Vita vya Ukraine; Wasichotuambia wazi

Vita vya Ukraine; Wasichotuambia wazi

Putin mwenyewe alitumia hadaa ya "special operation", kama tujuavyo special operation huwa shughuli ya siku chache, unapiga mabomu kwenye maeneo ya kimikakati kisha unatimiza lengo lako na kugeuza, kwa mfano angeishia kumega maeneo yanayomuunga mkono kisha maisha yaendelee.

Lakini badala ya special operation, amefanya full-scale military invasion, hata wanajeshi wengi wa Urusi walipigwa na butwaa maana hawakutegemea iwe hivi, waliokamatwa wote wanasema hilo moja kwamba hawakua wameandaliwa kisaikolojia wanakwenda kuvamia Ukraine mazima mazima, na kunao wanalia sana.

Uvamizi huu ungefaulu pakubwa kama rais wa sasa wa Ukraine angekua bonge la dikteta, wananchi wangepokea wanajeshi wa Urusi kwa vifijo na nderemo, ila sasa kidemokrasia Ukraine inaizidi Urusi, hivyo hapa inabidi kupambana dhidi ya raia wa Ukraine na wanajeshi wake. Unapovamia nchi inayotawaliwa na dikteta huwa rahisi, kwa mfano Tanzania ilipovamia Uganda, Waganda wengi hawakua wanamtaka Id Amin, walishukuru sana na kuna wengi walijiunga kwenye mapambano wakiwemo maelfu ya waasi waliokua wanaongozwa na Museveni na Tito Okello.

Putin kwenye huu ugomvi utamgharimu sana nje na nyumbani, pia ikumbukwe Ukraine na Urusi wana undugu, sio rahisi kwa wanajeshi wa Urusi kujitolea kizalendo hadi kufa kama walivyofanya dhidi ya Hittler. Ni kama leo hii Tanganyika iwatume wanajeshi kuvamia Zanzibar wafanye mauaji huko, wale Wazanzibari asilimia kubwa ukiondoa Waarabu, wengi ni Watanganyika waliovuka maji aidha enzi za utumwa au hivi majuzi, kila Mzanzibari mweusi ana asilia ya Tanganyika, utakuta ukifuata ukoo wake palipo makaburi ya mababu zake utakuta ni huko Unyamwezini, Usukumani n.k.

Urusi leo hii imepoteza hadhi hata kwa mataifa ya Uarabuni ambao hununua sana silaha zake, wengi wapo kimya wakishangaa hii aibu.
Umelishwa matangopoli mpaka akili imeamia kunako, rais wa Ukraine ni rais wa michongo amewekwa kimkakati na marekani. 2014 marekani aliandaa kundi na kuanzisha fujo kubwa sana ndani ya Ukraine mpaka rais aliyekuwa madarakani kidemokrasi kuachia ngazi. USA wakamsimika kiongozi wa kimichongo na haya yanayotokea sasa ndio zao la chokochoko za USA
 
Umejaza maneno ambayo sijayasema, labda huna uwezo wa kuelewa haya mavitu iwe najisumbua bure.


Kwa mujibu wa maelezo yako; mkataba ni makubaliano yaliyotiwa saini mbele ya mashahidi kama hakuna saini na mashahidi hayo ni makubaliano tu na yanawezwa kuvunjwa "kiholela" au sio??!
 
Kwa mujibu wa maelezo yako; mkataba ni makubaliano yaliyotiwa saini mbele ya mashahidi kama hakuna saini na mashahidi hayo ni makubaliano tu na yanawezwa kuvunjwa "kiholela" au sio??!

Soma nilichokisema herufi kwa herufi uje upya.....
 
Putin hajaitkisa dunia, kama vipi ameonyesha namna Urusi ilivyo dhaifu, wengi tulijua huu mchezo ataumaliza ndani ya siku tatu, leo wiki zimepita, ameingiza wanajeshi 120,000 Ukraine bado hawajafaulu kuiteka Kiev, wanajeshi wengi hivyo ni gharama hadi tumeshuhudia wanaiba vyakula kwenye maduka, njaa imeanza kuwatafuna.

Leo hii Putin ameanza kuwafuta kazi majenerali Putin awafuta kazi majenerali nane na pia agombana sana na taasisi y ujasusi ya FSB
Unavyoongea kwa madaha huku umebinua kichuguu! nakukumbusha tu kuna dude linaitwa Bulava yaani Lutin akibofya kitufe unaweza jikuta na mimba bila kujali jinsia
 
Putin
20220226_172241.jpg
 
Soma nilichokisema herufi kwa herufi uje upya.....


