Vita vya Gaza ndio vinahitimisha ukombozi wa kifikra kwa walimwengu wote.

Vita vya Gaza ndio vinahitimisha ukombozi wa kifikra kwa walimwengu wote.

Webabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2010
Posts
8,870
Reaction score
14,258
Uonevu,ubabe na udanganyifu pamoja na woga wa baadhi ya watu kwa binadamu wenzao ambavyo vimeoneshwa tangu mwanzo wa vita hivi hakuna shaka kutaleta mabadiliko ya maana kwa dunia nzima.
Kwa nje na kwa akili za kibinadamu kuna watu wanadhani Hamas na wenzao ndani ya Palestina wameshindwa.Kiundani vita hivi vitaondoa moja kwa moja fikra ya kumtegemea binadamu kutatua matatizo yako.Kila mmoja ataamua kujitetea kwa silaha aliyonayo mpaka mwisho wake bila kujali kiwango cha hasara atakachopata au kumsababishia adui yake.
Vitu visivyo vya kawaida ambavyo vimeonekana mubashara vimewafanya binadamu wasajili kwenye akili ushahidi mwingi.Si kawaida adui kuua mfululizo watoto na akinamama na kuwanyima chakula watu wengine bila adui huyo kushikwa mkono asiendelee na balaa hizo.
Kuanzia sasa hakuna atakayeamini kuwa kuna mataifa ya kidemokrasia ya kuamrisha mataifa mengine yafuate mifuomo yao.
Hakuna atakayekuwa tayari kutekeleza maazimio ya umoja wa mataifa wakati ameona maazimio yote yamekanyagwa na Israel na hakuna hatua iliyochukuliwa.
Hakutakuwa na taifa litakaloamini kuwa kuna jirani yake atamsaidia wakati wa shida anapovamiwa na adui yake.
Mlolongo wa mabadiliko wa tabia za binadamu huko mbele kutajenga zaidi imani ya kumtegemea Mwenyezi Mungu kuliko ilivyokuwa awali.
Kuna matukio chanya ambayo mpaka sasa hayajatokea lakini haitachukua muda mrefu sana yataonekana.Kuna mabalaa yatazikumba nchi ambazo zimeachia uonevu uendelee mbele ya macho yao mpaka zitadhoofika na hatimae tawala zao kuchukuliwa na watu waliokuwa hawakutegemewa kabisa .
Mfumo wa mapinduzi na kujiamini kupambana na wababe ambao umeonekana nchi za Afrika Magharibi utakuwa nidio mtindo wa nchi nyingi ambazo zilikuwa chini ya ukandamizaji wa mabeberu na wanayonyaji wa dunia.
Mwisho wa yote harakati za kuikomboa Palestina na kupomoroka kwa Israel zitapata kasi kutoka mikono ambayo haikufikiriwa kabisa.
Popote vita vya Gaza vitakapoishia basi Israel hatoweza kuitawala nchi pamoja na maeneo ya wapalestina na hatopata tena nguvu za kupambana na wapinzani wengine walio jirani naye kama ilivyokuwa mwanzoni.
Baadhi ya matukio chanya yaliyoanza kuonekana katika ukombozi wa kifikra ni kutambuliwa kwa taifa la Palestina na mataifa mengi japo wanajua mipaka ya taifa hilo imeshavurugwa na Israel.
 
Kubwa Hamas hawawezi kurudia tena huo ujinga
Wangekuwa wamechukua rai yako basi wangenyoosha mikono na kuachia mateka.lakini unaona mwenyewe mpaka leo wanapigana bila kusita.Mungu (Allah) atawainua sehemu waliyokuwa hawakutarajiwa kuonekana.
 
Wangekuwa wamechukua rai yako basi wangenyoosha mikono na kuachia mateka.lakini unaona mwenyewe mpaka leo wanapigana bila kusita.Mungu (Allah) atawainua sehemu waliyokuwa hawakutarajiwa kuonekana.
Mateka wote wamesha uwawa ndugu,neno mateka linatumika na Israel kuhalalisha kuendelea na vita. Na upande wa hamas wanatumia neno mateka kuweka presha kwa raia wa Israel ili Netanyahu asitishe vita kwa kuogopa maandamano nchini kwake na nia ya Hamas ilikuwa IDF isivamie kabsa Rafar maana ukweli utajulikana na kichapo kitaendelea maradufu
 
Mateka wote wamesha uwawa ndugu,neno mateka linatumika na Israel kuhalalisha kuendelea na vita. Na upande wa hamas wanatumia neno mateka kuweka presha kwa raia wa Israel ili Netanyahu asitishe vita kwa kuogopa maandamano nchini kwake na nia ya Hamas ilikuwa IDF isivamie kabsa Rafar maana ukweli utajulikana na kichapo kitaendelea maradufu
Hamas wangekubali kusitisha mapigano kwa kukubali masharti ya Israel wangetuvunja moyo sana kwani wangekuwa wametangaza kushindwa.Lakini mpaka mwisho nia ni kuendelea na mapambano na ndio utekelezaji wa yale matamko tutapigana mpaka tone la mwisho la damu ambalo wengi hushindwa kulitekeleza mambo yanapokuwa magumu dhidhi yao.
 
