Vita vya Kagera: Historia yangu - Sehemu ya kwanza

Mkuu Echolima

mbali na majeshi ya miguu mlitumia pia majeshi ya majini katika vita hii??

Vipi kuhusu majeshi ya anga nayo yalitumika sana au hatukua wazuri sana upande wa anga??
MFUMO DUME yote hayo nimeelezea katika sehemu ya pili labda tu subiri tu sehemu ya pili nimeelezea kila kitu pamoja na mengine mengi tu.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Nguruvi3, sisi Watanzania tuna problem na serious writers!. Tangu miaka ya 60 UDSM ilipoanzishwa, tumekuwa tukitoa wahitimu wa fasihi, lakini mpaka leo miaka 50 baadae hatuna fasihi yoyote ya maana!. Hadi kesho, kiada na rejea za literature bado kina Chinua Achebe, Ngungi wa Thing'o, Okot P'Bitek etc, where are the Tanzanians?!.

Hivi unajua mpaka leo hata historia ya Uhuru wametuandikia wazungu?!. Waandishi wetu wako wapi ili hali wapigania Uhuru wapo?!. Ndio maana nilimpongeza Maalim Mohamed Said na ile historia ya wazee wake wa Gerezani, japo mauongo mengi!, but he did something!.
Biographies za viongozi wetu tunangoja tuandikiwe na wazungu!.

Hivi unaweza kuamini mpaka sasa leo hapa ninapoandika, hakuna historia rasmi ya TANU iliyoko documented?!. Tenda alipewa Kanyama Chiume (Malawi), alipofariki kabla ya kukamilisha kazi, kazi hiyo imeishia hapo!.

Interview Public and Private Nyerere, ilifanywa once na jarida la African Now, hadi ameondoka nothing more!.
Jumbe is bed ridden, Mwinyi is growing old, Ben anawadharau Watanzania, hutuna simulizi zao zozote!, na wataondoka!.

Licha kukosa wenye uwezo to that job right, sisi wenye interest tupo, but with what resources?.
Niliwahi kuripoti humu kuhusu kuanzishwa kwa kituo cha kuhifadhi kumbukumbu za waasisi wetu.
Pasco
 
Hio usiite vita!
Hio ilikuwa ni fujo tu!
Na ghasia za watu wenye magobole!

Sasa hii ukiita vita na vietnam uite nini!?
Mkuu, hapa umenifanya nicheke sanaaaa. Sikujua kuwa kuwa yale mapigano na Idd Amin yalikuwa ni fujo na ghasia zilizosababishwa na watu wenye magobore! Hebu nipe darsa kiundani niweze kuelewa. Manake mimi na watanzania tulio wengi ile ilikuwa ni vita
 
Hapo Mkuu umepiga mkuki moyoni WE MUST WAKE-UP AND ACT NOW yote uliyoyasema mimi yameniingia sana ni lazima nasi tutende..
 
Mkuu, hapa umenifanya nicheke sanaaaa. Sikujua kuwa kuwa yale mapigano na Idd Amin yalikuwa ni fujo na ghasia zilizosababishwa na watu wenye magobore! Hebu nipe darsa kiundani niweze kuelewa. Manake mimi na watanzania tulio wengi ile ilikuwa ni vita


We kama umecheka basi inatosha!
manake ukichokoa sana hapa, utasababisha afande anitafute na lile gobole lake!!
na mimi kukimbia siwezi!

We kubali tu kuwa hio ya tz na uganda na ile ya Hitler zote zinaitwa vita! Hata sisi zile biscuti ngumuu za jeshi tulikula pia!
Na amin tulimfuata kwake tukamchapa vlvl!

kwa hiyo sina la kuongezea hapo!
 
