Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kuna jamaa wa Uganda namfahamu naye alikuwa uwanja wa mapambano, anasema kikosi chake kilikua chini ya Kanali Moyo. Inavyoonekana kulikua na makundi tofauti ya wanajeshi wa Uganda waliokuwa begakwabega
na majeshi yetu. Kuna walikuwa chini ya Yoweri K Museveni na wale wa Milton Obote ambao nadhani walikuwa chini
ya Ojok. Tafadhali tupe maelezo kuhusu hawa wapiganaji.
Gen.Tito Okello Lutwa alizaliwa katikakijiji cha Nam Okora wilaya ya Kitgum wakati wa vita vya kwanza vya Dunia mwaka 1914,Kuhusu elimu yake mengi hayajulikani hata hivyo alijiunga na Kings African Rifles(KAR)May 16,1940 kama ilivyokuwa kwa Idd-Amin naye alipigana vita vya Mau-Mau huko Kenya wakiwa upande wa waingereza mwaka 1957.Naongezea hapa alikuwepo pia Tito OKELO.
Historia ya Major-General David Oyite-OjokKuna jamaa wa Uganda namfahamu naye alikuwa uwanja wa mapambano, anasema kikosi chake kilikua chini ya Kanali Moyo. Inavyoonekana kulikua na makundi tofauti ya wanajeshi wa Uganda waliokuwa begakwabega
na majeshi yetu. Kuna walikuwa chini ya Yoweri K Museveni na wale wa Milton Obote ambao nadhani walikuwa chini
ya Ojok. Tafadhali tupe maelezo kuhusu hawa wapiganaji.
Wale mateka wa kutoka Libya na Palestina wote walikabidhiwa nchi zao baada tu ya sherehe Kaboya kuwakaribisha wapiganaji wetu waliokuwa wakipigana huko Uganda.Kuhusu kazi na majina ya Makamanda soma sehemu yangu ya kwanza na ya pili nilielezea labda nielezee wachace tu.Kwani Wale Mateka Wa Kiarabu Mliwapeleka Wapi? Wako Wapi Sasa? Na Vp Kuhusu Majina Ya Utani Ya Makamanda Yalikuwa Na Maana Gani?
Kijeshi si vizuri ku-Under-estimate adui yako maana huwezi jua ana uwezo gani kwenye silaha,mafunzo yao,mbinu zao na nidham za askari wao. hasa majibu yote hutokea kwenye uwanja wa MEDANI mara nyingi sana ingawaje si mara zote watu hutumia udhaifu wa upande wa adui hapo ndipo unaweza kupiga Bao kirahisi sana,Kumbuka pia vita si lelemama au mchezo wa kuigiza once you make any mistake you did great-mistake to you,your family and your country.Mimi binafsi nisingependa sisi kuwa POLISI au VIRANJA dhidi ya majirani zetu.Echolima maelezo yako yanaifanya niongeze imani kwa Jwtz.Vipi mchango wa makomando wetu ulikuwaje?Tunaweza tembea kufua mbele hata kipindi hiki dhidi ya majirani zetu yaani ke,ug,rwanda na malawi?
HISTORIA FUPI YA MAKAMANDA
Mwaka 1978 jeshi letu likuwa na Major General wawili tu, Major General Twalipo (aliyekuwa mkuu wa majeshi wakati huo) na Major General Sarakiya ambaye alikuwa balozi wetu huko Nigeria. Baadaya ya Major General kulikuwa na Mabrigadier sita au saba tu: Brigadier Marwa, Brigadier Musuguri, Brigadier Mayunga, Brigadier Walden, Brigadier Kiwelu, Brigadier Yusuf Himid nadhani na Brigadier Mkisi. Chini ya Mabrigadier kulikuwa na makanali kadhaa ikiwa ni pamoja na akina Moses Nnauye, Abdallah Natepe na wengineo.
Nitaendelea...
Kwa kweli Story za hii vita Vya Kagera huwa zinanisisimua sana tu, Nimesoma kile kitabu cha War In Uganda cha Martha Honey na Tony Avirgan yaani utapenda km unaangalia movie vile. Kuna picha mle za akina Ben Msuya, Mti Mkavu, Oyite Ojok huyu alikuwa kamanda ktk jeshi la ukombozi wa Uganda waliopigana bega kwa bega na majeshi yetu. Nakumbuka vita hivi vinapiganwa mie nilikuwa km na 4yrs tulikuwa Songea, kule kuna kambi kubwa za jeshi basi ikasemekana ndege za Nduli zaweza fika na kupiga kule, mji mzima kila family tukachimba mahandaki ya kujificha, mbaya zaidi mzee wangu alikuwa Polisi upande wa upelelezi, dah nilikuwa naomba mungu tusiambiwe mzee kapelekwa mstari wa mbele! ndege zikipita angani watu wanakimbia kujificha. nakumbuka baada ya vita kwisha askari wengi walirudi Songea mjini basi walikuwa km wamechanganyiiwa hivi na watu waliaswa kutowachokoza. siku moja niko na bro wangu tunakwenda town si nikagongana na soldier akasimama akaniambi mtoto Kaa chonjo kule saa mbaya i nearly did in my pant! hahahaha. Mkuu simulizi zako ziendelee huwa napensa sana jinsi mashujaa wetu walivyomtosa Nduli na kumchakaza vibaya!
Aksante sana RUVUMAN umeongea maneno mazuri sana na ushauri mzuri kwangu nilikuwa najibu tu swali aliloniuliza kuwa ni kitu gani nakikumbuka sana katika Vta hiyo,Najua sana vitani kuna mambo mengine yanatendeka huko si mazuri kwa jamii lakini nitajitahidi sana na staadhiri USALAMA WA TAIFA nitakuwa naongelea tu hali halisi iliyotokea nashukuru kwa maoni yako.