Hichi ndicho ulichosema:-

Makubaliano huwa hayana uzito kihivyo, na mataifa mengi duniani yana makubaliano, uruhusu niingize kwako sukari na mimi nitaruhusu uuze kwangu kuku na maisha yaende, tukubaliane usijiunge kwenye muungano fulani ila na mimi kama fadhila nitakulinda au hata kukusaidia kiuchumi.
Sasa ukifika mahali upate ukakasi kwenye hayo makubaliano unayatupa kuleee!!!!!



Kama hicho ndicho ulichosema, sasa inakuaje umlaumu Russia kumtwanga Ukraine ??!!
 
Hichi ndicho ulichosema:-





Kama hicho ndicho ulichosema, sasa inakuaje umlaumu Russia kumtwanga Ukraine ??!!

Hadi pale utaacha uzembe usome kila nilichokisema, na urudie mara kadhaa, hautakaa uelewe kitu, tutazungushana humu hadi Putin aje mwenyewe kukutuliza.....ha ha ha!!!!
 
Tanzania iivamie Mombasa nchini Kenya maana sehemu kubwa wanaongea Kiswahili fasaha.
 
Hadi pale utaacha uzembe usome kila nilichokisema, na urudie mara kadhaa, hautakaa uelewe kitu, tutazungushana humu hadi Putin aje mwenyewe kukutuliza.....ha ha ha!!!!


Hadi na wewe utakapoacha kuandika pumba zinazokufunga wewe mwenyewe na kukufanya uanguke mweleka usijue ni nani aliyekuangusha ndipo utaelewa kwamba Zelensky alipandikizwa na NATO ili avunje makubaliano na Russia kihuni ndipo naye Russia kaamua kumtwanga Kihuni, dawa ya moto ni moto, sasa wewe unalalamika nini??!!, au hadi Zelensky aje akupashe habari ya uhuni aliotaka kumfanyia Russia ndipo ujue??!!
 
Achilia mbali Ukraine hata Tanzania hapa hakuna anayeweza kuja na kuteka nchi yetu kwa siku mbili!! Kumbuka kuwa ndege na makombora huwa hazina uwezo wa kuteka nchi, bali jeshi la nchi kavu hususan askari wa miguu!! Kwa ngazi ya askari wa miguu hakuna tofauti kubwa ya nguvu na ujuzi miongoni mwa mataifa!! Ujue pia kuwa huwezi kuangamiza askari wengi kwa kutumia ndege na makombora. Hivyo huangamiza majumba, raia na miundombinu lakini si wanajeshi na silaha zao za mkononi!! Wewe piga mabomu lakini wako kwenye mahandaki wanakusubiri uingie mitaani!!! Ndiyo maana Marekani kawashindwa kabisa Taleban hadi kumwaga manyanga mchana kweupe!! Hali kadhalika hata Urusi yenyewe haitegemei kufikia lengo lake la kuipokonya silaha Ukraine kwa siku chacge tu! Hapa ni miezi kadhaa kama siyo miaka kadhaa!!
Pa1 sana mkuu. Hii vita imekuwa na vimitego vingi. Kwa mfano wanafunzi na raia wa kigeni kuzuiwa na kubaguliwa nahisi ndicho kilichomfanya putin apaki matanki nje ya mji akingoja watu wasepe... Hawa wanaodai mrusi kalegea angechukua ndani ya siku mbili tatu hawaangalii kwa jicho lingine. Angerush ina maana kulipua hata wabongo walioko huko
 
Hadi na wewe utakapoacha kuandika pumba zinazokufunga wewe mwenyewe na kukufanya uanguke mweleka usijue ni nani aliyekuangusha ndipo utaelewa kwamba Zelensky alipandikizwa na NATO ili avunje makubaliano na Russia kihuni ndipo naye Russia kaamua kumtwanga Kihuni, dawa ya moto ni moto, sasa wewe unalalamika nini??!!, au hadi Zelensky aje akupashe habari ya uhuni aliotaka kumfanyia Russia ndipo ujue??!!

Ha ha ha!! Ustadhi nafikiri nimeelewa shida yako, na ndivyo mlivyo kote kwa sasa mnafikiri Putin yupo anawasaidia kukomoa Marekani, wenye dini yao waarabu kwenye hili wamenyamaza kimya, maustadh wa Bongo ndio hamkamatiki.
 
Mlizima channels za Russia ili mtulishe matangopoli. Mmechelewa sana. Nani kakudananya mrusi a apigana vita Ukraine?? Kaishasema mala nyingi tu kuwa anafanya operation ndogo tu ya kijeshi.
Amka utakunya bure kitandani kumekucha... imagine huziamini habari za channel tofauti na za Russia ila unaamini matamshi kuwa kinachoendelea Ukraine sio vita..hujioni na wewe ni boya kuamini habari za upande flani ukiwa nanjilinji bila kuwa na ushahidi wowote?

