Vita ya Vinywaji...

Ni kweli meku sere lite kamkaba koo vibaya castle lite, K vant nayo kwa sasa inakimbiza kwa kasi wengi wanasema haiachi harufu kali mdomoni hata ukikesha nayo unaamka asubuhi kama umekunywa pepsi...
Tumuite mdau Mshana Jr aje na tathmini yake
Hiyo ya kaharufu nimeisikia kwa wengi... Nyagi ukiigonga asubuhi mdomo unatoa harufu kama choo cha bar...
 
Ni kweli meku sere lite kamkaba koo vibaya castle lite, K vant nayo kwa sasa inakimbiza kwa kasi wengi wanasema haiachi harufu kali mdomoni hata ukikesha nayo unaamka asubuhi kama umekunywa pepsi...
Tumuite mdau Mshana Jr aje na tathmini yake
Pombe ni dhambi jamani acheni, imeandikwa ole wake ampae mwenzie kilevi. Tena ole wake aamkiae kilevi.
 
Kawaida kila kinywaji kipya (masanga) kinakuja na kishindo chake. kwenye haya mambo yetu ni sawa tu na pale baa au club mpya inapofunguliwa, utadhani zingine hazifai.
Serengeti lite anapita tu, atapotea wakati ukifika. Castle lite ni chuma kile, hata kikijikongoja kwa sasa lakini kitabakia.
K Vant hauwezi mziki wa Nyagi. Konyagi ina wanywaji wake bwana. wanywaji wa kvant ni waigizaji tu, tena tunaweza sema ni waonjaji tu. Wanywaji wa ukweli wanaiheshimu na kuitukuza konyagi. Amini nawaambieni itafikia kipindi KVant atabaki historia.

Kwenye ulabu bwana mkongwe siku zote atabaki mkongwe na sifa yake itadumu. Balumi, japo si kongwe lakini huwezi kuilinganisha na Pilsner. Japo Pilsner ni ya kitambo lakini ni bia tofauti kabisa na balimi. ni sawa na kulinganisha bamia na kitunguu.

Angalia, kuna bia kama safari, Castle lager, Ndovu, nk ni za kitambo na bado zinatamba. zipo zitakozokuja na zitakazoondoka au kufifia, mkongwe anabaki na hashima yake milele.

Agggggh! wacha niwahi maeneo nikajipoze na safari+peck za nyagi (mambo ya bia na tera lake). Leo katikati ya wiki nitakuwa grocery tu ................... wadau wenzangu tunaopafahamu natangulia mie
 
Mzee baba we utakuwa umekunywa maji ya bendera ya TBL... hahahaha

Huko bar Castle lite zimekuwa kama mapambo wallah
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…