Hamasi wamefanikiwa maana sasa mataifa yanaitambua palestina kama state huo ni mwanzo mzuri kupelekea utaifa kamili
 
Hamasi wamefanikiwa maana sasa mataifa yanaitambua palestina kama state huo ni mwanzo mzuri kupelekea utaifa kamili
Ni mafanikio makubwa sana.Jana pia Slovenia imepeleka azimio bungeni la kuitambua Palestina,Hao na mataifa mengine ya Ulaya itakuwa wametiwa moyo na moyo wa kishujaa wa kutetea haki yao uliooneshwa na Hamas.
Mfumo wa mazungumzo ya amani umewapa muda sana Israel kumega ardhi za Palestina kutoka mipaka ya 1967.
 
Sisi tunazungumzia nini na wewe unazungumzia nini?.Jaribu kutumia akili yako kuchambua dunia inakoelekea.
Nyie mmezungumzia mengi na yeye amezungumza humohumo. Jaribuni kutumia na nyie akili zenu kuchambua yanayoendelea huko Gaza na sio kutoa blanket statements eti ni kwa dunia nzima. Kuweni focused. Dunia inao wenye akili na wachambuzi zaidi yenu. :KEKBye:
 
Mtaandika sana ila kipigo kiko pale pale, mumezoea kuua Wakristo mkajisahau na kudhani Wayahudi ni Wakristo, wale ni makatili, watawatafuna sana na chuki zenu hizo alizowalisha muarabu.
Wafia dini akina brazaj mjifunze siku nyingine msichokoze Wayahudi.
Kabisa mkuu. Hilo ndo la msingi ila majamaa hayasikii kamwe wamekaza shingo. Acha washikishwe adabu.
 
Hamasi wamefanikiwa maana sasa mataifa yanaitambua palestina kama state huo ni mwanzo mzuri kupelekea utaifa kamili
Mataifa kuitambua huku una ugomvi mkubwa na jirani yako ambaye ana nguvu kukuzidi , usalama wako bado utakuwa hatarini.
 
What if I told you, Hamas ni bawa la kushoto, Israel ni bawa la kulia na ndege mwenyewe anaitwa Zionist.
 
Mataifa kuitambua huku una ugomvi mkubwa na jirani yako ambaye ana nguvu kukuzidi , usalama wako bado utakuwa hatarini.
Hawajaelewa mbinu(cheap popularity) inayotumika hapo eti wametambuliwa na Mataifa. Hawajui kwamba ni Mataifa hayo hayo yatakayotoa hitimisho(Hatma) la mustakabali wao ili kupata hadhi ya kuitwa ni Taifa.
 
What if I told you, Hamas ni bawa la kushoto, Israel ni bawa la kulia na ndege mwenyewe anaitwa Zionist.
Then, tell us how comes that the bird (Zionist) can fly (can exist) while its wings are not coordinated - because the right wing is against the left wing i.e.they are fighting @ other.
Is it true to say that currently Zionist is self terminating?
 
Then, tell us how comes that the bird (Zionist) can fly (can exist) while its wings are not coordinated - because the right wing is against the left wing i.e.they are fighting @ other.
Is it true to say that currently Zionist is self terminating?
Its called Controlled Opposition, basically, they make one side of the government so terrible that people flock to the other side of the government to protect them from the bad side without realizing that they are both on the same side.
 
Its called Controlled Opposition, basically, they make one side of the government so terrible that people flock to the other side of the government to protect them from the bad side without realizing that they are both on the same side.
Mkuu asante; naona hiyo ni Falsafa tata kidogo. Ngoja waseme wabobezi wa hiyo kitu.
 
Mkuu asante; naona hiyo ni Falsafa tata kidogo. Ngoja waseme wabobezi wa hiyo kitu.
Falsafa hii inatumika sana hapa ulimwenguni, mfano wanasiasa wengi ni kama mapambo tu, haijalishi yupo chama gani lakini wenye maamuzi ya kweli yapo nyuma ya pazia na wana control pande zote mbili. (Watawala na wapinzani)
 
Falsafa hii inatumika sana hapa ulimwenguni, mfano wanasiasa wengi ni kama mapambo tu, haijalishi yupo chama gani lakini wenye maamuzi ya kweli yapo nyuma ya pazia na wana control pande zote mbili. (Watawala na wapinzani)
Waw! Kumbe. Nashukuru kwa ufafanuzi Mkuu.
 
Back
Top Bottom