Ni wanajeshi wangapi wa Tz waliopoteza maisha kwenye vita ya kagera.
Maana nikiangalia kama ulivyoeleza ni kama wachache
 

Taaluma ya uandishi wa vitabu Tanzania ilikufa siku nyingi sana baada ya vita wakati uchumi ulipoanza kuharibika, na watu wakaanza kuwa wanatafuta namna ya kusurvive kwa njia yoyote ile. Kwa hiyo manunuzi ya vitabu yakatoweka kabisa. Ndiyo maana kwa muda mrefu Tanzania imekuwa haina maduka binafsi ya vitabu ispokuwa vile vya kiada tu. Vitabu karibu vyote vya fasihi na riwaya viliandikwa kabla ya mwaka 1980: Musiba (ingawa walikuwa akikopi baadhi kutoka Nick Carter), Kezilahabi, Shaffi, Ben Mtobwa, Katalambula, na wengineo waanidhsi mashuhuri waliandika kabla ya mwaka huo wa 1980. Baada ya hapo kukatokea waandishi uchwara sana hasa pale UDSM waliokuwa wakiandika bila kutumia akili, na vitabu vyao vikawa pia havinunuliwi. Uandishi wa vitabu huchochewa na market, watu huandika vitabu ili vinunuliwe.
 

Nimesoma bila kuchoka!!
 
Ni wanajeshi wangapi wa Tz waliopoteza maisha kwenye vita ya kagera.
Maana nikiangalia kama ulivyoeleza ni kama wachache

Ndugu si rahisi kupata takwimu exactly kwa Vita kama hii ambayo imechua mezi ni ngumu sana labda uongozi wa juu wao wanaweza kutoa ilikuwa rahisi kidogo kama vita ingechukua wiki au siku chache.
 
Ndugu si rahisi kupata takwimu exactly kwa Vita kama hii ambayo imechua mezi ni ngumu sana labda uongozi wa juu wao wanaweza kutoa ilikuwa rahisi kidogo kama vita ingechukua wiki au siku chache.

Kwann takwimu zisipatikane??kwani serikali haijui ilipeleka askari wangapi??na wangapi walirudi waki hai,majeruhi au waliofariki??
 
Kwann takwimu zisipatikane??kwani serikali haijui ilipeleka askari wangapi??na wangapi walirudi waki hai,majeruhi au waliofariki??
Takwimu za vita inategemea unataka kupata kwa wakati gani.
Ni lazima uwe specific kwasababu madhara ya vita yanaendelea hata baada ya vita kwisha.

Kwa mfano, Nyerere alisema katika hotuba yake ya kurudisha askari 'tumepoteza vijana wetu 400'.
Leo makaburi ya Bunazi yana masuijaa 630 kama sijasoksea kwa kauli za JK juzi.

Hata baada ya vita vifo viliendelea kutokana na post war traumatic disorder syndrome (PTSD).
Kwa nchi masikini kama yetu na isiyokuwa na utaratibu ni ngumu kujua wangapi wali commit sucide, wangapi walifariki kutokana na majeraha ambayo hayakupata matibabu sahihi, wangapi walipatwa na matatizo kwa chanzo chake kikiwa ni vita n.k. katika wakati huo wa vita na hata miezi michache baadaye.

Na pengine chombo ambacho kingeweza kutoa japo takwimu zinazokaribiana na ukweli ni JWT.
Sidhani Echolima au askari mwingine anaweza kuongea kwa usahihi, nadhani ni swali gumu sana let us be fair
 
Kwann takwimu zisipatikane??kwani serikali haijui ilipeleka askari wangapi??na wangapi walirudi waki hai,majeruhi au waliofariki??
Takwimu zenyewe zipo na serikali ndiyo walizozitoa mimi nilikuwa nasema kama mimi siwezi kupata takwimu hizo labda Uongozi wa juu ndio unaweza kutoa lakini kama nilivyosema inakuwa ngumu sana kuzitoa kwa mtu binafsi.
 
WELL-DONE Nguruvi3 ni kweli kabisa uliyoyasema kwenye sehemu yangu ya tatu nimeongelea sana kuhusiana na PTSD ambayo naweza kusema imeua askari wengi sana waliotoka Vitani askari aliyekuwa akikumbwa na PTSD wanakufa sana na ikumbukwe kwa nchi kama yetu haikuweza kukundua hili.
 
Kuna huyu afande mstaafu wa JKT alikuwa anaitwa Brigedia Gen Stanslaus Msilu yeye hakupigana vita hii Echolima.
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…