Sent from my TECNO CD6j using JamiiForums mobile app
 
Ndoa mkishaachika kila mmoja achukue hamsini zake haipaswi kupangiana, Zanzibar wakiachana na Tanganyika, haipaswi Tanganyika aanze kumpangia Zanzibar eti asiungane na Oman.
Marekani aligoma Urusi kuweka silaha zake Cuba, kwa kisingizio Cha Usalama wake
 
Marekani aligoma Urusi kuweka silaha zake Cuba, kwa kisingizio Cha Usalama wake

Marekani hakufanya uvamizi Cuba, aliishi kwa ugomvi na Castro kwa miaka yote lakini hakuna hata siku moja aliivamia Cuba kijeshi.
Putin hakutumia akili, kwanza hapo Ukraine ilikua rahisi sana kwake yeye kupandikiza maana wote ni ndugu, unacheza propaganda fulani hivi mpaka wananchi wote wa Ukraie wanakuelewa na kuchukia Marekani, sasa kwa kuwapiga makombora amefeli vibaya mno.
 
Marekani hakufanya uvamizi Cuba, aliishi kwa ugomvi na Castro kwa miaka yote lakini hakuna hata siku moja aliivamia Cuba kijeshi.
Putin hakutumia akili, kwanza hapo Ukraine ilikua rahisi sana kwake yeye kupandikiza maana wote ni ndugu, unacheza propaganda fulani hivi mpaka wananchi wote wa Ukraie wanakuelewa na kuchukia Marekani, sasa kwa kuwapiga makombora amefeli vibaya mno.
Marekani hakufanya uvamizi Cuba, aliishi kwa ugomvi na Castro kwa miaka yote lakini hakuna hata siku moja aliivamia Cuba kijeshi.
Putin hakutumia akili, kwanza hapo Ukraine ilikua rahisi sana kwake yeye kupandikiza maana wote ni ndugu, unacheza propaganda fulani hivi mpaka wananchi wote wa Ukraie wanakuelewa na kuchukia Marekani, sasa kwa kuwapiga makombora amefeli vibaya mno.
Hivi hujui Ukraine tayari ilikuwa na silaha nyingi kutoka nchi wanachama wa NATO na kuwa tishio kwa majimbo yanayotaka kujitenga ya Luhansky na Donestky? anachofanya Putin, ni kuziondoa silaha zote hatari nchini Ukraine..kuhakikisha Ukraine inakuwa dhaifu kijeshi, kitu ambacho mpaka sasa kafanikiwa kwa 100%, hii operation ikiisha, Ukraine itakuwa haina tena ubavu wa kutisha majirani zake kijeshi.
 
Hivi hujui Ukraine tayari ilikuwa na silaha nyingi kutoka nchi wanachama wa NATO na kuwa tishio kwa majimbo yanayotaka kujitenga ya Luhansky na Donestky? anachofanya Putin, ni kuziondoa silaha zote hatari nchini Ukraine..kuhakikisha Ukraine inakuwa dhaifu kijeshi, kitu ambacho mpaka sasa kafanikiwa kwa 100%, hii operation ikiisha, Ukraine itakuwa haina tena ubavu wa kutisha majirani zake kijeshi.

Sijui utakua unafuata taarifa zipi maana naona umepotoka unaposema Urusi amefanikiwa 100%
Urusi amejiingiza kwenye kwenye vyumba visivyokua na milango ya kutokea, Putin amechanganyikiwa mpaka ametishia kutumia nyuklia maana hali inazidi kuwa mbovu, silaha zinaingizwa Ukraine kwa maelfu, na pia maelfu ya wapiganaji wanaendelea kutiririka Ukraine, vifaru vyake vinalipuliwa na kuondoshwa kama karanga, wanajesh na majeneral wake wanauliwa hadi hatari, nyumbani uchumi unaendelea kuangukia pua, ingia kwenye mitandao uone Warusi wanavyochukia balaa.

Hadi ameweka sheria ya kukamata Mrusi yeyote atakayepinga hivi vita au kulisemea mabaya jeshi lao. Amekua kama mwehu....

Mataifa yote ambayo hununua silaha kutoka Urusi yakiwemo ya Waarabu yamepigwa na butwaa, hawaamini macho yao kwamba waliyemtegemea ameonyesha udhaifu mkubwa sana.
 
Ha ha ha!! Ustadhi nafikiri nimeelewa shida yako, na ndivyo mlivyo kote kwa sasa mnafikiri Putin yupo anawasaidia kukomoa Marekani, wenye dini yao waarabu kwenye hili wamenyamaza kimya, maustadh wa Bongo ndio hamkamatiki.


Hapa hatuzungumzi kuhusu dini bali kuhusu Uhuni wa Zelensky kwa Russia na jinsi Russia inavyojibu huo uhuni.
 
Back
Top Bottom