu kubwa sana mwenyekiti wetu kuwa na tuhuma kama hizi hata kama siyo kweli ni tuhuma kubwa kwake.

Nilivumilia ile ya kunywa Viroba Kwa sababu ni tabia binafsi ya mtu ila kwa hili la Kuuza dawa za kulevya limenichosha

Baada ya jina lake kutajwa nimedondosha simu yangu na kuvuja kioo kwa kweli imeniuma sana.
Ni lini ulikua mwanachadema ndugu yangu?? Mbona dume zima unajitekenya??
 



Kumekucha!!Ni siku nyingine tena,Mkuu wa Mkoa na Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wa mkoa wa Dsm,ndugu Paul Makonda ataongea leo na waandishi wa habari kuhusu muendelezo wa vita ya madawa ya kulevya ktk jiji la Dsm.

Mkuu wa Mkoa atakuwa mubashara Azam Tv mara ifikapo saa 05:00 asubuhi leo hii.

Tetesi ni kuwa,mkutano huo unaweza kuwa ni kujibu tuhuma za kuwa anawakabili "dagaa" na wakati "mapapa" wa biashara hiyo wapo.Na majibu ya mkuu wa mkoa yatakuwa ni kuwataja hao mapapa na kuelezea hatua zitakazochukuliwa...

Tega usikie....(Stay Tuned)

=======
UPDATE:
=======

ORODHA KAMILI:

View attachment 468414
View attachment 468415
View attachment 468416
View attachment 468420
Ameanza kwa Kumshukuru Rais wa Jamuhuri.

Paul Makonda asema anataka wauzaji wa dawa za kulevya wajulikane hadharani na hakuna sababu ya kuficha.

Paul Makonda asema vita vya dawa za kulevya vilianza muda mrefu kwa kufutilia hali ilivyo mitaani.

'Kuna watu nilitaka nikutane nao polisi, kuna tofauti kati ya kukamatwa na kuitwa, unapoitwa unapewa nafasi ya kusikilizwa'-RC Makonda


'Kampeni hii dawa ya dawa za kulevya si ya kufanyika kimyakimya tunataka hata watoto wadogo wajue dawa hizi ni hatari kwa afya'-RC Makonda

'Asante kwa watu kama TID, nawapongeza kwa kukiri na kusema kuwa wanatambua namna walivyoingia na kuomba serikali kuwasaidia'-RC Makonda

'Tumemaliza awamu ya kwanza vita ya dawa za kulevya, sasa hii ni awamu ya pili ambayo itakuwa si nyepesi itakuwa na mawimbi mengi-Makonda

'Awamu ya 2 ya vita ya dawa za kulevya tunaianza leo na tunaianza tukiwa tumekamilika, nimekuwa kwenye operesheni usiku na mchana- Makonda

'Watu wanafanya biashara za dawa za kulevya na meli zinazokuja na mafuta'-RC Makonda

'Kuna mama kazi yake ni kusafirisha watoto wa kike ambao wanapewa dawa za kulevya, wawili wako jela China na amewatelekeza'-RC Makonda

'Tukiendelea kuvutanavutana tutapoteza lengo la kupambana na dawa za kulevya'-RC Makonda

'Tukishindwa vita hii ya dawa za kulevya, hajashindwa Makonda au Rais Magufuli tumeshindwa wote'-Rais Makonda

'Tuko na majina 65, nitahitaji kukutana nao ijumaa, wako wanaosemekana wanatumia, wako wanasemekana wanazo taarifa zitakazotusaidia-Makonda

'Nawashukuru wenyeviti wa mitaa wameanza kuleta majina ya watu ambao wanawasiwasi nao kuhusu dawa za kulevya'-RC Malone's

'Kila tunayemuita tunamfahamu kuliko mnavyofikiri kazi yetu ni kuwasikiliza'- RC Makonda

'Zile nyumba mnazozitilia shaka, hamuelewi hata kinachoendelea ni wajibu wetu wananchi kutoa taarifa na taarifa zitakuwa ni siri-RC Makonda

'Kuna ambao tuliwaita wako nje ya DSM, wapo waliotoa taarifa na watafika ila wapo waliokimbia tunawafuatilia na tutawapata wote'- RC Makonda

'Nawashukuru ndugu zangu walioko nchi mbalimbali kwa kunipigia simu na kunipa taarifa mbalimbali'-RC Makonda


Go Makonda go go go Mungu yuko pamoja wa wale wote tunaoombea hii vita itokomezwe.
 
Tanzania hakuna kitu jina halisi, ukianza kutafuta Majina halisi utakesha hautampata mtu, utakuta mtu nyumbani anaitwa Moshi, Shuleni anaitwa John, kazini Mushi, basi mkanganyiko tu,
ila Mbowe ni Mbowe-chadema!
Unaijua force king?basi ndiyo hiyo na baada ya hapo mshindi hujulikana!Vita hii si ya kitoto.
 
Mmeahitaji mapapa yanatajwa bado mnasema wanaonewa sasa nani atakuwa tayari kuona mtu mkubwa anatajwa kama wakitajwa wanaonewa,
Juzi Mdee katoa povu juu ya wanaokamatwa kuwa sio waagizaji na wanasambzaji ok, leo wametajwa tena hakuna aliye sema kuwa wao ndo wanauza,kuaagiza au kusambaza alichosema Makonda ni kuwa waende pale kati wakatoe statement na kusaidia dola juu ya ishu hii.
Makonda mbona kasema ukweli kuwa kama umekamatwa kwenye hii ishu bila kuitwa basi ujue wanauhakika na walichokifanya akatoa mfano MAJIZO,

Sasa naona mapovu yanawatoka wenzetu wa kupinga kila kitu kuwa mwenyekiti wao kaonewa.
kwahiyo ullitaka nani awpo na nani asiwepo? et, naongea na wewe unaesoma hii
Huko Lumumba hata kusoma hamjui?
 
Hivi mbunge wa Ilala anaitwa nani? na yule alokuwa wa Kino anaitwa nani?....nani ni Zungu kati yao...haya majina na la huyo alowekwa hapo juu ni kama yanafanana....wasije mharibia mtu asiyehusika
Mussa Azzan-Ilala
Iddi Azzan-Kino
 
Jamani Mimi naona makonda anganza na wahusika wakuu ambao kuna ingiza madawa ili kuwanusuru vijana wenzetu

Dada angu, Madawa ya kulevya hayauzwi kwenye duka la Mangi..hakuna mtu atakupeleka kwa drug Lord kama hakuamini. Utaishia tu kukamata vidagaa vinavyo chukua kete mojamoja.

Ila mtu kama Ray C, Wema na wengineo obviously wanachukua kwa supplier wakubwa kidogo coz wana uhakika na privacy na confidentiality ya hao suppliers na Makonda amelijua hilo.

Ukianza kumkamta teja pale mwananyamala huo mlolongo wake kabla hujamfikia big suppliers utakuwa umeweka watu laki 5 pale Central.
 
Mfano we mkaazi wa KINONDONI, mfuasi wa CHADEMA, shabiki wa YANGA, nguo zako unanunua kwa HUSSEIN pamba kali, matanuzi yako ni SEA CLIFF, YATCH CLUB, PALM BEACH na mafuta ya gari yako unaweka GBP petrol station na ibada yako unapiga kwa mchungaji GWAJIMA.
mmh! pole we
 
Back
Top Bottom